Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Katibu Mwenezi wake wa Mkoa wa Arusha, Saipulani Ramsey, kimepinga vikali madai yanayoenezwa mitandaoni kuwa kinakiwezesha Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), hususan kiuchumi. Baadhi ya watumiaji wa mitandao wamehoji chanzo cha fedha za CHAUMMA na kasi ya kuibuka kwake kuelekea uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari Mei 21, 2025 Makao Makuu ya CCM mkoani Arusha, Saipulani amesema kuwa madai hayo hayana msingi wowote na hayapaswi kupewa uzito.
“CHAUMMA ni chama kinachojiendesha chenyewe. CCM haina uhusiano wowote wa kifedha wala kimkakati na chama hicho. Tunajiuliza: Tungewasaidia kwa makubaliano yapi?” amesema
Ramsey ameendelea kusema kuwa kama CCM ingekuwa na nia ya kuidhoofisha CHADEMA kwa makusudi, basi kwa mtazamo wake binafsi, nguvu kubwa ingewekezwa katika kuisaidia ACT-Wazalendo au hata CUF, na si CHAUMMA.
Pia soma Pre GE2025 - DSM - CHAUMMA yapokea rasmi baadhi ya G55 walioondoka CHADEMA
Akizungumza na waandishi wa habari Mei 21, 2025 Makao Makuu ya CCM mkoani Arusha, Saipulani amesema kuwa madai hayo hayana msingi wowote na hayapaswi kupewa uzito.
“CHAUMMA ni chama kinachojiendesha chenyewe. CCM haina uhusiano wowote wa kifedha wala kimkakati na chama hicho. Tunajiuliza: Tungewasaidia kwa makubaliano yapi?” amesema
Ramsey ameendelea kusema kuwa kama CCM ingekuwa na nia ya kuidhoofisha CHADEMA kwa makusudi, basi kwa mtazamo wake binafsi, nguvu kubwa ingewekezwa katika kuisaidia ACT-Wazalendo au hata CUF, na si CHAUMMA.
Pia soma Pre GE2025 - DSM - CHAUMMA yapokea rasmi baadhi ya G55 walioondoka CHADEMA