Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 305
Chama Cha Jamii (CCJ), Jumatatu ijayo kitakwenda kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kuomba usajili wa kudumu baada ya kutimiza sharti la kupata wanachama 2,000 katika mikoa 10.
Chama hicho kimevuka kiwango cha idadi ya wanachama wanaotakiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa ajili ya kupatiwa usajili wa kudumu, baada ya kufanikiwa kupata wanachama 7,000 badala ya wanachama 2,000 waliotakiwa kupatikana katika mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar.
CCJ kimepata mafanikio hayo katika kipindi cha siku 15 tangu kipatiwe cheti cha usajili wa muda Machi 2, mwaka huu.
Kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa, chama chenye usajili wa muda kinatakiwa ndani ya siku 180 kiwe kimepata wanachama 200 kwa kila mkoa kwa walau mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar, ambapo CCJ ilipewa muda iwe imekamilisha suala hilo hadi Novemba, mwaka huu.
Kutokana na mafanikio hayo, chama hicho kimesema kinatarajia kuwasilisha kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini orodha ya wanachama kilichowapata katika mikoa hiyo, Jumatatu kuomba kupatiwa usajili wa kudumu.
Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, aliitaja mikoa ambayo chama hicho kimefanikiwa kuvuna wanachama hao kuwa ni Mwanza, Dodoma, Morogoro, Iringa, Mbeya, Shinyanga, Tabora, Pwani, Dar es Salaam na Unguja na Pemba.
Alisema katika mikoa hiyo waliteua watu kwenda katika mikoa hiyo kuandikisha wanachama na kwamba, katika kila mkoa walipeleka kadi 700 na hadi kufikia jana taarifa walizozipata kutoka vyanzo vyao katika uendelezaji wa uandikishaji wa wadhamini wanaowahitaji, zimethibitisha kwamba, kadi hizo zote zimeisha.
Kwa hiyo sasa hivi tume-stop tangu jana, ni kwamba, tunatengeneza hizo kadi sasa, kwa maana ya kuendelea tena kuzigawa, alisema Muabhi katika mkutano na waandishi ulioandaliwa na chama hicho kwa mara ya kwanza, jijini Dar es Salaam jana tangu kipatiwe cheti cha usajili wa muda.
Alisema mafanikio hayo yanaashiria jinsi gani Watanzania walivyoweza kukiunga mkono chama chao.
Kwa hiyo, tumeona kwamba itakapofika tarehe 22, mwezi huu, kama hakutatokea tatizo lingine, ambalo liko juu ya uwezo wetu, tutakwenda kuwasilisha kwa Msajili wa Vyama Siasa, John Tendwa idadi ya hao wadhamini, kwa maana ya wanachama 200 katika kila mkoa katika mikoa 10, alisema Muabhi.
Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCJ, Dickson Amos, alisema wakereketwa wa CCJ Morogoro waliwaomba kadi 3,000.
Katibu Mkuu huyo alisema wanatarajia kufanya uzinduzi rasmi wa CCJ na shughuli zake Machi 21, mwaka huu.
Alisema wameshakamilisha taratibu zote za kiofisi, hivyo wanataka sasa kukitambulisha chama hicho kwa Watanzania kwamba chama chao kiko imara na kiko tayari sasa kwa kazi.
Aliwataka wananchi kujitolea kuiunga mkono CCJ, ikiwa ni pamoja na kujiandikisha kwa wingi, kujitolea ofisi sehemu mbalimbali kutokana na mahitaji yatakayojitokeza kwa sababu chama hicho ni cha wananchi.
Sababu ya kusema kwamba, wao inatakiwa waguswe moja kwa moja na ujio wa CCJ ikiwa ina malengo ya pekee kabisa na ya makusudi kabisa kwamba, imedhamiria kurudisha hadhi ya taifa la Tanzania, ambayo iliasisiwa na Baba yetu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alisema.
Akitilia mkazo suala hilo, Amos, alisema katika uzinduzi huo, watapokea wanachama wapya, ambao baadhi yao wamewahi kushika madaraka makubwa ndani ya vyama vingi vya siasa.
Alisema viongozi wa CCJ wanatarajia kufanya ziara kwenda kuzuru makazi ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, Butiama, wilaya ya Musoma Vijijini, mkoani Mara kesho.
Alisema katika ziara hiyo, wanataka kwenda kuona kaburi la Mwalimu Nyerere na kufanya mazungumzo na familia yake, ikiwa ni sehemu ya kuthamini na kujali mchango wake katika taifa la Tanzania kama muasisi wake.
Alisema wako viongozi wengi nchini, ambao ni waasisi wa taifa, wamekuwa na heshima kubwa, hivyo ilistahili nao wawape umuhimu wa hali ya juu kwa kuwafanyia ziara.
Hata hivyo, alisema wameona kwa sasa wajaribu kuanzia kwa hayati Mwalimu Nyerere, ambaye tayari ana heshima ya pekee, kwa kuwa anatambuliwa rasmi kama Baba wa Taifa.
Kwa hiyo, hata wale waasisi wengine, napenda kutumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kabisa kwamba, tuko nao na tunawathamini na tunathamini michango yao waliyoitoa katika taifa hili, alisema Muabhi. Alisema watakapomaliza ziara ya Butiama kwa Mwalimu Nyerere, watakwenda kufanya mkutano katika eneo walikouawa kikatili watu 17 hivi karibuni, wilayani Musoma ambako watazungumza na wananchi wa eneo hilo pamoja na wazee. Muabhi alisema katika mazungumzo hayo watatoa usia wao kwa wazee hao pamoja na Watanzania wengine juu ya tukio lilitokea hapo kwamba, halikuwa la kawaida na halikustahili kuwapo katika misingi ya kibinadamu.
Chama hicho kimevuka kiwango cha idadi ya wanachama wanaotakiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa ajili ya kupatiwa usajili wa kudumu, baada ya kufanikiwa kupata wanachama 7,000 badala ya wanachama 2,000 waliotakiwa kupatikana katika mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar.
CCJ kimepata mafanikio hayo katika kipindi cha siku 15 tangu kipatiwe cheti cha usajili wa muda Machi 2, mwaka huu.
Kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa, chama chenye usajili wa muda kinatakiwa ndani ya siku 180 kiwe kimepata wanachama 200 kwa kila mkoa kwa walau mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar, ambapo CCJ ilipewa muda iwe imekamilisha suala hilo hadi Novemba, mwaka huu.
Kutokana na mafanikio hayo, chama hicho kimesema kinatarajia kuwasilisha kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini orodha ya wanachama kilichowapata katika mikoa hiyo, Jumatatu kuomba kupatiwa usajili wa kudumu.
Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, aliitaja mikoa ambayo chama hicho kimefanikiwa kuvuna wanachama hao kuwa ni Mwanza, Dodoma, Morogoro, Iringa, Mbeya, Shinyanga, Tabora, Pwani, Dar es Salaam na Unguja na Pemba.
Alisema katika mikoa hiyo waliteua watu kwenda katika mikoa hiyo kuandikisha wanachama na kwamba, katika kila mkoa walipeleka kadi 700 na hadi kufikia jana taarifa walizozipata kutoka vyanzo vyao katika uendelezaji wa uandikishaji wa wadhamini wanaowahitaji, zimethibitisha kwamba, kadi hizo zote zimeisha.
Kwa hiyo sasa hivi tume-stop tangu jana, ni kwamba, tunatengeneza hizo kadi sasa, kwa maana ya kuendelea tena kuzigawa, alisema Muabhi katika mkutano na waandishi ulioandaliwa na chama hicho kwa mara ya kwanza, jijini Dar es Salaam jana tangu kipatiwe cheti cha usajili wa muda.
Alisema mafanikio hayo yanaashiria jinsi gani Watanzania walivyoweza kukiunga mkono chama chao.
Kwa hiyo, tumeona kwamba itakapofika tarehe 22, mwezi huu, kama hakutatokea tatizo lingine, ambalo liko juu ya uwezo wetu, tutakwenda kuwasilisha kwa Msajili wa Vyama Siasa, John Tendwa idadi ya hao wadhamini, kwa maana ya wanachama 200 katika kila mkoa katika mikoa 10, alisema Muabhi.
Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCJ, Dickson Amos, alisema wakereketwa wa CCJ Morogoro waliwaomba kadi 3,000.
Katibu Mkuu huyo alisema wanatarajia kufanya uzinduzi rasmi wa CCJ na shughuli zake Machi 21, mwaka huu.
Alisema wameshakamilisha taratibu zote za kiofisi, hivyo wanataka sasa kukitambulisha chama hicho kwa Watanzania kwamba chama chao kiko imara na kiko tayari sasa kwa kazi.
Aliwataka wananchi kujitolea kuiunga mkono CCJ, ikiwa ni pamoja na kujiandikisha kwa wingi, kujitolea ofisi sehemu mbalimbali kutokana na mahitaji yatakayojitokeza kwa sababu chama hicho ni cha wananchi.
Sababu ya kusema kwamba, wao inatakiwa waguswe moja kwa moja na ujio wa CCJ ikiwa ina malengo ya pekee kabisa na ya makusudi kabisa kwamba, imedhamiria kurudisha hadhi ya taifa la Tanzania, ambayo iliasisiwa na Baba yetu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alisema.
Akitilia mkazo suala hilo, Amos, alisema katika uzinduzi huo, watapokea wanachama wapya, ambao baadhi yao wamewahi kushika madaraka makubwa ndani ya vyama vingi vya siasa.
Alisema viongozi wa CCJ wanatarajia kufanya ziara kwenda kuzuru makazi ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, Butiama, wilaya ya Musoma Vijijini, mkoani Mara kesho.
Alisema katika ziara hiyo, wanataka kwenda kuona kaburi la Mwalimu Nyerere na kufanya mazungumzo na familia yake, ikiwa ni sehemu ya kuthamini na kujali mchango wake katika taifa la Tanzania kama muasisi wake.
Alisema wako viongozi wengi nchini, ambao ni waasisi wa taifa, wamekuwa na heshima kubwa, hivyo ilistahili nao wawape umuhimu wa hali ya juu kwa kuwafanyia ziara.
Hata hivyo, alisema wameona kwa sasa wajaribu kuanzia kwa hayati Mwalimu Nyerere, ambaye tayari ana heshima ya pekee, kwa kuwa anatambuliwa rasmi kama Baba wa Taifa.
Kwa hiyo, hata wale waasisi wengine, napenda kutumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kabisa kwamba, tuko nao na tunawathamini na tunathamini michango yao waliyoitoa katika taifa hili, alisema Muabhi. Alisema watakapomaliza ziara ya Butiama kwa Mwalimu Nyerere, watakwenda kufanya mkutano katika eneo walikouawa kikatili watu 17 hivi karibuni, wilayani Musoma ambako watazungumza na wananchi wa eneo hilo pamoja na wazee. Muabhi alisema katika mazungumzo hayo watatoa usia wao kwa wazee hao pamoja na Watanzania wengine juu ya tukio lilitokea hapo kwamba, halikuwa la kawaida na halikustahili kuwapo katika misingi ya kibinadamu.