CCM acheni utapeli kupitia TV, inatia kinyaa

CCM acheni utapeli kupitia TV, inatia kinyaa

Tangazo la CCM katika maTV la kuwaalika wajumbe wa Mkutano Mkuu mjini Dodoma linawataka kwamba July 23 ni siku ya kumuaga Dr.Jakaya Kikwete na kumchagua mwenyekiti mtarajiwa Dr.Magufuli kuwa mwenyekiti wa CCM.

Halafu linaongeza kuwa ‘‘njoo Dodoma tuimarishe Demokrasia’’

MAONI YANGU

Huu ni utapeli wa wazi wazi. Magufuli haendi kuchaguliwa, anakwenda kukabidhiwa chama. Uchaguzi ni ushindani, tuambieni anakwenda kushindana na nani. Ni lini fomu za kugombea uenyekiti zilitolewa

Hata kama shetani anapenda watu waongo lakini kwa uongo huu wa CCM hata shetani atashituka. Kwamba CCM inawaalika wajumbe waje Dodoma kuimarisha Demokrasia??? Demokrasia ya kukiuka katiba inayotaka mwenyekiti kuchaguliwa nyinyi mnaenda kukabidhi?
kamanda wewe upo chama gani. maneno haya unayatoa kwa kutegemea ulinganifu upi. kwa sababu sidhani kama ulilinganisha na chadema kwa sababu huko ndio kabisaaa. uozo mtupu. mwwnyekiti ekuaa Mungu mtu
 
Sidhani kama unaelewa ulichokiandika.

Kazi ya Magufuli ni kuwatumikia Watanzania na siyo ccm, wapuuzi wengi kama wewe hili hamlijuhi, ndio maana anaomba Watanzania wamuombee na siyo wanaccm wamuombee.

Ni mtu dhaifu peke yake hapa duniani ndio uhogopa upinzani, ukiona shabiki wa Simba anaombea Yanga ife au kinyume chake huyo ni wa kupimwa akili.

Wewe ni mwehu, katiba ndio sheria mama dunia nzima, watu makini tunapenda ccm iwe imara ili siku vyombo vya dola vikikubali kuheshimu maamuzi ya wapiga kura basi ningependa nione ccm kikiwa ni chama cha upinzani imara na kisigeuke kuwa historia kama KANU.

Lowasa alichukuwa fomu kama taratibu zinavyomtaka.

Badly hakuna ulijuwalo, CUF wapo kwenye uchaguzi na fomu zipo wazi kwa wanachama wote wenye sifa kuchukuwa fomu kugombea uenyekiti.

Je una lingine?
Nitamuombeaji wakati mm nina njaa?
Ajira kasitisha mm nitapataje hizo nguvu za kimuombea wakati huku mtaan nahangaika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom