Mleta mada, kwani CCM wameenda kinyume na katiba yao?
107. (1) Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa itakuwa
na wajumbe wafuatao:-
(a)
Mwenyekiti wa CCM.
(b)
Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wanaotokana na
CCM.
(c) Makamu wawili wa Mwenyekiti wa
CCM.
(d) Rais wa Zanzibar anayetokana na CCM
(e) Katibu Mkuu wa CCM.
(f) Manaibu Katibu Mkuu wa CCM
(g) Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa
Organaizesheni.
(h) Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa
Itikadi na Uenezi.
(i) Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa
Mambo ya Siasa na Uhusiano wa
Kimataifa.
(j) Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa
Uchumi na Fedha.
(k) Wenyeviti wote wa CCM wa Mikoa.
(l) Makatibu wote wa CCM wa Mikoa.
(m) Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Makamu
Mwenyekiti kutoka kila Jumuiya ya
wananchi inayoongozwa au
inayojishirikisha na CCM.
(n) Wajumbe wengine wote wa
Halmashauri Kuu ya Taifa
wanaopatikana kwa mujibu wa vifungu:
92(4)(b); 105(10); 105(15); 106(5)(c) na
108(13)(e).
114
(13) Unapofika wakati wa Uchaguzi,
Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa
itashughulikia mambo yafuatayo:-
(a) Kuteua jina la Mwanachama
atakayesimama katika uchaguzi wa
Mwenyekiti wa CCM, na majina mawili
ya Wanachama watakaosimama katika
uchaguzi wa Makamu wa Mwenyekiti
wa CCM.
(b) Kupendekeza kwa Mkutano Mkuu wa
CCM wa Taifa majina yasiyozidi matatu
ya Wanachama wanaogombea nafasi
ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na kuyawasilisha mbele ya
Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa.
(c) Kuchagua jina moja la Mwanachama
atakayesimama katika uchaguzi wa
Rais wa Zanzibar.
(d) Kuwachagua Katibu Mkuu wa CCM,
Manaibu Katibu Mkuu wa CCM, Katibu
wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa
Organaizesheni, Katibu wa
Halmashauri Kuu ya Taifa wa Itikadi na
Uenezi, Katibu wa Halmashauri Kuu ya
Taifa wa Mambo ya Siasa na Uhusiano
wa Kimataifa na Katibu wa Halmashauri
Kuu ya Taifa wa Uchumi na Fedha.
(e) Kuwachagua Wanachama wasiozidi
kumi kuwa Wajumbe wa Halmashauri
Kuu ya CCM ya Taifa kutokana na
mapendekezo ya Mwenyekiti wa CCM.
Duh!! huo ni uchaguzi gani? wakati kinachoonyesha kwenye Katiba ya CCM ni jina moja tu linateuliwa kwa ajili ya kupigiwa kura ikiwa na maana hakuna ushindani wa wagombea zaidi ya mmoja na hakuna uchukaji wala urejeshaji wa fomu za kugombea.