CCM imepigwa kitu kizito kisogoni

CCM imepigwa kitu kizito kisogoni

Hii nchi wapinzani(chadema) hawapo serious kbsa.. Wenyewe kazi yao ni kubishana twitter..

Siku mbowe akifariki au ikijitoa kabsa chadema.. Itakufa kifo cha mende..

Mbona vya vipo vingi, mbona chadema tu?
 
Nakubaliana na wewe kwamba walioifanya CCM kwenda ICU ndiyo wameeudi Chini ya upole wa mama SSH.
Ccm inaenda kuwa dhaifu lakini si dhaifu kufikia udhaifu wa upinzani.

Wapinzani bado hawajaweza kushawishi wapiga kura.
Wanacheza ngoma ya watawala. Wamekuwa ni kikundi cha kusubiri ccm kafanya nini na ndiyo watoke kusema.

Wapiga kura wanataka kusikia vitu tofauti kutoka kwa wapinzani.
Mwenyekiti wa CCM anapoteuwa Tume yote ya uchaguzi na kutumia watumishi wa umma aliowachagua na kuwateua kwenye halmashauri unategemea wafanyeje?

Hivi kura zinapoporwa kwa mtutu wa bunduki wapiga kura wameshawishiwaje?

Tume ya uchaguzi inapokata majina ya wagombea wa upinzani kuna uchaguzi gani kwa mpiga kura?
 
Labda ubunge sawa ila sio nchi

Wewe Ni Mungu hadi ujue kesho?. Nani alijua Kinana atakuwa Makamu Mwenyekiti kutoka kupewa adhabu?. Leo Membe kasamehewa. Waliomtukana Magufuli kwenye simu ndio mawaziri leo. Usijipe nafasi ya umungu.
 
CDM badilikeni acheni Uanaharakati....!

FANYENI SIASA, tambueni mahitaji halisi ya mlala hoi na jinsi gani ya kusolve..!

2025 ni Kama Kumsukuma Mlevi ...!
Iwe kwa Katiba mpya au hii hii...iwe Kwa Tume mpya au hii hii ...

Muuza mihogo ukimwambia andamana Dai KATIBA Mpya haielewi.

Lakini ukimwambia bei ya mafuta Kukaangia mihogo itashuka ukinichagua ujue umempata..!

Mtu wa Kawaida Ukimwambia 'tozo la miamala' hatuambiwi tena Zimekusanywa shin ngapi ? Na Zinaenda Wapi? Anaelewa. Amkeni Amkeni!

Lile Genge la 'Wahuni' limesusiwa Chama. Mnataka nini tena?
Tanzania inahitaji chama kipya. Chenye maslahi ya dhati, mikakati na dhamira thabiti kwa Watanzania wote.

Chama kitachowaunganisha Watanzania wote wa vyama vyote, makabila, dini, kanda, maskini, matajiri wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima na wamachinga, mama ntilie nyuma ya maslahi ya wengi, maslahi ya Taifa.

Kwa sasa hatuna chama kama hicho. Vyama vyote kwa sasa vipo kwa ajili ya maslahi yao, (Narrow interest) na sio kuipigania Tanzania na Watanzania kwa ujumla wao.
 
Wewe Ni Mungu hadi ujue kesho?. Nani alijua Kinana atakuwa Makamu Mwenyekiti kutoka kupewa adhabu?. Leo Membe kasamehewa. Waliomtukana Magufuli kwenye simu ndio mawaziri leo. Usijipe nafasi ya umungu.

Uko Umungu na ushetani vyote vinaweza kufanya haya uliyo yasema.
 
Kuna familia ambazo inabidi tukubaliane kama Taifa zipigwe marufuku kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi maana tumeshaona namna walivyo na uchu wa madaraka na kutaka kujibinafsishia hii nchi kama mali binafsi.
 
Ccm hii inakwenda kuiimarisha upinzani kama ilivyozoeleka na kama inavyotakiwa kuwa. Wapondaji wataongezeka, watukanaji, wale wa kusema serikali hii ni dhaifu na wale wa nchi hii haina raisi wataongezeka na kuwa wengi. Si kwa sababu hawakuwepo ila ni kwa sababu ccm hii ilipumzishwa kwa muda na sasa imerudi.

Mbona upinzani ulikuwepo. Umesahau kwa Mara ya kwanza Kuna kiongozi aliminiwa risasi. Upinzani ulikiweopo mkubwa tu sema, ulizimwa kwa nguvu ya dola.
 
Vyama vya upinzani huu ni wakati wa kujipanga na si kuvuruga. Njoeni na sera zinazotekelezeka si sera shikizi. Wananchi wanatamani na wapo tayari kufika katika nchi ya ahadi.
 
Ccm kamwe haitakaa itoke madarakani labda uvunjike yenyewe huu ni ukweli mchungu ambao hamtaki kuusikia


Na ndio maana nimeachaga kupiga kura

Acha propaganda. Wewe unadhani wanaodai katiba mpya na Tume huru Wana maana gani?
 
Tanzania inahitaji chama kipya. Chenye maslahi ya dhati, mikakati na dhamira thabiti kwa Watanzania wote.

Chama kitachowaunganisha Watanzania wote wa vyama vyote, makabila, dini, kanda, maskini, matajiri wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima na wamachinga, mama ntilie nyuma ya maslahi ya wengi, maslahi ya Taifa.

Kwa sasa hatuna chama kama hicho. Vyama vyote kwa sasa vipo kwa ajili ya maslahi yao, (Narrow interest) na sio kuipigania Tanzania na Watanzania kwa ujumla wao.

CCM ndio chama pekee ambacho kimetawala nchi hii tangu enzi. Kwanini uviingize vyama vingine?. Acha unafiki, kura mnaipa CCM halafu lawama mnataka kuvipa vyama vingine.
 
Kuna familia ambazo inabidi tukubaliane kama Taifa zipigwe marufuku kugombea nafasi yoyote ile ya uongozi maana tumeshaona namna walivyo na uchu wa madaraka na kutaka kujibinafsishia hii nchi kama mali binafsi.

Nani wakuwapiga marufuku.
 
Mnao itwa Wabunge wa vimemo tieni vichwa venu maji tayari kwa kunyolewa. Stefu Nyerere amewasaidia sana kuelewa wako wanao wangonga ndani ya CCM. Ukweli ikifika 2025 hamtapata mwanya kugombea ndani ya CCM. If mmeamua siasa iwe kazi yenu mtafute jinsi mtakavyo tetea ubunge wenu nje ya CCM kabla hamja chelewa.
 
Ni Suala la muda mfupi ujao, haya niyasemayo yatadhihirika huko site.

CCM ya wanyonge imepigwa kitu kizito na CCM ya mtandao. Hili sio la kuogopa kusema,labda Moderators wanifanyie yao kwa kuuondoa uzi huu.

Ila ukweli utabaki kuwa ukweli.

Kwa hii safu yenu mpya,
mmeingizwa chaka na walewale walioshindwa kulivua gamba.

Walewale walioiacha hadi ikaingia ICU.

Hakuna kipindi CCM itaishi kwa unafiki baina ya wanachama wenyewe kwa wenyewe kama sasa.

Ni vigumu kusema CCM haitagawanyika kuelekea 2025.

Mnaweza kubaki na raisi asiye dhibiti bunge la jamhuri.
Maana wabunge 75% ni ngumu kurudi bungeni.

Wapinzani mngekuwa makini,hiki ndio kipindi muhimu mrudi site kujijenga.

Tokeni huko mijini mje kuongea lugha ya wapiga kura na kero zao.

CCM hii ya mama na Kinana kwa mtindo huu wa majibu ya jazba kwa wananchi.

Kama tume itasimamia haki...CCM 2025 ni ngumu sana kutoboa.

View attachment 2170598View attachment 2170601
Ccm ishindwe kutoboa dhidi ya nani hasa?
 
Back
Top Bottom