CCM inaogopa watu, isiwaudhi

CCM inaogopa watu, isiwaudhi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,972
Reaction score
16,621
Miji ni michafu sana, biashara kila sehemu kila aina. Shagalabagala kila kona kasoro Ikulu tu. CCM wanadhani kwa kufanya hivi itaepuka lawama la wananchi kumbe ndio inabeba lawama.

Raia mwenye akili timamu anajivunia kitu kizuri na safi kama vile masoko, mashule, barabara zilizopangika.

Shaghalabagala hii ni dalili kuwa serikali na CCM wanaelekea kubaya sana. Kitu ambacho CCM haikijui ni kwamba wanaofanya biashara holela na kucgafua mitaa sio wapiga kura, hawana muda wa kupiga kura.
 
Na bidhaa feki kushamiri kwenye biashara hizo zenye vurugu nyingi nalo ni tatizo
 
Miji ni michafu sana, biashara kila sehemu kila aina. Shagalabagala kila kona kasoro Ikulu tu. CCM wanadhani kwa kufanya hivi itaepuka lawama la wananchi kumbe ndio inabeba lawama.

Raia mwenye akili timamu anajivunia kitu kizuri na safi kama vile masoko, mashule, barabara zilizopangika.

Shaghalabagala hii ni dalili kuwa serikali na CCM wanaelekea kubaya sana. Kitu ambacho CCM haikijui ni kwamba wanaofanya biashara holela na kucgafua mitaa sio wapiga kura, hawana muda wa kupiga kura.
Si wamejiajiri? Si hiyo ndiyo secta isiyo rasmi? Kama ambayo ccm inaamini kwamba bodaboda ni ajitira ndivyo ambavyo inapaswa kuamini kwamba biashara holela mjini ni ajira pia
Unani wewe chawa tulia ccm Ina wenyewe, wewe ni mwenyewe ai chawa
 
Si wamejiajiri? Si hiyo ndiyo secta isiyo rasmi? Kama ambayo ccm inaamini kwamba bodaboda ni ajitira ndivyo ambavyo inapaswa kuamini kwamba biashara holela mjini ni ajira pia
Unani wewe chawa tulia ccm Ina wenyewe, wewe ni mwenyewe ai chawa
Mtu kutoka nje ya nchi akifika leo tz atajua kuwa tz kuna ombwe la utawala kwa kuangalia tu namna barabara zetu zilivyo chafu na kusongwa na wafanyabiashara kila pahala na mitaa ilivyo shagala. Ni rahisi sana kuporwa pochi yako na mtu ambao utashindwa kumkimbiza kutokana na msongamano.

Serikali imeshindwa kuanzia mwenyekiti wa kitongoji, mtendaji wa mtaa hadi Waziri mkuu huko juu kuwaambia watu hapa usifanye buashara. Mbona nchi nyingine wanaweza? Hapa kwetu serikali inawaza uchaguzi muda wote.
Hawajui kuwa hawa wanaosongamana barabarani na masokoni ndio wanaochoma moto maduka ya wengine na masoko ili ama wakose wote au waanze upya kugawana nafasi baada ya soko kujengwa upya. Hawa wanaosongamana ndio ambao ni rahisi kushawishiwa kuandamana kupinga serikali, nk
 
Mbagala kumejengwa mwendokasi...good move.

Ila sasa hiyo barabara ya lami ya kupita magari mengine, ni kama inatumika nusu tu kwani nusu nyingine yote ni stendi ya madaladala, bajaj, bodaboda na utitiri wa wafanyabiashara wa matunda na vyakula vingine, uchafu uliotelekezwa n.k
 
Back
Top Bottom