Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
Wapo watu ambao hufurahi wanaposifiwa kwa kila jema na zuri watendalo. Hili ni jambo zuri tu. Pia, wapo ambao huwa hawapendi sifa hata kama wakifanya mambo makubwa na mazuri. Hawa ni wachache. Kwa wenye busara, unaposifiwa sana lazima ujiulize. Ya kweli haya? Maana, ngoma ikivuma sana hupasuka.
Unaposifiwa, lazima uangalie anayekusifia na kwa lipi? Nitatoa mfano, wanasiasa kama Yusuf Makamba, Abdulrahman Kinana, Lusinde Kibajaji, Joseph Msukuma, Lameck Madilu Nchemba, na wengine wanaotetea matumbo yao wanapokusifia ujue unapaswa kulaumiwa.
Imekuwa jambo ambalo sasa linakera sina mfano kila mwana CCM kumsifia mama hata pale asipostahili. Nashangaa ni kwanini mama anakubali kusifiwa hata bila kustahiki. Tujikumbushe usifiaji ulipovuka mipaka pale Profedheha Kabundi alipomuita Mwendazake Magufuli akimsifu kwa kumtoa kwenye jalala wakati alikuwa kwenye nafasi nzuri na ya heshima chuo kikuu alichokigeuza kuwa choo kikuu kwa upofu na uroho wake.
Kwa wanaofuatilia mijdala bungeni na kwenye maeneo mengine, wabunge, karibia wote wa CCM humsifu na kumshukuru mama baada ya Mungu na wengine kusahau hata kumshukuru Mungu.
Je hii inatufundisha nini? Inaweza kufundisha yafuatayo:
Mosi, kuwa kuna viongozi wanaopenda kusifiwa hata wasipostahiki,
Pili, kuwa wanasiasa wengi ni wababaishaji na wachumia tumbo,
Tatu, kuwa sifa hizi si za kweli na stahiki bali wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili wamtumie.
Nne, kuwa kusifiwa ni jambo la hatari na hovyo. Nani alitegemea kuwa Mwendazake angegeukwa tena hata kabla ya mwili wake kuoza. Laiti angefufuka leo, huenda angebakia na Bashiru Ally peke yake kati ya wale wengi waliozoea kumtukuza na kumsifia naye akaridhika asijue ni umalayaa wa kisiasa.
Tano, kuwa ni wachache wenye hekima wanaopenda kukosolewa na kuchukia kusifiwa upuuuuzi. Rejea maneno ya Job Ndugai. Alisema bila kumung'unya kuwa Tanzania itakuja pigwa mnada. Je sasa tunafanya nini? Nani anamsifia hata kumshukuru Ndugai kwa kuliona hili?
Sita, kuwa wapo viongozi wanaopenda kusikia wanachotaka kusikia ila si kile wanachopaswa kusikia. Wako vizuri na kusikiliza uongo na mapambio ya kijinga badala ya ukweli na busara vinavyouma na kuwasuta ili wajirekebishe.
Je ni vibaya kuwashauri CCM watangaze rasmi kuwa kusifia nayo ni sera yao mpya ambayo italindeleza taifa japo kwenye sintofahamu hasa kutokana na kuchukia ushauri?
Unaposifiwa, lazima uangalie anayekusifia na kwa lipi? Nitatoa mfano, wanasiasa kama Yusuf Makamba, Abdulrahman Kinana, Lusinde Kibajaji, Joseph Msukuma, Lameck Madilu Nchemba, na wengine wanaotetea matumbo yao wanapokusifia ujue unapaswa kulaumiwa.
Imekuwa jambo ambalo sasa linakera sina mfano kila mwana CCM kumsifia mama hata pale asipostahili. Nashangaa ni kwanini mama anakubali kusifiwa hata bila kustahiki. Tujikumbushe usifiaji ulipovuka mipaka pale Profedheha Kabundi alipomuita Mwendazake Magufuli akimsifu kwa kumtoa kwenye jalala wakati alikuwa kwenye nafasi nzuri na ya heshima chuo kikuu alichokigeuza kuwa choo kikuu kwa upofu na uroho wake.
Kwa wanaofuatilia mijdala bungeni na kwenye maeneo mengine, wabunge, karibia wote wa CCM humsifu na kumshukuru mama baada ya Mungu na wengine kusahau hata kumshukuru Mungu.
Je hii inatufundisha nini? Inaweza kufundisha yafuatayo:
Mosi, kuwa kuna viongozi wanaopenda kusifiwa hata wasipostahiki,
Pili, kuwa wanasiasa wengi ni wababaishaji na wachumia tumbo,
Tatu, kuwa sifa hizi si za kweli na stahiki bali wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili wamtumie.
Nne, kuwa kusifiwa ni jambo la hatari na hovyo. Nani alitegemea kuwa Mwendazake angegeukwa tena hata kabla ya mwili wake kuoza. Laiti angefufuka leo, huenda angebakia na Bashiru Ally peke yake kati ya wale wengi waliozoea kumtukuza na kumsifia naye akaridhika asijue ni umalayaa wa kisiasa.
Tano, kuwa ni wachache wenye hekima wanaopenda kukosolewa na kuchukia kusifiwa upuuuuzi. Rejea maneno ya Job Ndugai. Alisema bila kumung'unya kuwa Tanzania itakuja pigwa mnada. Je sasa tunafanya nini? Nani anamsifia hata kumshukuru Ndugai kwa kuliona hili?
Sita, kuwa wapo viongozi wanaopenda kusikia wanachotaka kusikia ila si kile wanachopaswa kusikia. Wako vizuri na kusikiliza uongo na mapambio ya kijinga badala ya ukweli na busara vinavyouma na kuwasuta ili wajirekebishe.
Je ni vibaya kuwashauri CCM watangaze rasmi kuwa kusifia nayo ni sera yao mpya ambayo italindeleza taifa japo kwenye sintofahamu hasa kutokana na kuchukia ushauri?