CCM ivunjike tu


CCM itavunjika hilo halina shaka. Unachochangaya hapa ni matokeao ya kuvunjika huko. Huo mvunjiko upo kwa pande mbili. Upande wa kwanza utakuwa na NGUVU NA MAMLAKA kuliko CCM ya mwanzo. Upande wa pili utakuwa CCM iliyopitwa na wakati.

Awamu ya 5 iko mikononi mwa CCM yenye Nguvu na Mamlaka yaliyoirudishia Uasisi na Uasili Wake. Hali Halina UBISHI.
 

The Boss nimemnyooshea concept yake. Na kumuonyesha UIMARA WA CCM ulipo.

Na kusema kweli UKAWA haiwezi kupuuzwa kwenye ujenzi wa Demokrasia Ya Taifa Tanzania. Naiheshimu UKAWA kwa pressure na ufuatiliaji ulioifanya CCM kuwa kwenye Sura mbili ambapo moja inachukua Uongozi wa Taifa Tanzania.
 
Last edited by a moderator:

Uwezekano wa Wa Kutokea CCM moja nzito yaye Heshima na Mamlaka yenye Nguvu kuliko UKAWA na CCM Lowasa UPO. Na hiyo ndiyo ya kuchukua Uongozi.
 
Typical statement from a dead man walking, at least this much I expected! Maybe you didn't say it in so many words, truth is you implied it and that is even worse; you don't even have the courage to do so plainly. Tatizo ni kwamba wanafiki mko wengi. Mara ngapi swali linajitokeza humu likiuliza hao wapinzani wamefanya nini, mbona wameshindwa kutimiza ahadi zao, kwa nini wanapenda kulia lia. Wakiandamana wakipinga, wakashambuliwa na polisi, wakapigwa wakaumizwa na hata wengine wakauawa, mpo watu mtakaowabeza mkidai wameyataka wenyewe. Shame on you people!
 
T Analysis yako ni sahihi. Wote wameamua kukomalia humo humo iwe kwa woga au kiburi. Tatizo hata wakikubaliana baadaya uteuzi wa wagombea bado kutabaki makundi. Chama kitaendelea kuwa na matatizo makubwa zaidi maana ni afadhali adui aliyeko nje kuliko adui wa ndani. Makundi yaliyoko ndani na ya kisiri yanasumbua aidi kuliko yaliyoko nje na dhairi. Kwa vyovyote vile ni shida, wampitishe Lowassa au wasimptishe!
 

Mkuu kama nchi yetu HAIITWI Tanzania basi maandishi mekundu yana ukweli. Lakini kama inaitwa Tanzania basi umepotoka kabisa. Nakuuliza.. hao viongozi na wanachama wenye uwezo na uthubutu wa kufanya vurugu ni kina nani?
 
Mzee Mwanakijiji wewe ni team mdmu tunakujua ila kwa taarfa yako na uweke kwenye diary yako 1995 Abdulrahman Kinana na Anna Makinda walitoa machozi lowasa alipowatangazia kua ameamua kujitoa kugombea urais na kumuunga mkono kikwete wakiamini lowasa amekosea ebu mwanakijiji na midimu wenzako jiulize machozi ya kinana yalifutika lini mpaka amchukie lowassa mnacheza ngoma msiyoijua na kna nape bahati nzuri mangula anaijua ndio maana anachoma na kupuliza ila.si kikwete wala.mangula wenye uwezo wa kumzuia lowasa kugombea urais take it from me.
 
Last edited by a moderator:
Uwezekano wa Wa Kutokea CCM moja nzito yaye Heshima na Mamlaka yenye Nguvu kuliko UKAWA na CCM Lowasa UPO. Na hiyo ndiyo ya kuchukua Uongozi.
Na wewe The President, tatizo lako ni kwamba unadhani unaielewa CCM lakini kulingana na post yako naona huielewi na huijui CCM. CCM wameweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu moja, umoja wao na uwezo wao katika kulindana na kuteteana pale wanapokabiliwa na utata. Kama unafuatilia malumbano ambayo mara nyingi yangehatarisha umoja wao, huwa wanaitana na kuwekana sawa na kutoka hapo wakiwa wamoja.

Uchafu hufagiliwa hadi mvunguni kwa sababu kila moja anatoka hapo akijua mapungufu ya mwenzie na hakuna wa kumnyooshea kidole mwenzake hadi pale litakapozuka tafrani nyingine. Unakumbuka walivyoenda kumtafuta Mang'ula kule kijijini alipokuwa analima nyanya? CCM ilikuwa inachungulia kaburi, magamba yamekwama kiunoni huku Nape akipita huko na huko akiropoka...waliyamaliza kwa maazimio, maazimio ya kufunika kombe.

Maazimio ya kulindana ndio dawa kwa CCM na leo hii akipita Lowassa, tofauti zote ndani ya CCM zitaisha na ataungwa mkono na wale wale wanaomtupia madongo. Hiyo ndiyo CCM, chama kinachoishi kwa ulaghai na nguvu za dola; watamtoa wapi huyo msafi asiye na doa? Jaribu kukaa chini ufikirie huyo atakayeteuliwa na CCM halafu, Mungu atupishilie mbali, awe Raisi wa awamu ya tano, atapambana vipi na wenziye ndani ya CCM?
 
Mzee Mwanakijiji

Tatizo kubwa sana nilionalo mimi Watz wengi sana mnafananisha CCM na KANU na kwamba kilichotokea kwa KANU basi kitatokea CCM hilo haliwezekani!
CCM SIYO KANU!
Mazingira ni tofauti kabisa, Kenya na TZ tuko tofauti sana na sababu kubwa ni hii!
Kenya siasa ni Mtu na ndio maana KANU ilivunjika kwa maana Wananchi wanafwata Mtu, hapa kwetu siyo hivyo Siasa siyo Mtu bali ni Chama hivyo leo hii Mtu yoyote yule maarufu CCM pmj na Lowasa mwenyewe kama akitoka CCM hakuna atakayemfwata na huo ndio utakuwa mwisho wake!

Na hii ni kwa sababu hakuna kitu ambacho kitamfanya Mtz awe tayari kufa kwa ajili ya binadamu mwingine tofauti na Kenya au nchi nyingine wana siasa za Ukabila hivyo kama kwa mf. Raila akiwa KANU basi wajaluo wanaona wana muwakilishi KANU hivyo kama akitoka ni rahisi kufanya propaganda na kuwadanganya Wajaluo kwamba anaonewa na Wakikuyu na hivyo Wajaluo wote wanafwata kwa maana wanaona kama wanatea Kabila lao vivyo hivyo kwa Wakikuyu au sijui Kalenjili sasa hilo TZ halipo hivyo Lowasa akitoka kesho CCM ambacho ni chama Dola watamtumia TAKUKURU watamtafungulia mashitaka na watamfunga kabla ya Uchaguzi na HAKUNA kitu yeye (Lowasa) au wafuasi wake watafanya sana sana wataingia brn. mara moja Serikali watapiga risasi wawili watatu na wengine hawataona umuhimu wa kufa kwa ajili yake kwa maana hakuna bond ya aidha Ukabila au udini zaidi ya siasa hivyo hakuna aliye tayari kufa kwa ajili tu ya siasa hiyo ndiyo tofauti!

Ukitaka kuielewa CCM angalia Chama cha kikomunisti cha Uchina au Komunisti ya Urusi hivyo ndivyo vyama ambavyo CCM imefwata muundo wake na siyo KANU, hivyo na Urusi hakuna mwenye uwezo wa kuitoa Chama cha Putini madarakani hata iweje labda ije Vita Kubwa sana lkn siyo kwa Kura na sababu ni moja tu kama ilivyo CCM ni Chama Dola!

Kumbuka ukubwa wa madaraka ya Raisi wa JMT ambaye ndiye Mkubwa wa CCM, Kikwete ana uwezo wa kuahirisha uchaguzi na hakuna kitu Mtz yoyote yule anaweza kufanya, anaweza kubuni tu kwa kutumia Usalama wa Taifa hali ya hatari na kila kitu kwisha, anaweza kukifuta CHADEMA kesho na hakuna kitu CHADEMA watafanya zaidi ya kwenda kulia kwa Wazungu ili waikemee CCM, hivyo yoyote yule kwenye makundi ya CCM analijua hilo, kwani Amrani kombe yuko wapi si alipigwa risasi live na hakuna kitu Mtu alifanya?

Haya ndio mambo (Katiba Mpya) ambayo Upinzani walipaswa kupigania kwenye katiba Mpya, Madaraka ya raisi, kofia mbili lkn wapi walikuwa busy kudai haki ya Mtz Bara kuishi Zanzibar akina Tundu Lisu wakaishi kumtukana Nyerere na kusifiwa kwenye Majukwaa lkn mambo ya muhimu wakayapuuzia, hivyo CCM itabakia Madarakani hata Miaka 50 ijayo labda nguvu za nje ziingilie na hilo kutokea ni lazima Wazungu waone maslahi yao yako hatarini!
 
Last edited by a moderator:

mkuu Mag3, watu nchi hii bado sana kwenye eneo la ukombozi wa kifikra....what's even more dismaying ni kuona kuwa ukombozi huu wa fikra kumbe bado unahitajika hata kwa watu "wenye vidato" vyao ambao tulitegemea wawe ndiwo crusaders. pathetic.

kuna mchangiaji mmoja kwenye uzi huu hapo juu amemjibu huyu bwana kuwa afadhali ya pengo kuliko jino bovu...a sobering answer to a slumbering retard!

anyways, historia inatufundisha kuwa watu wa aina hii watakuwepo daima...kama ilivyokuwa wakati Mwl Nyerere alipokuwa anigania uhuru - kuna wasomi wa wakati ule walitaka mkoloni ang'olewe lakini bado walitia shaka kuhusu mbadala (huku wakijua fika kuwa Mwalimu was already there at the helm of it all)
 

CCM ife hata leo, tuanze upya. Shida kubwa ya matatizo tunayokumbana nayo tanzania ni mfumo ambao CCM wameutengeneza.
 
Kifo cha nyani miti yote huteleza ndivyo ilivyo kwa utawala hakuna njia za kuzuia kuondoka madarakani.
-wakimpitisha Lowasa kuwa mgombea uraisi kupitia ccm UKAWA tunashinda asubuhi kabisa
-wasipompitisha Lowasa kugombea lazima ccm ipasuke vipande vipande kutokana na makundi .
CCM imeshavunja siku nyingi sana sema itamalizikia rasmi 12.07.2015
 
Lowasa hatiishi ccm kama unavyodai, ila amejua wezi wapo wengi wamejifa kwenye jina lake wakitaka kumtoa kafara, kama ccm ni chama makini kwanini lowasa hakufukuzwa uanachama?

CCM wote ni wezi, wanatafuta mtu wa kulinda wizi wao. Sitegemei kiongozi imara toka CCM kwasababu hakuna kiongozi anayeweza kuongoza system ambayo ni corrupt kutoka levels za juu hadi chini.
 
lowassa hawezi kuhama ccm...akienguliwa atakaa kimya....tatizo kubwa ni huyo mweyekiti wao..

CCM ambayo viongozi/wanachama matajiri walikuwa hawahami ni ile ya kabla ya 95-ile iliyomdhibiti Kolimba. CCM ya sasa inapungua nguvu, ndio maana viongozi wanaanzisha chama(CCJ) wakiwa bado ndani ya CCM. CCM ya zamani iliyokuwa na ubavu, Lowassa asingeanza 'kampeni' mapema kama anavyofanya, maana wanahitajika wadhamin 450, yeye ana laki 8, na anaendelea kuwakusanya. Ni kweli anawatishia CCM kuwa ana kundi kubwa nyuma yake, wasiwasi wangu ni kuwa ameshaanza kuamini kuwa kweli atashinda hata nje ya CCM. Vurugu zinaweza kutokea kwasababu kila mwanachama sasa ana sharubu kama ukoo wa Kambale. Heshima ya Mwenyekiti iliyokuwepo zamani, haipo tena. Naamini, bila kuwa na FFU nje ya ukumbi wa mikutano, si NEC wala Mkutano Mkuu utakaofanyika.
 
CCM usalama wao upo katika kuvua Gamba baada ya hapo watakua lmara sana kuwahi kutokea,

Tatizo liko kwa UKAWA kushindwa kutengeneza MoU mpaka sasa jinsi watakavyo gombea Urais na Ubunge na jinsi watakavyo gawana hicho watakachopata.

Replacement inatakiwa UKAWA watuthibitishie kama wako tayari siyo kukaa kimya kungoja CCM wamkate Lowasa na Mzee wa Makengeza.

Ukitazama katikati ya kauli ya Kinana wako tayari sasa kuvuana Magamba hilo halina shaka.
 
Nafunga na kuomba jina la Lowassa likatwe tuone mikwara yake itaishia wapi. Mtu mmoja fisadi na mwizi hawezi kutishia watu wazima kana kwamba chama ni chake.

Hatuwezi kuongozwa na rais fisadi.

Ccm kwa lowasa wanalo mwaka huu wakimkimbia mshale wakimchukua mkuki yaani wana boonge la soo waamue kukumbatia moto uwachome au wauzime upepo uueneze kwingine sijui watauzimaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…