Uchaguzi 2020 CCM kumtumia Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete mikoa ya Kusini Wananchi waonesha furaha

Kwani Kikwete si ndiye aliyepeleka jeshi Mtwara kwa ajili ya gesi ya Msimbati? Jiwe, akawanyang'anya korosho zao. Unadhani kuchekewa huko ndio kumesafisha mioyo yao wakati walitendwa na hao hao? Wenyeji wa kusini wanahitaji mfariji na mfariji hawezi kuwa mtesi wao.
Mtu anapeleka korosho yake ghalani anaambiwa arudishe iko chini ya kiwango. Huo usumbufu unadhani ni mdogo? Subirini mpewe na nyie haki yenu. Kama vipi mkawapige shangazi zao ili wawape kura zote.
Mfariji ni yule anaye wapelekea malinda kutoka uberigiji?
Au ni wale wanaofukuza waandishi wa habali wakati hawajawakodi huku wakisema wanatetea vyombo vya habali.
 
Mfariji ni yule anaye wapelekea malinda kutoka uberigiji?
Au ni wale wanaofukuza waandishi wa habali wakati hawajawakodi huku wakisema wanatetea vyombo vya habali.
Ndio maana TAL anataka watu wafundishwe lugha. Ndio umeandika nini sasa. Malinda; uberigiji ndio majitu gani hayo. Mtu kama wewe ndio ccm ikiwaona wanafurahi kweli kweli. Maana ndio oksijeni yake.
 
Mikoa ya kusini nayo imetelekezwa kama kaskazini ndio maana kusini kapelekwa kikwete na kaskazini kaenda Majaliwa.
Nini bhana miaka 5 itaisha na awamu hii itaondoka na makandokando yake, awamu ijayo sidhani kama itakuwa na sera za 'migawanyiko ya kikanda' kama hii
 
Yaani Kiwete huyu aliyewapelekea Jeshi watu wa kusini na kufanyiwa ukatili wa kila aina ndo apendwe huko?

Kikwete aliyewaweka ndani Masheikh ndo apendwe na watu wa kusini ambapo waislamu ni wengi sana?

Ngoja Wapinzani waanze kampeni ya bampa to bampa huko mikoa ya kusini watakumbushwa yote hayo!
 
Kwani jiwe anaogopa kwenda kule!
Hahahaha. Mna utani nyie.
Kwa hiyo km hataenda watu wa mtwara kwani hawajui kua anawakimbi?!
Yaani mtu akukimbie usijue kua anakukimbia?!
 
Wenyeji wa kusini wanahitaji mfariji na mfariji hawezi kuwa mtesi wao.
[/QUOTE Mkuu huu mstari una busara kubwa japo mimi si mccm ila uko sahihi sana ingawa wananchi wa kusini bado wataona Kikwete anamtetea mtesi wao hivyo kusema ni wale wale.
 
Back
Top Bottom