CCM malipo ya DOWANS.....''NO''

CCM malipo ya DOWANS.....''NO''

Acha kuwa na akili za kushikiliwa CCM ndiye nani hapa???JK+Pinda au huyo mpayukaji Nape

mgomo palepale sijui watafanyaje lazima nape arudishe ile takrima kwa waandishi wa habari..
 
NAPE ni mtu au Kampuni ya Kuzalisha maneno, kila kukicha neno jipya na waandishi tele. NAPE kilefu chake ni New Ambush Pure Engine, kwa kuchonga ajambo siku 90 zimeisha ili kaliacha karukia jingine
 
ilianza ccm;
DOWANS lazima ilipwe by CHILIGATI

ikaja CHADEMA;
mukiilipa dowans tunaandamana.

ikaja ccm tena;
musiandamane hatilipi tulikuwa tunatania tu.
MY TAKE:nchi inaongozwa na chadema ndo maana chadema inachosema ccm na serikali inafuata.mia
 
Nawaomba wanaharakati na watanzania wote wenye nia njema na nchi hii wajitahidi kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa maandamano kwa maendeleo endelevu ya taifa letu lililojaa uozo wa kila aina, kwa sababu naamini wengi wetu (hasa vijijini) kupata taarifa inakuwa ngumu sana na inachukua muda.
 
Na hapa, Nape tena, huyu jamaa kwanini asiwe mtangazaji wa Jahazi, ashirikiane na kibonde, pale clouds atoe matamko yake mpaka kipindi kiishe.
 
Wanazunguka mbuyu hao, haiwezekani mazuri yawe associated na CCM halafu mabaya ya serikali yasiusianishwe na CCM. Nao saizi wanaipinga mahakama!
Hata na mimi ninashangaaaaa, au wanataka wafanye hivyo kuonyesha nao inawakela ili kupunguza munkali wa wana-arakati ktk kudai haki ya msingi.
 
Yeah, CCM watakuwa kwenye maandamano kuishinikiza serikali isiilipe Dowans, kiongozi wa maandamano ni m/kiti CCM taifa Jk! Umesasau wakati wa kikao cha NEC CCM iliilalamikia serikali kwa kupandisha bei ya mafuta?

Mmh.! JK mwenyewe gamjui huyo mmiliki wa dowans, ila watanzania wanamjua.! A SMART GOVT SHOULD KNOW EVERYTHNG HAPPENING WITHN THE COUNTR, JK' GOVT DOESNT KNOW ALOT OF THINGS.!
 
CCM kupitia msemaji wake ambaye anakaribia kupoteza umaarufu wa jina la baba yake Nape Nauye akiongea na TBC1 amesema CCM hawatambui uamuzi wa mahakama kuu kwa kubariki na kuridhia Tanesco kuilipa DOWANS.
source: habari kwa ufupi TBC1 saa 10
Kwani hao si ndio wanajitapa kuwa wanafuata utawala wa sheria. Sasa inakuwa hawatambui maamuzi ya mahakama, tena mahakama Kuu!
 
navuta picha ya huo U-DC aliopachikwa na mkuu wa kaya,ni afadhali jamii imemtambua jinsi alivyo...kama angeendelea kuwa dc,hiyo wilaya sidhani kama ingekuwa na dc me ata simuelewi huyu jamaa..shame on him
 
Natoa angalizo ccm hawaaminiki wanabadilika kama kinyonga huyo vuvuzela nape ili aone watu watalichukuliaje, tunataka kauli ya kikwete
 
Haya miujiza inaendelea, ni kama macho ya mtu mmoja, la kulia linaona green la kushoto linaona red. Total confusion and anarchy.
 
Yaani hapa unataka kuniambia kuwa CCM hawataki serikali ya CCM iwalipe CCM (mafisadi)
 
Ukitaka kuwawin watz 2015 ni kuwa na ela lukuki za kununua fulana na tshirt bila kusahau khanga
Na ela za Dowans ndo starting capital kwa ajili ya izo kazi

ELA!ndo nin mkuu?
 
Ndo kusema CCM wanajaribu kukimbia kivuli chao sio?mazuri ya serikali ni ya ccm na mabaya yanabki kwa serikali.kwli ccm kwishenei!!
 
ilianza ccm;
DOWANS lazima ilipwe by CHILIGATI

ikaja CHADEMA;
mukiilipa dowans tunaandamana.

ikaja ccm tena;
musiandamane hatilipi tulikuwa tunatania tu.
MY TAKE:nchi inaongozwa na chadema ndo maana chadema inachosema ccm na serikali inafuata.mia

masaburi yanakuwasha.chaga development manifesto wanakuongoza wewe sio watanzania.
 
good start for us....kama tutakuwa pamoja kuipinga serikali ya ccm na wana ccm wakiwa ni among protesters then i m sure we will win the battle ila kama ni janja ya nyani pia tutajua ila nijuavyo mimi dogo katumwa kupuliza upepo ajue unaelekea wapi...tutaanza kwa kupinga malipo ya dowans then rais wa nec simple
 
Back
Top Bottom