CCM ikubali kuwa imetengeneza Taifa la Wamachinga hivyo iendelee kulilea kwa uangalifu mkubwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,975
Natoa tu angalizo kwamba hili taifa la Wamachinga limetengenezwa na ilani ya CCM huku Wakuu wa Wilaya na Mikoa wakishindana kutoa kwa wingi Vitambulisho vya Mjasiriamali.

Ghafla tena Wakuu wa Wilaya wale wale wanaanza kuwakana wamachinga kwamba wanafanya biashara barabarani na maeneo yasiyoruhusiwa.

Angalizo langu ni kuwa hawa wamachinga, bodaboda na bajaji limeshakuwa kundi kubwa lililooteshwa kama "uyoga" hivyo linahitaji akili kubwa kulidhibiti.

Wakati wanapewa vitambulisho kwa lazima ilijulikana kabisa kwamba wapo barabarani, tusisahau hilo.

Kazi Iendelee!
 
Muko mwatengeneza problem kishapo mwaitafutia suluhu, this time around mumeboil pakubwa mazee
 
Si mlikuwa mnapita barabarani mkijidai ni viongozi wa wanyonge, mkatengeneza mazingira kila mtu awe mnyonge ...... Mlichokuwa mnakitafuta mtakipata
 
Back
Top Bottom