Bwana harusi amuua baba yake kwa risasi

Bwana harusi amuua baba yake kwa risasi

ndo maana "wazungu" wanasemaga "stand where you are and put your hands where i can see them or i will shoot you"...sasa huyu hajatoa hata tahadhari yeye kakimbilia kufyatua tu,..
r.i.p mzee
 
wachaga awahaminiki unaweza kuta alikuwa anafanyia taimingi kwa mwanae.R.I.P. Mzee wetu
 
Bwashee Shirima ameitumia silaha yake kujilinda (self defense) ipasavyo kutokana na mazingira ya tukio lenyewe. Lakini pia nafikiri pombe ilichangia kumfanya marehemu akasahau uelekeo wa kwenda msalani.
 
Chezea papuchi wewe!! So sad!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
huyu shirima atakuwa ni ndugu yake na yule aliyejitupa ghorofani pale kariakoo
 
Mtu mmoja wa miaka 47 aliyejulikana kwa jina la Shirima mkazi wa Kibaha, amemuua baba yake mzazi anayekadiriwa kuwa na miaka 70 kwa kumpigarisasi iliyotoka kwenye SMG yake.

Inasemekana baba huyo alikua amelala nyumbani kwa mwanae na alitokea Moshi kwa mualiko wa harusi ya bwana Shirima ambayo ilikwisha fanyikana hapo bwana Shirima na mkewe walikua honeymoon hapo nyumbani kwao.

usiku wa jana baba yake alipatwa na haja ndogo akaenda chooni wakati anarudi akakosea mlango wa chumba chake na kuingia chumbani kwa mwanae ndipo mke wa Shirima aliposikia mlango unafunguliwa na mtu yupo ndani - akapiga kelele za mwizi hapo ndo mumewe akachukua short gun yake na kumlenga babake na kumuua akidhani ni mwizi.

Inasemekana makazi ya bwana Shirima mtaani kwao nyumba zipo mbalimbali ndo mana akachukua uamuzi wa kumimina risasa bila kuuliza hata swali moja kwa mvamizi huyo wa chumbani kwake.

Imenisikitisha sana habari hii, yamkini tuwe waangalifu kabla ya kuchukua uamuziwowote.

SOURCE WAPO RADIO ASUBUHI HII

yesuuuuuuuuuuu Shirima uwe anaangalia vizuri umeona sasa ulichofanya?
 
Mtazamo wangu kwa hili ambalo limeshatokea tayari ni mmoja tu!

Sheria ichukuwe mkondo wake na mambo ya mahakama isiingiliwe!

Lala Baba kwa Amani yake BWANA wetu!
 
umenikumbusha ndugu yangu, sheria mwaka wa kwanza. mistake of fact.
 
Ila na bwana harusi nae analala na smg chini ya mto au? Manake kusikia kelele tu za mkewe akashoot? Ina maana na baba hakutoa sauti yoyote wakamtambua? Nna maswali milioni!
still walilalaje bila kufunga mlango wa chumba chao wakati tayari walikuwa kwenye fungate? maswali ni mengi kuliko majibu iko kama ilipangwa. kama ni bahati mbaya kweli nampa pole maana haitomtoka.
 
Habari nilizopata ni Kwamba alieua sio Bwana Harusi bali ni Kaka wa Bwana Harusi ndie alieua. Habari yenyewe ni kama ilivyoelezwa hapo juu ingawa kuna marekebisho kidogo.
Mauaji hayo yalitokea usiku huo huo walipotoka kwenye harusi, Kama ilivyo ada Mzee Shirima senior na Mwenyeji wake walikua wamekamata kinywaji (yani Bwana Shirima muuaji na Baka yake). Usiku wa manane (sijui saa ngapi), Marehemu alibanwa na haja, na kwa sababu ya ugeni na Pombe alitoka Nje ili kumaliza haja yake, Cha ajabu ni kwamba aliporudi ndani ya nyumba, alikosea mlango na kufungua mlango wa mwenyeji wake ambae labda kwa sababu ya pombe alilala bila kufunga Mlango wa chumba.

Yaliyoendelea ni kama yalivyoelezwa hapo juu.
 
RIP marehemu.. Ila huyu jamaa inavyoelekea ana shabaha ya kufa mtu.. Kama sniper..!
 
Dah! R.I.P mzee shirima.huyu Shirima anatokea maeneo gani huko Rombo?
 
ni kweli Tiba ni bahati mbaya sana, ila huyo jamaa anatakiwa anyanywe hiyo silaha maana atakuja kuimaliza familia siku moja. au wewe tuambie Tiba ni nini?
Hiyo ni manslaughter, ameua bila kukusudia!!!! Ni bahati mbaya sana hii.

Tiba
 
Last edited by a moderator:
Mke wa Shirima aliposikia mlango unafunguliwa na mtu yupo ndani - akapiga kelele za mwizi hapo ndo mumewe akachukua short gun yake na kumlenga babake na kumuua akidhani ni mwizi.

SOURCE WAPO RADIO ASUBUHI HII

Kuna nchi zina sheria kwamba kumpiga risasi mwizi bila kumuonya ni kuua kwa makusudi na unahukumiwa jela. Sheria zinataka kabla hujamfyatulia mtu risasi uzingatie yafuatayo;

1. Uwe umeona sura ya mtu unaetaka kumuua
2. Ufyatue risasi kwa kuwa mtu huyo yuko katika harakati za kukudhuru wewe
3. Uwe na nia ya kufyatua risasi kwa nia ya kumjeruhi asikudhuru au kutoroka sio kumuua (mfano kumpiga risasi ya mguu)

Sheria hizo pia zinatumika kwa Polisi, na ndio maana polisi Marekani watasema neno "Freeze!" kabla ya kufyatua risasi, sio kama hawa askari wetu yeboyebo wanajipigia tu risasi kama mgambo asiyeiva.
 
Back
Top Bottom