GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Wanabodi, tulileta ushauri hapa JF sisi wana CCM tunaojitambua ni hatua gani za kufanya mikoa ya Kusini mwa Tanzania hasa Lindi na Mtwara. Tulishauri mikoa hiyo atumike Mama Salma Kikwete kuweka mambo sawa kuhusu korosho. Tulishauri Majaliwa waziri mkuu asitumike huko kabisa.
Uamuzi wa CCM kumtumia Mama Salma Kikwete ambaye ni mzaliwa wa huko na kumuongeza Rais Mstaafu Kikwete kuzindua kampeni ni karata kubwa sana.
Tulishauri kwenye uzi huu Uchaguzi 2020 - CCM inapaswa kuchukua hatua na kujibu hoja: Je, Maisha ya wananchi yameboreka kwa miaka mitano iliyopita?
Hivyo basi, nampongeza Kikwete kwa kuanza kuhubiri maendeleo ya watu na sio vitu huko Lindi kwenye uzinduzi wa kampeni, watu wengi wana hali ngumu kimaisha.
Kikwete amejaribu kwa uwezo wake leo huko Lindi kupooza machungu ya gesi na korosho kwa njia ya kidiplomasia zaidi na kwa kutumia lugha laini ya ushemeji shemeji kwani ameoa huko Lindi.
Siasa za kuongelea maisha ya watu hasa Bima za Afya, Ajira ndio hatua kuu ya kujibu na kubomoa hoja za Tundu Lissu. Kwa maisha yalivyo mioyoni mwa watu bila kuwahubiria uchumi binafsi ni dhahiri CCM tutachakazwa sana kwenye kura. Ushahidi wa maisha magumu ni watu jinsi hata furaha hawana, shamra shamra za ngoma na sherehe za kuchangiana kwa mapesa sasa hali ni hovyo.
Napongeza chama changu kwa kuzingatia ushauri hapa JF, tutaendelea kushauri kwa nguvu na uwezo wetu ili CCM ishinde.
Uamuzi wa CCM kumtumia Mama Salma Kikwete ambaye ni mzaliwa wa huko na kumuongeza Rais Mstaafu Kikwete kuzindua kampeni ni karata kubwa sana.
Tulishauri kwenye uzi huu Uchaguzi 2020 - CCM inapaswa kuchukua hatua na kujibu hoja: Je, Maisha ya wananchi yameboreka kwa miaka mitano iliyopita?
Hivyo basi, nampongeza Kikwete kwa kuanza kuhubiri maendeleo ya watu na sio vitu huko Lindi kwenye uzinduzi wa kampeni, watu wengi wana hali ngumu kimaisha.
Kikwete amejaribu kwa uwezo wake leo huko Lindi kupooza machungu ya gesi na korosho kwa njia ya kidiplomasia zaidi na kwa kutumia lugha laini ya ushemeji shemeji kwani ameoa huko Lindi.
Siasa za kuongelea maisha ya watu hasa Bima za Afya, Ajira ndio hatua kuu ya kujibu na kubomoa hoja za Tundu Lissu. Kwa maisha yalivyo mioyoni mwa watu bila kuwahubiria uchumi binafsi ni dhahiri CCM tutachakazwa sana kwenye kura. Ushahidi wa maisha magumu ni watu jinsi hata furaha hawana, shamra shamra za ngoma na sherehe za kuchangiana kwa mapesa sasa hali ni hovyo.
Napongeza chama changu kwa kuzingatia ushauri hapa JF, tutaendelea kushauri kwa nguvu na uwezo wetu ili CCM ishinde.