Tumeamua kususia zoezi la uhakiki :angry: !
Hee hee heee! Mimi sipo huko, nilikuwa natania tu (kama muungwana alivyokuwa anatania kuhusu kitochi) !Nafahamu kuwa mmesusia zoezi,nachotaka kufahamu baada ya kususa what next,mnatoa tena tamko kali kama amabvyo huwa mnadai!au mnafanyaje siku ndio zasonga hivyo.
Siasa si lele mama, Kugomea kujitokeza na kuhakikiwa na wakati awali ulishakubali na ukatahadharishwa kama hukutokea zoezi litaendelea hii ni kupoteza muelekeo.CCJ mambo magumu
Imeandikwa na Wakuru Kuliga, Kibaha; Tarehe: 4th June 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 278;
SIKU moja baada ya kuambulia wanachama 13 Dar es Salaam, Chama cha Jamii (CCJ) kimeshindwa kuwasilisha wanachama wake wa mkoa wa Pwani kwa ajili ya uhakiki.
Hali hiyo ilitokea jana katika vijii vya Picha ya Ndege na Kwa Mathias, Kibaha, ambako ndiko uhakiki ulikopangwa kufanyika kwa ajili ya kutambua wanachama wa mkoa huo.
Hatua hiyo pengine inatokana na kauli ya Mwenyekiti wa CCJ, Richard Kiyabo aliyoitoa juzi katika uhakiki wa wanachama wake wa mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, Dar es Salaam.
Katika kauli hiyo, Kiyabo alisema chama chake hakina imani na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, na hivyo kuhitaji vyama vya hiyari na waangalizi wa kimataifa kushuhudia uhakiki ili kujenga heshima kwa nchi na chama hicho.
Wachunguzi wa masuala ya siasa wanasema hatua ya CCJ kumkataa Tendwa, inaweza ikawa inaipotezea muda, kwani haitakuwa rahisi kwa ofisi nyingine kuendesha uhakiki huo kwa kuwa kisheria ofisi ya Tendwa ndiyo inahusika.
Kwa hali ya kawaida isingekuwa rahisi pia kwa chama kama hiki kilichoibuka kwa kishindo kukosa mwanachama hata mmoja mkoani Pwani, wakati kikijua kwamba uhakiki utafanyika katika mkoa huo ambao ni jirani na Dar es Salaam, yaliko makao makuu yake.
Hiyo inathibitisha kauli ya Kiyabo ya kususia uhakiki na hivyo inawezekana wanachama wakawa wamekatazwa kujitokeza kuhakikiwa, hali ambayo hata hivyo inakiweka katika hali mbaya ya kukosa usajili wa kudumu.
Timu ya uhakiki huo ikiongozwa na Tendwa, ilipowasili jana katika vijiji hivyo, haikukuta mwanachama, kiongozi wala kuona ofisi ya CCJ, mazingira yanayohatarisha usajili wa kudumu wa cghama hicho kilichopania kushiriki uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
"CCJ wamekuwa wakipiga kelele kwamba ofisi yangu inawahujumu, haitaki kuwahakiki, wanataka kuwahi uchaguzi, sisi tumejitolea kuwahakiki ili wafanye uchaguzi, lakini ninyi ni mashahidi hali halisi ya uhakiki ndiyo hii," alisema Tendwa.
Alisema pamoja na nia njema ya ofisi yake kufanya uhakiki wa wanachama wa CCJ ili kama hesabu yao itatosha waweze kukipa usajili wa kudumu, chama hicho kimerudi nyuma na kushindwa kutoa ushirikiano kwa ofisi yake na kukosa wanachama katika mikoa kama yalivyokuwa makusudio yao.
"Sisi tumejitolea tuwahakiki wafanye uchaguzi, kama wao wanarudi nyuma tena, hiyo ni bahati mbaya kwao, nia yetu ni nzuri, tungekuwa na ushirikiano mzuri na wao tungemaliza hii vizuri, kama kungekuwa na mkwamo wowote tungeshirikiana kutatua matatizo hayo," alisema Tendwa.
Msajili alisema CCJ katika uhakiki wa Dar es Salaam juzi hawakufanikiwa, Pwani kwa Mathias na Picha ya Ndege hawapo kabisa, hakuna mtu yeyote anayewajua, hawana viongozi wala ofisi.
Alipoulizwa kuna haja gani kuendelea na uhakiki katika mikoa mingine wakati hali imeonesha kuwa mbaya, Tendwa alisema tayari walishapanga, baada ya CCJ kuleta barua iliyopanga maeneo ya kufanyiwa uhakiki waliyodai wanayamudu na kusisitiza kuwa lazima yote yahakikiwe.
Alisema leo watakuwa Ifakara mkoani Morogoro kuendelea na uhakiki na baada ya hapo, watakwenda Unguja na hatimaye watatoa taarifa ya uhakiki wao.
"Nimechukua jukumu hili mimi mwenyewe, nitatenda haki na kutimiza wajibu wangu, kama watashindwa kujitokeza na mikoa mingine, CCJ watakuwa wameshindwa kutekeleza wajibu wao kama chama cha siasa," alisema Tendwa.
Juhudi za kumpata Kiyabo azungumzie mazingira ya wanachama wake kutojitokeza Kibaha jana kuhakikiwa, hazikuzaa matunda kutokana na simu yake kuita bila kupokewa.
Mwenyekiti wa Chama Cha Jamii (CCJ) Richard Kiyabo, akizuiwa na mlinzi wake wakati akielekea kwenye meza ya msajili wa vyama, John Tendwa kumlalamikia kuhusu zoezi la kuhakiki wanachama wa chama hicho viwanja vya Temeke Mwembeyanga jijini Dar es Salaam jana. Picha na Silvan Kiwale
Hivi kweli CCJ ina Wanachama halali 13 tu Dar nzima? Kaaz kwer kwer!
Watanzania hakuna tunaloliweza; tunashindwa hata kupata watu 200 ambao sio mamluki halafu tunaomba tupewe uongozi wa nchi? Very disapointing!
Waungwana hapa kuna mkono wa sisiemu angalia news hizi-🙂
CCJ kumburuza kortini Msajili vyama vya siasa
NA MOSHI LUSONZO
6th June 2010
Wabaini namba za wanachana kubadilishwa
Uongozi wa Chama Cha Jamii (CCJ), umeibuka na kutoa madai ya kufanyiwa hujuma baada ya kugundua namba za wanachama wake zilizokuwa ndani ya fomu za Msajili wa Vyama vya Siasa nchini zimebadilishwa.
Akizungumza na Nipashe jana, Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, alisema kutokana na kubainika kwa kasoro hiyo, wamepanga kumfikisha Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa mahakamani Jumatatu (kesho) ili asiendelee na zoezi la kuhakiki wanachama wao hadi hapo hali hiyo itakaporekebishwa.
Muabhi alisema, baada ya kuvunjika kwa uhakiki wa wanachama wa Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na watu wengi kuonekana sio halali, uongozi umegundua fomu alizokuwa nazo Tendwa nyingi zimebadilishwa namba pamoja na majina ili kuhakikisha kinashindwa kupata wanachama wa kutosha na kunyimwa usajili ya kudumu.
"Kwa kweli tumebaini kuna njama zimefanyika kwa kubadilisha namba kwenye fomu alizokuwa nazo Msajili, lakini hilo litamalizwa kisheria kwa sababu tunatarajia kwenda mahakamani kupinga mchakato wote wa kuhakiki wanachama hadi hapo totakapokaa na kumaliza tatizo hili," alisema Muabhi.
Katika zoezi hilo lililofanyika Jumatano iliyopita katika Viwanja vya Mwembeyanga, wanachama 40 waliofanikiwa kuhakikiwa kabla ya zoezi hilo kusitishwa, 27 walishindwa kutambuliwa na Msajili baada ya kuonekana sio halali na 13 pekee ndio waliotambuliwa.
"Kitu hiki bado kinatuumiza kichwa sisi kama viongozi wa CCJ, haiingii akilini tuwe na wanachama 13 tu ikiwa tulikuwa na maandalizi ya kutosha kabisa, hili jambo lazima tutakwenda mahakamani ikiwa ni pamoja na kumzuia Tendwa asiendelee kuhakiki wanachama wetu bila ridhaa yetu," alisisitiza.
Aidha, alisema ametoa agizo kwa viongozi wa mikoa yote itakayotembelewa na Msajili kutotoa ushirikiano wowote kwa sababu wao wamejitoa.
Aliwataka wanachama wa chama hicho kutulia kwa kuwa ana matumaini makubwa suala hilo litatatuliwa haraka ili uhakiki huo urudiwe kwa mara ya pili.
Hata hivyo, Tendwa alipozungumza wakati akiendelea na zoezi la uhakiki wa chama hicho Ifakara mkoani Morogoro, alisema fomu alizokuwa nazo ni halali kitu ambacho hata viongozi wa CCJ wanakitambua, bali kinachofanyika sasa ni kulidanganya taifa.
Alisema, anachoendelea kukiona katika ziara yake hiyo ni kitu ambacho hakukitarajia, kwani kuanzia uhakiki wa Mkoa wa Pwani hadi alipofika Ifakara jana hakuweza kumpata hata mwanachama mmoja.
"Nadhani CCJ wanaliongopea Taifa, hawa watu hawana wanachama kama wanavyodai, jambo hilo ndilo nakumbana nalo kwenye ziara yangu kuanzia jana (juzi) Kibaha na sasa Ifakara hali ni hiyo hiyo, japokuwa huku nimeona ofisi yao," alisema.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Waungwana hapa kuna mkono wa sisiemu angalia news hizi-🙂
CCJ kumburuza kortini Msajili vyama vya siasa
NA MOSHI LUSONZO
6th June 2010
Wabaini namba za wanachana kubadilishwa
Uongozi wa Chama Cha Jamii (CCJ), umeibuka na kutoa madai ya kufanyiwa hujuma baada ya kugundua namba za wanachama wake zilizokuwa ndani ya fomu za Msajili wa Vyama vya Siasa nchini zimebadilishwa.
Akizungumza na Nipashe jana, Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, alisema kutokana na kubainika kwa kasoro hiyo, wamepanga kumfikisha Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa mahakamani Jumatatu (kesho) ili asiendelee na zoezi la kuhakiki wanachama wao hadi hapo hali hiyo itakaporekebishwa.
Muabhi alisema, baada ya kuvunjika kwa uhakiki wa wanachama wa Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na watu wengi kuonekana sio halali, uongozi umegundua fomu alizokuwa nazo Tendwa nyingi zimebadilishwa namba pamoja na majina ili kuhakikisha kinashindwa kupata wanachama wa kutosha na kunyimwa usajili ya kudumu.
"Kwa kweli tumebaini kuna njama zimefanyika kwa kubadilisha namba kwenye fomu alizokuwa nazo Msajili, lakini hilo litamalizwa kisheria kwa sababu tunatarajia kwenda mahakamani kupinga mchakato wote wa kuhakiki wanachama hadi hapo totakapokaa na kumaliza tatizo hili," alisema Muabhi.
Katika zoezi hilo lililofanyika Jumatano iliyopita katika Viwanja vya Mwembeyanga, wanachama 40 waliofanikiwa kuhakikiwa kabla ya zoezi hilo kusitishwa, 27 walishindwa kutambuliwa na Msajili baada ya kuonekana sio halali na 13 pekee ndio waliotambuliwa.
"Kitu hiki bado kinatuumiza kichwa sisi kama viongozi wa CCJ, haiingii akilini tuwe na wanachama 13 tu ikiwa tulikuwa na maandalizi ya kutosha kabisa, hili jambo lazima tutakwenda mahakamani ikiwa ni pamoja na kumzuia Tendwa asiendelee kuhakiki wanachama wetu bila ridhaa yetu," alisisitiza.
Aidha, alisema ametoa agizo kwa viongozi wa mikoa yote itakayotembelewa na Msajili kutotoa ushirikiano wowote kwa sababu wao wamejitoa.
Aliwataka wanachama wa chama hicho kutulia kwa kuwa ana matumaini makubwa suala hilo litatatuliwa haraka ili uhakiki huo urudiwe kwa mara ya pili.
Hata hivyo, Tendwa alipozungumza wakati akiendelea na zoezi la uhakiki wa chama hicho Ifakara mkoani Morogoro, alisema fomu alizokuwa nazo ni halali kitu ambacho hata viongozi wa CCJ wanakitambua, bali kinachofanyika sasa ni kulidanganya taifa.
Alisema, anachoendelea kukiona katika ziara yake hiyo ni kitu ambacho hakukitarajia, kwani kuanzia uhakiki wa Mkoa wa Pwani hadi alipofika Ifakara jana hakuweza kumpata hata mwanachama mmoja.
"Nadhani CCJ wanaliongopea Taifa, hawa watu hawana wanachama kama wanavyodai, jambo hilo ndilo nakumbana nalo kwenye ziara yangu kuanzia jana (juzi) Kibaha na sasa Ifakara hali ni hiyo hiyo, japokuwa huku nimeona ofisi yao," alisema.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
KNKU, CCJ walishasitisha zoezi la kuhakikiwa baada ya kugundua alichofanya Tendwa Mwembeyanga. Walitangaza kuwa kwa upande wao zoezi hilo lisingeweza kufanyika. Msajili alijua hivyo lakini aliamua kwenda kuhakiki wanachama ambacho chama chao kimewaambia zoezi limesitisihwa na CCJ haitatoa ushirikiano.. Msajili alitarajia kukuta kina nani huko?
Tatizo la vyama vyetu vya siasa ni kufikiri CCM watakuja kuwapisha madarakani kirahisi. Siasa ni mapambano. CCJ walipaswa kujua kwamba kuna uwezekanao wa kuchezewa shere na wajiandae kuzuia. Hapa tayari mchezo umekwisha. Wanaenda mahakamani, kesi itatajwa Januari 2011, na itaanza kusikilizwa Mei 2011, Halafu?
Halafu wamelipiga mno debe tupo hadi linawatisha washika mpini. Kulikuwa na ubaya gani kufanya haya silently halafu mnaibuka mkishasajiliwa. Sasa mnatisha kabla hamjazaliwa si mnafanya muendelee kubaki mimba, MM hata wewe hii michezo unashindwa kuisoma?
Kifupi ni kwamba CCJ wameshindwa kufanya siasa,walidhani ni rahisi kama kunywa maji.Kumkimbia Tendwa hata kama hawakuwa na imani na Tendwa ni kuionyesha jamii kuwa hawawezi mapmbano na yale maneno ya Mwanakijiji kuwa eti CCJ itafanya yale ambayo vyama vya upinzani vimeshindwa kufanya kwa miaka 15 sasa yanatimia..Pamoja na Ujinga wote wa chama cha PPT Maendeleo lakini wao waliweza kufikia masharti..CCJ ilipaswa kuprove kwa Tendwa kwamba wanachama wanao wa kutosha.Wangekubali tu waionyeshe jamii kuwa wanao kwa huo Mkoa wa Pwani na kwingineko..Chama cha Mahakamani,Mtikila part II.