CCM kwisha kabisa

CCM kwisha kabisa

Dah maskini Tanzania yangu…kwa nn viongozi hawana upeo mkubwa hivi? Mpaka sasa hivi kosa la gwajima ni lipi? Ameshauri…ameonya…ameomba majibu…kama mtanzania lakin kwa nn wanapuuza hoja zake ambazo ni za kweli?
Kosa lake ni kumfunga paka kengele
 
Yaani speech moja tu ya kada wake kuishauri mamlaka ya juu... Wote wamejaa kwenye mfumo wake

Tangu juzi siku moja bada ya speech yake iliyowakonga nyoyo Watanganyika wengi... Makada, chawa kunguni na viroboto wanashindana mitandaoni na kwenye press conference za mchongo kumjibu
Kujibu sio tatizo je wanajibu nini?

Mipasho
Kejeli
Matusi
Vitisho
Mipasho
Mazonge yake ya nyuma
Mpaka sasa hakuna hata mmoja aliyejitokeza kumpongeza na kumshukuru kwa uthubutu mkubwa aliouonesha.. Kila anayenyanyua kinywa chake anatoa boko lake kumzidi mwenzake

Wanapofanya hivi wanadhani wanamfurahishq rais kumbe ndio wanazidi kumharibia, kumbe ndivyo wanavyozidi kukifanya chama kizidi kuchukiwa

Ndani ya saa 48 Gwajima amesjageuka shujaa na staa kuliko mwanzo

Naye anasafiria upepo huo.. Anadonyoa donyoa hapa na kule.. Na kila anapodonyoa anahakikisha anatoa kitu chenye maana, miongozo na maono mbalimbali kuhusu Tanganyika😂
Tulipofeli

Tulipokosea

Tulipoharibu na nini tunatakiwa tufanye nini kwenye nini kuondokana na mikwamo ya muda mrefu😂😂😂😂
CCM watafute haraka mtu mwenye hekima wa kuwajibu hawa wanaomjibu Gwajima la sivyo atazidi kujijenga binafsi huku akizidi kukibomoa chama chao chakavu mahututi kilichojichokea na kukongoloka kabisaView attachment 3347706
Ninachoamini ni kwamba kusudi la Mungu linaendelea kutimia.
 
Uzuri ni kwamba mboga mboga hata wao wanajua kama hawapendwi,hata hawa wanaosifia humu ni unafiki tu na njaa..ila deep down hata wao wanajua Kuna mambo hayako sawa..ila watafanyaje na ukizingatia njaa na msimamo havikai pamoja!
 
Mkuu shida sisi watanganyika hatuwezi kuamka na kudai nchi yetu kwa umoja
Na njia ni rahisi sana haiitaji hata kwenda barabarani...ni kwamba siku ya kupiga kura kila mtu anaamka na kuendelea na shughuli zake...hakuna mtu kuelekea kwenye foleni ya kura.....watawala watachanganyikiwa.
 
Nyie @tcra_tanzania kwanini mnazuia media zisiripoti press ya Askofu Gwajima? Na zile zilizoripoti kwanini mnalazimisha zifute? Kama maudhui ya Gwajima yana shida, si aitwe polisi kuhojiwa?

Pamoja na mambo mengine, Gwajima ameongelea issue ya watu kutekwa/kupotea. Hivi nyie hamuoni hilo ni tatizo? Hamuoni taarifa mitandaoni watu kudaiwa kutekwa na kupotea? Yuko wapi Mdude? Yuko wapi kijana aliyechoma picha ya Rais? Yuko wapi Erick Msyaliha? Yuko wapi Daniel Chonchorio?

Gwajima amesema ana orodha ya watu zaidi ya 80 waliotekwa/kupotea mwaka huu. Hivi nyie hamshtuki? Watu 80+ kwa miezi minne? Kumbuka hao ni walioripotiwa. Je, ni wangapi hawajaripotiwa au hawana umaarufu?

Taarifa hii ilitakiwa iwashtue na mtoe ushirikiano ili watu hao wajulikane walipo. Mtoe mawasiliano yao ya mwisho ambayo yangeonesha waliwasiliana na nani kabla ya kupotea.

Lakini badala ya kufanya hivyo, nyie mnazuia maudhui ya Gwajima yasichapwe. Hivi kati ya hao waliopotea, wangekuwepo wafanyakazi wa TCRA, mngezuia maudhui yasichapwe? Ndio maana Gwajima akauliza, hivi mnadhani nyie ndio binadamu peke yenu, wengine ni mbuzi? Mpaka apotee mtoto wa nani ndio muone hili ni tatizo?

Cha ajabu, Gwajima amekemea utekaji, nyie mnazuia habari zake zisiandikwe, lakini wale wanaomjibu wakisema utekaji umekuwepo tangu enzi za Nyerere, mnaruhusu habari zao zichapishwe. Hivi mnataka tuwaeleweje? Kwamba mnaunga mkono utekaji au?

Halafu mnadhani mkizuia "mainstreams" ndo mmedhibiti habari isisambae? Hayo ni mawazo mgando. Imeshaenea nchi nzima, kwa sababu inahusu maisha ya watu. Kwa hiyo, nakupeni pole. Mmechelewa sana.

Bibi yangu kule Tarakea (95) aliposikia roho za watu 80 hazijulikani zilipo, ameumia sana. Ameanza Novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia kukemea watekaji. Nimemuomba aunganishe na watumishi wa TCRA wanaozuia habari za utekaji zisichapwe. Kwa hiyo, subirini matokeo.

Na nyie waandishi mnaozuiwa kuripoti, msifikiri mko salama. Kumbukeni alitekwa Azory Gwanda, mwandishi mwenzenu, na hadi leo hata mfupa wake haujaonekana. Kufyata mkia ni kuungana na watesi. Siku mkitekwa, hakutakuwa na wa kuwapazia sauti. Chagueni leo kusimama na umma. Kuweni sauti ya wasio na sauti. Kila mtu ana haki ya kuishi!
FB_IMG_1748368238131.jpg
 
Ni mtu asiye na akili tu,ndie atashindwa kufananisha hawa nyoka wa kijani na shetani,kiroho nyoka wa kijani ni ishara uharibifu wa ustawi,hawa wanatimiza hiyo kazi ya uharibifu hata wa maadili.
 
Mbunge anasema eti martha Karua naye angebakwa.. Unajiuliza ndio sasa iweje? Chama cha majinga tuu
Unasema kweli, au unatania mkuu. Mbunge katamka hivyo hivyo Bungeni; ni mbuge gani huyo?
 
Ndiyo ushangae na jiwe akiwepo. Leo hii hawa ndiyo wamsumbue wanajichosha tu. Gwaji ni zaidi ya tunavyomuona kwa macho ya nyama. Ndiyo mtu pekee nchini kayasemea maovu ya utekaji na mauaji akiwa nchini na bado yupo.
Mm huo napenda kusema... haya majamaa yenye uwezo wa kukusanya watu maelfu Kwa maelfu, yanawaseti kwa kuwauzia maneno ya matumaini yakitumia biblia, na watu hao wanamimina hela za kutosha huku majamaa yanakuwa mabilionea...hivyo vichwa sio vya kawaida! Ni binadamu wenye akili nyingi sana! Hata lile jamaa la pale packers sio la kawaida! Lile jamaa la kawe kila mkoa linapotua lina nyomi kama mafuriko ya lowasa!
 
Kuna mpango ninawaza nifanye kwa maeneo niliyiyopo.

Nataka kudowload audio yote ya speech ya MNEC Gwajima kisha niende kwenye yale maeneo wanalusha movie na audio wale wa mtaani wanapiga mziki mkubwa kwa sauti. Niwalipe waweke hiyo audio kwa kurudia masaa mawili elfu 40.
 
Ubwabwa, maharagwe na mchuzi pembeni.Mpishi amepiga kanga moja tu mkishakula mnaenda chumbani mnakitendea haki chakula.Mpishi ameshachoma sindano ya uzazi ya miezi site.Utakata kiuno hadi kiwiliwili kijitenge
Hakuna alama inayofaa kwa mchango kama huu, imebidi niweke tu hiyo ya "kicheko"

'Hakika 'mabutu1835' alikuwa mbali sana kiakili na mada hii!
 
Kuna mpango ninawaza nifanye kwa maeneo niliyiyopo.

Nataka kudowload audio yote ya speech ya MNEC Gwajima kisha niende kwenye yale maeneo wanalusha movie na audio wale wa mtaani wanapiga mziki mkubwa kwa sauti. Niwalipe waweke hiyo audio kwa kurudia masaa mawili elfu 40.
Ni wazo zuri.
Hata hizi juhudi za "Bila Marekebisho, Hakuna Uchaguzi", yanaweza kufaidika sana na mpango kama huo ukiratibiwa vizuri.

Siyo muhimu "kurudia rudia kwa masaa", unawezakupangwa kiustadi zaidi, kwa kuingiza vidokezo mbalimbali katikati ya kila kipande cha hotuba yenyewe; na inaweza kuwa ni kwa wiki nzima, kila siku kipande maalum.

Wafikishie ujumbe wataalam wa CHADEMA waufanyie kazi.
 
Back
Top Bottom