Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Chanzo: Tanzania Daima
na Irene Mark
CHAMA Cha Jamii (CCJ), kimejiandaa kujibu kauli ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, ya kuwa hana pesa za kufanya uhakiki wa majina ya wanachama wao kabla ya kuwapa usajili wa kudumu.
Taarifa za ndani kutoka kwenye chama hicho ambacho kimekutana kwa dharura na kujifungia kwa siku tatu kujadili kauli hiyo, inasema imeshtushwa na kauli za msajili, hivyo kimejipanga kutoa tamko kwa maandishi leo.
Tendwa alikaririwa na vyombo vya habari hivi karibuni akisema kwa sasa ofisi yake haina fedha kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa majina ya wanachama wa CCJ, badala yake fungu lililopo ni kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu sheria mpya ya uchaguzi iliyosainiwa kwa mbwembwe na Rais Jakaya Kikwete Machi 17, mwaka huu.
Aidha, msajili huyo alisema majibu ya kuwa na fedha ama kutokuwa nazo kwa ajili ya kuzunguka mikoani kufanya ukaguzi wa majina hayo, atayatoa Agosti 19 mwaka huu, muda ambao ni vigumu kwa CCJ kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31.
Ukweli viongozi na wanachama wa CCJ wameshtushwa sana na hii inaonekana ni mbinu ya kutuzuia kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu ujao, hivi ninavyoongea na wewe tangu juzi wanakutana wanajifungia wakijadili suala hilo hilo.
Kesho watazungumza na waandishi wa habari kuwaeleza nini wamekubaliana kama chama na kuona namna nyingine inayofaa kupitia ofisi ya msajili itakayotuwezesha kupata usajili wa kudumu ikiwezekana kabla ya Juni, kilisema chanzo hicho cha uhakika kutoka CCJ na kubainisha kwamba tamko hilo kali litatolewa kwa maandishi.
Aidha, chanzo hicho kilihoji kuwa: Kila mwaka serikali inatenga fungu kwa ajili ya usajili wa vyama vipya, tangu kuanza kwa mwaka huu hakuna chama kilichosajiliwa ni vipi Tendwa anakosa fedha?
NB:
Majibu hayo yanatarajiwa kutolewa leo saa tano asubuhi kwenye Ofisi za Maelezo. MM
na Irene Mark
CHAMA Cha Jamii (CCJ), kimejiandaa kujibu kauli ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, ya kuwa hana pesa za kufanya uhakiki wa majina ya wanachama wao kabla ya kuwapa usajili wa kudumu.
Taarifa za ndani kutoka kwenye chama hicho ambacho kimekutana kwa dharura na kujifungia kwa siku tatu kujadili kauli hiyo, inasema imeshtushwa na kauli za msajili, hivyo kimejipanga kutoa tamko kwa maandishi leo.
Tendwa alikaririwa na vyombo vya habari hivi karibuni akisema kwa sasa ofisi yake haina fedha kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa majina ya wanachama wa CCJ, badala yake fungu lililopo ni kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu sheria mpya ya uchaguzi iliyosainiwa kwa mbwembwe na Rais Jakaya Kikwete Machi 17, mwaka huu.
Aidha, msajili huyo alisema majibu ya kuwa na fedha ama kutokuwa nazo kwa ajili ya kuzunguka mikoani kufanya ukaguzi wa majina hayo, atayatoa Agosti 19 mwaka huu, muda ambao ni vigumu kwa CCJ kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31.
Ukweli viongozi na wanachama wa CCJ wameshtushwa sana na hii inaonekana ni mbinu ya kutuzuia kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu ujao, hivi ninavyoongea na wewe tangu juzi wanakutana wanajifungia wakijadili suala hilo hilo.
Kesho watazungumza na waandishi wa habari kuwaeleza nini wamekubaliana kama chama na kuona namna nyingine inayofaa kupitia ofisi ya msajili itakayotuwezesha kupata usajili wa kudumu ikiwezekana kabla ya Juni, kilisema chanzo hicho cha uhakika kutoka CCJ na kubainisha kwamba tamko hilo kali litatolewa kwa maandishi.
Aidha, chanzo hicho kilihoji kuwa: Kila mwaka serikali inatenga fungu kwa ajili ya usajili wa vyama vipya, tangu kuanza kwa mwaka huu hakuna chama kilichosajiliwa ni vipi Tendwa anakosa fedha?
NB:
Majibu hayo yanatarajiwa kutolewa leo saa tano asubuhi kwenye Ofisi za Maelezo. MM