Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,607
- 3,187
Mtu mmoja wa miaka 47 aliyejulikana kwa jina la Shirima mkazi wa Kibaha, amemuua baba yake mzazi anayekadiriwa kuwa na miaka 70 kwa kumpigarisasi iliyotoka kwenye SMG yake.
Inasemekana baba huyo alikua amelala nyumbani kwa mwanae na alitokea Moshi kwa mualiko wa harusi ya bwana Shirima ambayo ilikwisha fanyikana hapo bwana Shirima na mkewe walikua honeymoon hapo nyumbani kwao.
usiku wa jana baba yake alipatwa na haja ndogo akaenda chooni wakati anarudi akakosea mlango wa chumba chake na kuingia chumbani kwa mwanae ndipo mke wa Shirima aliposikia mlango unafunguliwa na mtu yupo ndani - akapiga kelele za mwizi hapo ndo mumewe akachukua short gun yake na kumlenga babake na kumuua akidhani ni mwizi.
Inasemekana makazi ya bwana Shirima mtaani kwao nyumba zipo mbalimbali ndo mana akachukua uamuzi wa kumimina risasa bila kuuliza hata swali moja kwa mvamizi huyo wa chumbani kwake.
Imenisikitisha sana habari hii, yamkini tuwe waangalifu kabla ya kuchukua uamuziwowote.
SOURCE WAPO RADIO ASUBUHI HII
Ni sawa.ndio maana honeymoon tunahimizwa twende mbali.........
mfanyabiashara maarufu mkazi wa mlandizi, mkoa wa pwani ndugu BON KAVISHE,amemuua babake mdogo kwa risasi majira ya saa 10 usiku nyumbani kwake mlandizi. tukio hilo limetokea siku ya jumamosi kuamkia jumapili ya tarehe 12.05.2013 baada ya kukamilika sherehe ya harusi ya mdogo wake.taarifa zinadai kuwa baada ya sherehe hiyo ndugu jamaa na marafik wakaenda kujipumzisha.ndipo ndugu KAVISHE ambaye ni mmiliki wa bar maarufu hapa mlandizi ya zimbabwe bar alipoenda kujipumzisha nyumbani yeye na babake mdogo, lakin wakati wa usiku babake mdogo akataka aende choon ndipo katka harakati akajikuta ameingia chumbani kwa mwanae na ndipo mke wa kavishe akapiga kelele akidhani ni mwizi na ndugu kavishe kumpiga risasi na kufariki papo hapo.mpaka sasa ndugu kavishe anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi.
Hapo kwenye RED, hivi SMG na shortgun ni kitu kile kile? Kwa sheria za kumiliki silaha za Tanzania, zinaruhusu kweli mtu binafsi kumiliki SMG?
Naomba ufafanuzi hapa!!!!.
Tiba
Ni sawa.
Kwa sie ambao hatuwezi kwenda mbali je?
Ni sawa kabisa. SMG ni submachine gun, na shotgun ni bunduki ambayo risasi ndani yake mna gololi.Muite Dingswayo anajua vizuri. mi nadhani SMG stands for saab machine gun, bunduki inayoweza kutema mfululizo.
Ni kama corolla ni toyota lakini toyota sio lazima iwe corolla
It seems walijiachia sana, hawakufungaIna maana hao maharusi wapya hawakufunga mlango wa chumba chao?
Ok nimekupata BigBro mi bado nipo shule ya kata topic hiyo hatujaifikia
Hiyo ni manslaughter, ameua bila kukusudia!!!! Ni bahati mbaya sana hii.
Tiba
hapana bwana wewe utamiminaje shaba ovyo bila kuangalia kitu unachokipiga au ndo usingizi