CCM Igunga wafyekana mapanga kugombea pesa

CCM Igunga wafyekana mapanga kugombea pesa

Nape na mwenzio Mwigulu hiyo mifedha ya kifisadi mnayogawa kama pipi itawatokea puani nyie hayeni tu
 
pole kwa bint aliyebakwa jamani maisha yanawafanya watu wanakuwa wanyama?mungu ibariki tanznaia ibariki igunga.
 
ndiyo maana kuna umuhimu wa kuangalia pia maana halisi ya majina ya vyama vya siasa kwa mfano.....Chama Cha Mapinduzi (ccM)wanapindua nini?.....wanapindua reaslimali za taifa kuwa za mafisadi?......halafu kinaitwa chama cha wakulima na wafanyakazi kivipi wakati wafanyakazi wananyongwa kupitia kodo kubwa iliyokithili na inayosababishwa na uvivu wa kufikiri wa watawala wetu...cha wakulima kivipi wkt wanapandisha bei kipindi cha kampeni tu ili wapate kura?...........Chama Cha Magamba (CCM), Chama Cha Mafisadi (CCM)-all are meaningless...........kUNA majina mazuri bana....Mfano Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHANDEMA)-vey meaningful...kwa hiyo vyama vingine tunapochagua na haviteni km tunavyotaka kn CCM ni matokeao ya kutofuatilia itikai zao kikamilifu.......................
JAMANI ONDOKENI KWENYE MAPINDUZI YA RASILIMALIU, ONDOKENI KWENYE MAFISADI, ONDOKENI KWENYE MAGAMBA NJOONI KWENYE MAENDELEO NA DEMOKRASIA YA KWELI...AU NINYI HAMTAKI JAMANI?...MUNGU AWAPE NINI SANA....,AGAMBA ZAIDI?.....MAFISADI ZAIDI.....MAPINDUZI ZAIDI? SEMENI HAPANA INATOSHA
 
Hakuna haja ya kuifurahia na kuishabikia habari hii. Mtu muungwana angeanza kwa kutoa pole kwa majeruhi kabla ya kushangilia watu kukatana mapanga. Uzalendo wetu uko wapi sasa kama tunafikia hatua ya kushangilia watu kuuana?
 
Na wapambe wngine wajiitao green gurd wanaendelea na makambi ya mazoezi ili kufanya nini jamani, wanatangaza vita na nani?
 
zote hizo ni taarifa. kwa vyombo vya ulinzi na usalama, wanatakiwa kuwa makini. mtu ana taarifa, halafu unamwacha aendelee kuitangaza bila kumakamata na kumhoji anazitoa wapi taarifa. huu ni uzembe kwa polisi, uhamiaji na usalama wa taifa.

Inaelekea Polisi na Usalama wa Taifa wana taarifa hizi vizuri, ila sasa wafanyeje wakati inabidi walinde maslahi wanayoyajua/ wanayoyakusudia.
 
"CCM Igunga wafyekana mapanga kugombea pesa". maoni yangu hiki kichwa cha habari kimekekaa kisiasa zaidi, je kuna uthibitisho kwamba uyo mkataji na mbakaji aliangusha kadi ya CCM kwenye harakati zake na kujua kwamba ni mwanachama wa CCM? au ndio siasa za uchaguzi unafanya umakini wa uwandishi uwekwe kapuni?Kwenye matukio kama haya siasa ziepukwe ili sheria ifuate mkondo wake.
 
  • Kada wa CCM ajeruhiwa kwa panga, bintiye abakwa

KADA wa CCM, Francisco Msalika amejeruhiwa kwa panga kichwani na binti yake kubakwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Mtaa wa Benki ya zamani mjini Igunga na watu ambao walimtaka atoe pesa za kampeni. Akizungumza akiwa kitandani katika wodi ya majeruhi katika hospitali hiyo, kada huyo alisema tukio hilo lilitokea juzi kuamkia jana majira ya saa nane za usiku. Alisema alisikia kishindo ambacho kiliuvunja mlango wake wa chumbani na kisha watu hao kummulika kwa tochi kali usoni.

Alisema wakati akijaribu kuchukua panga lake ambalo alilihifadhi chini ya kitanda ili akabiliane na mhalifu huyo, alikatwa panga la kichwa ambalo lilimfanya aanguke chini na kishindo hicho kilimwamsha mkewe na mwanaye wa kike ambao nao walijikuta wakikabiliana na mvamizi huyo.

“Alininyang'anya panga nililokuwa nataka kuchukua na kusisitiza kuwa anataka simu na pesa nilizopewa za kampeni,” alisema na kuongeza kuwa alimruhusu achukue suruali ambayo alikuwa ameining’iniza katika msumari ukutani ambayo ndiyo iliyokuwa na fedha.Msalika alisema mhalifu huyo alimtwanga panga jingine kichwani ambalo lilimfanya apoteze fahamu kwa muda na kisha kumshika mkono mtoto wake wa kike na kuondoka naye.

“Nilizinduka na kujikokota nikisaidiwa na mke wangu hadi kwa jirani zetu ambao wana pikipiki ili waniwahishe polisi na baadaye hospitali, lakini kabla hatujaondoka binti yangu akarudi,” alisema Msalika. Alisema kuwa walimwuliza alipokuwa amemuachia akajibu kuwa ni jirani na mtoni. Msalika alisema kwa kuwa binti huyo hakuwa katika hali nzuri, hakuendelea kumhoji zaidi na badala yake alipelekwa polisi na kupewa PF 3 na kisha kupelekwa hospitali ya wilaya.

Msalika alisema kesho yake asubuhi alikuja mkewe na makada wengine wa chama hicho akiwamo mwanamke aliyemtaja kwa jina moja la mama Kashi walikuja kumletea chai ndipo mama wa mtoto alipomueleza kuwa binti yao katika kadhia ile alibakwa. “Mimi nashangaa huyo mtu kuja kutaka pesa kutoka kwangu wakati kampeni za safari hii sikushiriki kabisa tofauti na inavyokuwa miaka ya nyuma,” alisema na kuongeza kuwa CCM huwa wanamtumia kutumbuiza kwa kwaya katika hafla tofauti.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Anthony Ruta alithibitisha kutokea kwa tukio hilo: “Ni kweli tukio hilo lipo na mtoto amethibitika hospitalini kuwa alibakwa na hali yake inaendelea vizuri na jeshi la polisi limefungua faili kuhusiana na tukio hilo la ubakaji na hakuna mtu ambaye ameshatiwa mbaroni kuhusiana na tukio hilo.”

Hilo litakuwa ni tukio la pili ambalo linahusiana na masuala ya kampeni za kisiasa zinazoendelea mjini Igunga za kuwania kiti cha ubunge katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2, mwaka huu. Katika tukio la kwanza, mtu mmoja, Mussa Tesha alimwagiwa tindikali na jeshi la polisi linamshikilia mtu mmoja kuhusiana na tukio hilo.

Mwananchi

Hao ni majambazi tu wanaotaka hela. Hata hivyo CCM wanawaweka hatarini wale wanaowapa fedha kugawa.
 
"CCM Igunga wafyekana mapanga kugombea pesa". maoni yangu hiki kichwa cha habari kimekekaa kisiasa zaidi, je kuna uthibitisho kwamba uyo mkataji na mbakaji aliangusha kadi ya CCM kwenye harakati zake na kujua kwamba ni mwanachama wa CCM? au ndio siasa za uchaguzi unafanya umakini wa uwandishi uwekwe kapuni?Kwenye matukio kama haya siasa ziepukwe ili sheria ifuate mkondo wake.

Kabla ya uchaguzi CCM ilishaanza kugawa pesa Igunga na kulalamikiwa na vya vingine, Kamati kuu ilipokaa ilitoa kauli kwamba hizo pesa zinagawiwa na chama kwa mawakala wa kampeni kama posho na hivyo TAKUKURU wasiwafanye kitu, hii ilishatoka kwenye luninga na vyombo vingine.

Ya juzi ndo huyo kada wa CCM anafuatwa na kuumizwa na bintiye kufanyiwa .... kwa shinikizo la kudai pesa za kampeni.

Yakhe unataka ushahidi gani huu ya hili kwa utetezi wako kwamba ni jambo la kisiasa wakati waadhirika ni wananchi tokana na mambo ya kisiasa na papo hapo shughuli inayofanyika Igunga ni ya kisiasa?

 
Huyo binti aliyebakwa ana umri gani? Sooo sad. We mbaba ukitoka hospali rudisha na kadi ya CCM, hnawezekana ndo malipo ya kuwa magamba.
 
Mmezoea kila ki2 Chadema b serious guyz
Pole sn kwa panga na bint wa wa2 ambae hauckin maskin,u ppo get serious mnaumiza baba na dada zenu
 
hapa kuna walakini Jamani CCM acheni kugawa pesa hovyo ona sasa watu wameanza kuuana kisa pesa za kampeni Muogopeni Mungu jamani aidha tangazeni wazi kiwango mnacho wapa makada wenu ili wauaji wapime kama pesa inatosha au la maana utakuta mtu alipewa sh. 10000 tu wauaji wanadhani alipewa nyingi MUNGU INUSURU IGUNGA
 
Back
Top Bottom