CCM and UDASA, this is shameful

CCM and UDASA, this is shameful

Upuuzi waliotokea UDASA na iwe Red Bull kwa wapenda haki na mabadiliko ya kweli popote pale walipo...Hata siku moja isije ikatokea kubweteka kuwa CCM watakubali kuachia madaraka kirahisi! Tambueni kuwa CCM wana fedha nyingi za Ufisadi zikiwemo za MNCs zinazotumika kuhalalisha wanachokitaka... Mazingira ya Umasikini na kukosekana kwa ajira kwa vijana ni mtaji tosha kwa CCM... Tujipange upya, tuongeze kasi maana upumbavu unazidi kutamalaki miongoni mwa Wanajamii hususan the so called intellectuals ...
 
PICHA HALISI YA MDAHALO WA LEO STAR TV.

Ndg watazamaji, wasomaji na wafuatiliaji wa MIDAHALO hii mbalimbali ya Katiba mpya, naamini kwamba, leo 03/08/2014 siku ya Jumapili mmepata wasaa mzuri wa kuutazama mdahalo wa leo uliofanyika katika ukumbi wa NKRUMAH pale mlimani Chuo Kikuu, kupitia Kituo cha Television cha Star tv.

Kama ilivyo kawaida yao watawala, huandaa midahalo inayohusu masuala ya Kitaifa kwa kujikita zaidi katika misingi ya uchama zaidi, na hii imedhihirika leo pale UDSM.

Ni mdahalo ambao watu maalumu wa kuzungumzia hoja za kuibeba CCM katika issue nzima ya mchakato wa Katiba mpya, tayari walikuwa wamekwishaandaliwa kwa majina kama tulivyoona wakisomwa majina mmoja baada ya mwingine, na kulipuka kama mabomu yalokuwa yametegwa.

KISA CHA MIMI KUZUILIWA MARA MBILI KUZUNGUMZA PALE JUKWAANI LEO.

Mimi Francis, nilikuwa nimekaa line ya mbele kabisa chini kwenye floor pale ndani Nkrumah Hall, kushoto kwangu alikuwepo Adams Chagulani, nyuma yangu walikuwepo Habib Mchange na Mtela Mwampamba, sasa basi, wakati nikiendelea kuandaa hoja zangu pale chini ili nikaziwasilishe kwa niaba ya Watanzania hasa wale wote wenye Imani na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kumbe wakati huo akina Chagulani walikuwa wananichora na kunilia target ya kunidhibiti kwa namna yoyote ile, ili mradi nisipate nafasi ya kuwasilisha yale yote niliyoyaandaa kwenye Document zangu, hivyo ili kutimiza azma yao hiyo ikawalazimu kula dili na maafisa usalama waliokuwepo pale ndani bila ya mimi kuugundua mchezo kwamba unanihusu mimi.

Niliponyanyuka mara ya kwanza na kufika jukwaani ghafla nimevamiwa na watu zaidi ya watatu na kushushwa chini na hatimaye tena nikapanda mara ya pili, lakini sikuweza kufua dafu kwa sababu tayari walikuwa wamejenga mtandao mkubwa wa kunidhibiti pale ndani.

Ishaalah nashukuru mola tumehitimisha salama bila mtafaruku wowote, ingawa CCM wameangukia pua
vibaya sana!
 
Mambo KUMI niliyojifunza kwenye mdahalo wa leo Nkurumah Hall.

1.Kongamano lilikua la CCM ku-counter attack makongamano mengine yaliyotangulia ambayo yalidhaniwa ni ya UKAWA.

2.Kwa mara ya kwanza tangu nimemfahamu Mwigulu Nchemba hatimaye leo ameongea kizalendo na ameitendea haki skafu aliyovaa.

3.Dr. Kitila Mkumbo nimemfahamu vzr leo. Nimegundua ni mtu mstaarabu (labda kuliko wanasiasa wote), mwenye ushawishi, uwezo wa kujenga hoja na mzalendo. Sikuwa namjua hivi kabla ya leo.

4.Mzee Wassira ni mtaji mkubwa sana wa CCM kwenye Propaganda. Na bila shaka siku akiondoka itawachukua miaka 50, CCM kumtengeneza mtu kama Wassira.

5.Mungu amemtunuku Tundu Lissu akili nyingi sana. Yeye anajua hili, lakini CCM wanalijua pia, na wanamuogopa kwa hilo.

6.Uwezo wa Prof.Tibaijuka kujenga hoja ni mdogo sana. Pengie kuliko maprofesa wote kusini mwa Jangwa la Sahara.

7.Baadhi ya wachangiaji waliojiita "raia" walikua wameandaliwa na vyama vya siasa. Na walizungumza yale waliyoelekezwa kuzungumza na vyama vyao.

8.Mzee Makaidi na yule mzee mwenzie wameonesha hali halisi ya wazee wa nchi hii ilivyo.

9.CCM walibadili rasimu kwa makusudi kwa utetezi kuwa "rasimu si msaafu" ambao haufai kurekebishika. Wakasahau kuwa hata serikali mbili si "msaafu" pia.

10.Uwezekano wa kupata Katiba mpya kwa sasa HAUPO.!
 
heshima ya GRADUATES wa UDSM NA WASOMI TOKA PALE ILIISHIA 2006.

FROM THERE NI VIMEO TU. NAWAZA KUANZISHA UZI 'POROMOKO LA UDSM'
NA ELIMU YA JUU KWA UJUMLA.
 
mdahalo huu umeidhalilisha zaidi ccm , wala usikonde mkuu .
 
Mambo ya kawaida kwenye demokrasia, sasa upinzani hata hamtaki cha kibisha?! Wengine tunapenda yawepo kama challenge kwenu upinzani, hasa ukichukulia upinzani wenyewe ni kama wa kichaga au kipemba..
Mtu kuwa kichaa si lazima aokote makopo.. Hata upuu.zi kama huu!
 
Kilichoniuma Ni Jinsi Upendeleo Wa Wazi Kwa Wachangiaji Yaani WacCm Kibao Halafu Mwishoni Walisema Dk Mbili Wakampa Lukuvi Dkika 45 Amalizie, Haya Nikasema Nikajiliwaze Na Matokeo Ya Taifa Starz Nako Tumechezeia, Nchi Hii! Aaah Cjui Niende Wapi?

mkuu mbavu zangu.....pole ndio tulivyo watizi wazito kuelewa wepesi kusahau'
 
Hahah mi nimemkubali wasira' nahisi hata sifa za kuwa rais anazo na ataweza kutuwakilisha vizur hata kimataifa
 
kwani dar hakuna wanaosoma udsm.mbona wengine tulihudhuria coz tupo field hapa dar plus wanaoishi hapa.

Hivi wewe matosile ungekuwa mwanafunzi wa chuo kikuu ungeshindwa kuelewa maneno haya?

quote_icon.png
By Micro E coli


Pale hakuna wanafunzi wapo likizo
 
Mdahalo wa udasa unaonekana kuwa tatizo lakini mchakato majimboni wa Shabani Kisu ulikuwa sahihi. Nawapongeza udasa kwa kuaandaa mdahalo ambao umeendelea kutufungua macho juu ya ukawa.
 
Kwa mdaharo wa leo nimejifunza mambo mengi sana ya ajabu kwa wasomi wetu. Na kilichonisikitisha ni wasomi kutoka chuo kipi?. Sehemu ambapo inaaminiwa na watu wengi kuwa greater thinkers wa Tanzania ndipo walipo au wanategemea kutoka....duuuuuu!!!!. Niachane na hilo nirudi kwenye maada yangu niliyokusudia kuitoa.

Dr.kitila kasifiwa leo na CCM hasa Lukuvu kuwa ana akili sana,na Lukuvi amesisitiza na kumuomba Kitila afanye utafiti kuhusu kama kweli Muungano wa watu watatu yaani UKAWA una nia thabiti au njema ya kupata katiba mpya?. Wamekuomba wao,na ukifanya hivyo watakusaidia sana maana watawala wanapenda kusifiwa.

Mfano,lukuvi anajua kabisa Kitila na CHADEMA wana UGONVI, ivi mtu mwenye akili unategemea huyu atakuja na majibu ambayo kweli yanaonyesha uhalisia wa utafiti....maana yeye mwenyewe ana interest. Dr. Fanya hicho kitu haraka sana na watakupa pesa nyingi na utakuja na majibu wanayotaka wao ili wayatumie kwenye midaharo..fanya....fanya haraka. Unaweza ukajifungia hotelini siku tano au wiki ukamaliza machezo.

Nilitegemea angalau AWAAMBIE wana UDASA kwa ujumla na si Dr.Mkumbo. Dr. Dili hilo fanya na pesa ipo nadhani maana wao ndio wamekuomba. Usiwape majibu tofauti baada ya utafiti maana hawatakupa hizo pesa.

We taa.hira kabasa. Na pale mwishoni alipomsifia Tundu Lisu ina maana alikua anamwambia ili ampe hela?
Acheni mahaba yenu ya kingese na ki u-chadema. Kunya anye kuku,akinya bata kaharisha???
Sn.itch mkubwa.
 
aibu kubwa vijana nawaona wanashangilia wasira hata akijamba...duuu njaa mbaya sana.

kaka vijana wa chuo kikuu cha dar wako likizo ila sitashangaa ccm wakisema hao walioletwa na mabasi ya UDA ya mafisadi ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar
 
watu elimu zao wamezitia mifukoni kutwa ni propaganda na uzandiki!!! nakumbuka miaka ya 2007 kipindi nipo udsm watu kama Lukuvi h
wasinge pata chance ya kuonge ugoro kwenye aridh ya udsm. nakumbuka ata Jk akutia mguu pale!
 
Niliipenda CCM kwa kuwa kulikuwa na Mwalimu na akina warioba na tume yake ila sasa siipendi CCM kwa kuwa iko na Mwigulu na Wasira maana sioni nini wanafanya bado kwa mbali naheshimu Mangula na Lowasa tu.
 
Mambo ya kawaida kwenye demokrasia, sasa upinzani hata hamtaki cha kibisha?! Wengine tunapenda yawepo kama challenge kwenu upinzani, hasa ukichukulia upinzani wenyewe ni kama wa kichaga au kipemba..

Nawe umechangia?
 
Aibu kubwa kuliko zote ni kuiba wake za watu,unaleta porojo zako ambazo hazina kichwa wala miguu.

mkuu mbona mmengoja tukiwa likizo ndo mkaja UD hmna lolote mnaleta pumba zenu ili muonekane kuwa tunawaunga mkono wanafunzi wa UD hatupo nanyi wezi na mafisadiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Makene...

Ni kwa nini Tundu Lissu asingekataa mwaliko?...

Ilishaelezwa hapa nini CCM wanafanya kuhusiana na Kongamano hilo...Nimeshangaa sana kuwaona Lissu, Machali , Kafulila na wajumbe wengine wa UKAWA kama sehemu ya Kongamano hilo...

Bala, kwa mtu mwelewa ni ngumu sana kugomea mwaliko wa Wanataaluma wa UDASA, lkn kwa lililofanyika leo UDASA litawagharimu sana unless watoe Press Release ya kujisafisha na kuanika ukweli bila kuwaonea aibu hao wanasiasa waliofanya ujinga huu.

Labda ndio maana Mzee Warioba na wenzake kesho nao wataeleza ya kwao, huenda tutapona.

Wanachofanya CCM hakikubaliki, ni udhalilishaji wa hali ya juu kwa Wasomi. UDASA must come up with a Press Release about this unbecoming behaviour of these kind of politics and politicians- otherwise their remaing reputation is finished!
 
Back
Top Bottom