CCM Hali mbaya, Janja yake Yabainika !

CCM Hali mbaya, Janja yake Yabainika !

Kuna tatizo kubwa sana la kiuongozi kwa CCM na nchi kwa ujumla.
Uongozi wa kitaasisi haumtegemei mtu mmoja bali washauri wengi wenye akili nzuri (intelligence), na kikubwa kinachokosekana ni hao washauri.
Kama washauri wangekuwa wazuri, ilikuwa rahisi tu kuacha mchakato uendelee kama Warioba alivyoanzisha halafu wanafanya frustration kwenye kura ya maoni. Hapo heshima ya uongozi wa awamu ya nne ingepanda bila hata ya wananchi wa kawaida kujua kilichotokea. Huu mgogoro wa katiba umesabishwa na kukosa hekima na maarifa tu, hata kama Rais hakutaka Muungano wa serikali tatu, ilikuwa ni rahisi kurekebisha.
Jamii imepotoka kwa kuchagua viongozi kwa kuangalia madaraja ya ufaulu bila kuangalia kama wana akili nzuri ama la. Ni muhimu kujua kwamba akili nzuri haipimwi kwa madaraja ya ufaulu tu. (Please note that ''Grades don't measure intelligence and learned fools are more fool than ignorant fools'')
Bahati mbaya zaidi, viongozi wanaweza kuwa hawana akili nzuri na wakateua washauri wenye akili duni kuliko wao.
Tunahitaji sasa kuboresha mfumo wa uongozi hasa idara za usalama.
Uongozi ni kujua namna ya kuwatumia washauri wenye intelligence.
Viongozi wakipata washauri wazuri kuanzia ngazi za chini mambo yataenda vizuri tu hata kama wao wenyewe hawako smart sana!
 
Ccm ilikuwepo ipo na itaendelea kuwepo

Natofautiana na wewe kidogo, Mungu peke yake ndiye aliyekuwepo na ataendelea kuwepo.

Mleta mada kasema tuondoe itikadi zetu tujikite kwenye hoja ya msingi kwa ajili ya ustawi na afya ya nchi yetu.

Nakubaliana na mleta mada hapo chama chetu kilikosea sana. Rais wetu alikuwa na nia njema katika jambo hili lakini makada wakamtisha ndo ikawa hivo tena.

Naungana na maoni ya wananchi bila kuogopa chama changu.
 
Natofautiana na wewe kidogo, Mungu peke yake ndiye aliyekuwepo na ataendelea kuwepo.

Mleta mada kasema tuondoe itikadi zetu tujikite kwenye hoja ya msingi kwa ajili ya ustawi na afya ya nchi yetu.

Nakubaliana na mleta mada hapo chama chetu kilikosea sana. Rais wetu alikuwa na nia njema katika jambo hili lakini makada wakamtisha ndo ikawa hivo tena.

Naungana na maoni ya wananchi bila kuogopa chama changu.

Haiwezekani mbona ccm weye una akili?
 
Tunaweza kumlaumu JK kwa maelezo yake lakini aliweka angalizo kwamba naomba ni mnukuu ."Akili za kuambiwa changanya na zako". Wenye matatizo ni wabunge wenyewe kwa uwoga wao na kujipendekeza kwao wao wakachukua za kuambiwa tu na za kwao wakaziacha sasa tutegemee nini? Hivi mtu akikwambia kula sumu utakula? Au itabidi utafakari kabla haujaibwia?
 
Natofautiana na wewe kidogo, Mungu peke yake ndiye aliyekuwepo na ataendelea kuwepo.

Mleta mada kasema tuondoe itikadi zetu tujikite kwenye hoja ya msingi kwa ajili ya ustawi na afya ya nchi yetu.

Nakubaliana na mleta mada hapo chama chetu kilikosea sana. Rais wetu alikuwa na nia njema katika jambo hili lakini makada wakamtisha ndo ikawa hivo tena.

Naungana na maoni ya wananchi bila kuogopa chama changu.

ccm wote mngekuwa reasonable hivi tungefika mbali.
 
Tunaweza kumlaumu JK kwa maelezo yake lakini aliweka angalizo kwamba naomba ni mnukuu ."Akili za kuambiwa changanya na zako". Wenye matatizo ni wabunge wenyewe kwa uwoga wao na kujipendekeza kwao wao wakachukua za kuambiwa tu na za kwao wakaziacha sasa tutegemee nini? Hivi mtu akikwambia kula sumu utakula? Au itabidi utafakari kabla haujaibwia?
Mkuu, tujaribu kujiuliza kwa nini Rais aliamua kuelemea upande wa chama chake na kuwaacha wananchi wengi wengine? Pale BMK alikuwa mgeni rasmi kama Rais wa nchi hivo alikuwa akitoa maagizo kwa wanachama wake kusimamia msimamo wa chama chake. Rais angejitambua pale alikuwa kama mkuu wa nchi na kutoonesha HAMASA ya chama chake basi wabunge wa chama chake (sio wote) tungewalaumu kwa kuegemea maslahi ya chama.
 
Mkuu, suala sasa ni wananchi kuchukua UAMUZI wa kumshughulikia anaye hujumu UPATIKANAJI wa katiba kama ilivotayarishwa na tume HALALI ya katiba.

Ujinga unatughalimu sana watz.
Badala kumshughulikia aliyevunja sheria kwa kuwasilisha rasimu feki ya kundi fulani, tunashughulika na waliokataa kushiriki dhuluma hiyo.
 
Ujinga unatughalimu sana watz.
Badala kumshughulikia aliyevunja sheria kwa kuwasilisha rasimu feki ya kundi fulani, tunashughulika na waliokataa kushiriki dhuluma hiyo.
Badala ya kuahidi kuijadili rasimu rasmi ya tume ya katiba sasa hivi wamewakimbilia viongozi wa dini ili watoe miito ya kuwataka UKAWA kurejea BMK badala ya wao kukiri kuwa ndio chanzo cha tafran hii.
 
Kurudi bungeni kujadili rasimu ya tume ya warioba au rasimu ya CCM? Nini chanzo cha ukawa kutoka bungeni? na je, chanzo hicho kimetafutiwa mwarobaini? serikali mbili zipo kwenye rasimu ipi?
 
Wametoka mkataba hadi tatu, wametoka majimbo hadi tatu, wametoka mbili na wamebaki na mbili hawataki mabadiliko lakini wako tayari kuruhusu "uhuru zaidi" kwa upande mmoja (wanauogopa au wanaukejeli). Bahati mbaya uhuru zaidi inamaana serikali ya JMT inazidi kuwa ya kitanganyika (majukumu yake). Mambo ya Tanganyika waachiwe watanganyika na ya wanzibari waachiwe wazanzibari. Yale ya muungano yawe ya muungano. Mbili zilizoboreshwa haziwezi kamwe kutupatia hili hivyo ni longolongo. Wakiendelea na msimamo wa mbili hakuna cha kujadili-watengeneze katiba yao.
 
Rais Kikwete Alipolitangazia Taifa Kuhusu Nia Yake Ya Dhati Ya Kuona Tanzania Inapata Katiba Mpya,katiba Itakayotokana Na Matakwa Ya Wananchi, Nilimuona Bonge La Jembe Anayetaka Kuacha Historia Isiyofutika Kwa Watu Wa Kizazi Hiki. Lakini Alikuja Kunishangaza Wakati Wa Ufunguzi Wa BMK Pale Alipoyakana Maoni Ya Wananchi Tena Kwa Vitisho Kua Yakipita Maoni Ya Wananchi Jeshi Litachukua Nchi,na Kuacha Majukumu Kwa Wajumbe Wa Ccm Waliomo Kwenye BMK Kuhakikisha Maoni Ya Wananchi Hayajadiliwi Bali Wanajadili Ya Kwao Yasiokuemo Kwenye Rasimu.Mh.Rais Ndiye Anaekwamisha Mchakato Wa Katiba Wa Mpya, Lolote Litakalotokea Kuhusiana Na Katiba Kama Kenya Huo Msalaba Ni Wake.Kama Kweli Alikua Na Nia Nzuri Na Taifa Lake Abadilishe Msimamo Na Amuamuru Mwenyekiti Wa BMK Aweke Rasimu Ya Warioba Mezani Ndiyo Ijadiliwe UKAWA Watarudi Ndani Ya BMK Haraka Sana. SOTE TUNAJUKUMU LA KUJENGA NA KUILINDA NCHI YETU,SOTE TUNAHITAJI HAKI SAWA NA MGAWANYO WA KEKI YA TAIFA. Katiba Ndiyo Mkombozi Wetu.
 
Kurudi bungeni kujadili rasimu ya tume ya warioba au rasimu ya CCM? Nini chanzo cha ukawa kutoka bungeni? na je, chanzo hicho kimetafutiwa mwarobaini? serikali mbili zipo kwenye rasimu ipi?

UKAWA wakikosea tu na kurudi bunge la katiba ya ccm historia itawahukumu !

...maana ccm watawaambia walishiriki kuhalifu maoni ya wananchi !
 
Natofautiana na wewe kidogo, Mungu peke yake ndiye aliyekuwepo na ataendelea kuwepo.

Mleta mada kasema tuondoe itikadi zetu tujikite kwenye hoja ya msingi kwa ajili ya ustawi na afya ya nchi yetu.

Nakubaliana na mleta mada hapo chama chetu kilikosea sana. Rais wetu alikuwa na nia njema katika jambo hili lakini makada wakamtisha ndo ikawa hivo tena.

Naungana na maoni ya wananchi bila kuogopa chama changu.


Kwa namna ulivyotiririka inanipa shida kuamini kama wewe unakunywa supu ya mbogamboga, kama ni kweli basi be careful watakukolimba very soon
 
Kwa namna ulivyotiririka inanipa shida kuamini kama wewe unakunywa supu ya mbogamboga, kama ni kweli basi be careful watakukolimba very soon

...usimtishe mwenzio !

Hayo mambo yalishapitwa wakati.

Mtaendelea kuumbuka sana !
 
kila siku ninasema kwamba hila za ccm ni pembe la ngombe azifichiki tena kila hila inayofanywa na ccm lazima igundulike,huu sio wakati wa hila ni wakati wa ukweli kama anavyofanya Lema na ndio maana anafanikiwa Lema hana hila katika mambo yake
 
Back
Top Bottom