Jamani Jamani, dunia imekwisha,
Shemeji yangu (ndugu yake na mume wangu) ameoa mwishoni mwa mwezi April mwaka huu wa 2013 na harusi yenyewe ilifana sana...ilikuwa harusi ya kukata na shoka(naweza sema) kwa manjonjo yaliyokuwapo...kiukweli ilipendeza sana..
Lakini cha kusikitisha hivi majuzi tu huyu shemeji yangu amemfumania mke wake akiwa na mwanaume mwingine live..
Huyo shemeji yangu ni mfanyakazi wa bank hapa dar, na huyo mkewe ni mwalimu huko mkoani, kwa hivo baada ya kufunga ndoa na honeymoon kumalizika wife akarudi kazini kwake, na Mr akaendelea na kazi kama kawaida huku akihangaika kutafuta uhamisho wa mkewe aje jijini dar, au ikishindikana yeye ahamie huko mkoani alipo mkewe..
shemeji yangu alikuwa akienda huko alipo wife au mkewe anakuja dar wanapopata nafasi..Sasa siku moja shemeji yangu akaamua kwenda kwa mkewe kwa supraise, hakumwambia wife kama anaenda..alifanya hivyo ili kumfurahisha mkewe na kuongeza mapenzi kati yao hakujua kuwa atakutana na msiba badala ya furaha aliyotegemea..yeye anasema hakuwa anamhisi mkewe chochote na wala hakuwahi kufikiria kama mkewe anamsaliti
shemeji yangu huyu akaenda shopping ya nguvu kamnunulia wife zawadi, nguo, na makochokocho kibao..bila kusahau shoping ya vyakula mbalimbali...huyoo akawasha gari kwenda kwa wife kimya kimya bila kumwambia kama anaenda..akitegemea kumfurahisha mkewe na yeye mwenyewe kufurahi,...alipofika ilikuwa jioni mida ya saa 12 ivi jua halijazama na milango ilikuwa wazi (imerudishiwa tu haijafungwa) akaingia hadi chumbani akiwa na hamu ya kumuona mke wake kwa surprise na kupokelewa mazawadi aliyobeba..
Ghafula kuingia chumbani akakuta sinema live, wife akiwa na mwanaume mwingine wako bize kitandani...HEEE..LA HAULA..SHEMEJI YANGU NUSURA acolapse..lkn alijikaza kiume huku akitumbua macho asiamini kinachotokea...na wao kuona hivo wakasitisha zoezi na kubaki wanatumbua macho...uzuri shemeji yangu hakukurupuka kwa hasira na kuanza kuleta vurugu lkn alitoka nje na kuwafungia ndani na kuita majirani...walipofika wakakuta wameshavaa nguo huku bi harusi akilia na kuomba msamaha sana...
mbele ya majirani wazee waliwaambia kila mmoja aandike maelezo na kuweka sahihi yake akikiri kufumaniwa ambapo wote walifanya hivo na shemeji yangu naye akaandika maelezo jinsi alivyowakuta na wakasaini wote...
shemeji yangu akaondoka hapo nyumbani na kwenda kulala hoteli akisubiri kesho yake arejee dar.. ndipo alipowapigia simu ndugu zake na kuwaeleza alichokikuta na hatua waliyofikia ya kuandikisha na wote wakasaini..mpaka hapo alikuwa hajamuuliza wife wake chochote na wala hajamsemesha huyo mgoni wake..walipoandika maelezo na kusaini akawashukuru wazee na kuondoka zake...
kufika dar ndugu wameitisha kikao na mwenye mke amesema ndoa imefikia ukingoni wala hataki kikao na ndugu za mke wake wala hataki kumwona huyo mwanamke tena.(labda ni hasira baada ya muda zitapungua) ila imemdisturb sana..
huyu shemeji yangu kwa sasa hapendi kusocialize kama zamani,muda mwingi yuko peke yake, amekonda ghafla, sijui hali chakula, kazi anataka kuacha japo hajapata kazi nyingine (anaona aibu jinsi watu walivyohangaika kumchangia) leo hii hata miezi 6 haijafika ndoa imevunjika..
Kwa nature yake ni mchangamfu sana, lkn siku hizi amekuwa mkimya sana..ninaamini atakuwa anaumia sana ndani kwa ndani...
sijui tufanyeje katika kumsaidia maana kwa jinsi alivyo anaweza kucomit hata suicide, mawazo yenu jaman
Shemeji yangu (ndugu yake na mume wangu) ameoa mwishoni mwa mwezi April mwaka huu wa 2013 na harusi yenyewe ilifana sana...ilikuwa harusi ya kukata na shoka(naweza sema) kwa manjonjo yaliyokuwapo...kiukweli ilipendeza sana..
Lakini cha kusikitisha hivi majuzi tu huyu shemeji yangu amemfumania mke wake akiwa na mwanaume mwingine live..
Huyo shemeji yangu ni mfanyakazi wa bank hapa dar, na huyo mkewe ni mwalimu huko mkoani, kwa hivo baada ya kufunga ndoa na honeymoon kumalizika wife akarudi kazini kwake, na Mr akaendelea na kazi kama kawaida huku akihangaika kutafuta uhamisho wa mkewe aje jijini dar, au ikishindikana yeye ahamie huko mkoani alipo mkewe..
shemeji yangu alikuwa akienda huko alipo wife au mkewe anakuja dar wanapopata nafasi..Sasa siku moja shemeji yangu akaamua kwenda kwa mkewe kwa supraise, hakumwambia wife kama anaenda..alifanya hivyo ili kumfurahisha mkewe na kuongeza mapenzi kati yao hakujua kuwa atakutana na msiba badala ya furaha aliyotegemea..yeye anasema hakuwa anamhisi mkewe chochote na wala hakuwahi kufikiria kama mkewe anamsaliti
shemeji yangu huyu akaenda shopping ya nguvu kamnunulia wife zawadi, nguo, na makochokocho kibao..bila kusahau shoping ya vyakula mbalimbali...huyoo akawasha gari kwenda kwa wife kimya kimya bila kumwambia kama anaenda..akitegemea kumfurahisha mkewe na yeye mwenyewe kufurahi,...alipofika ilikuwa jioni mida ya saa 12 ivi jua halijazama na milango ilikuwa wazi (imerudishiwa tu haijafungwa) akaingia hadi chumbani akiwa na hamu ya kumuona mke wake kwa surprise na kupokelewa mazawadi aliyobeba..
Ghafula kuingia chumbani akakuta sinema live, wife akiwa na mwanaume mwingine wako bize kitandani...HEEE..LA HAULA..SHEMEJI YANGU NUSURA acolapse..lkn alijikaza kiume huku akitumbua macho asiamini kinachotokea...na wao kuona hivo wakasitisha zoezi na kubaki wanatumbua macho...uzuri shemeji yangu hakukurupuka kwa hasira na kuanza kuleta vurugu lkn alitoka nje na kuwafungia ndani na kuita majirani...walipofika wakakuta wameshavaa nguo huku bi harusi akilia na kuomba msamaha sana...
mbele ya majirani wazee waliwaambia kila mmoja aandike maelezo na kuweka sahihi yake akikiri kufumaniwa ambapo wote walifanya hivo na shemeji yangu naye akaandika maelezo jinsi alivyowakuta na wakasaini wote...
shemeji yangu akaondoka hapo nyumbani na kwenda kulala hoteli akisubiri kesho yake arejee dar.. ndipo alipowapigia simu ndugu zake na kuwaeleza alichokikuta na hatua waliyofikia ya kuandikisha na wote wakasaini..mpaka hapo alikuwa hajamuuliza wife wake chochote na wala hajamsemesha huyo mgoni wake..walipoandika maelezo na kusaini akawashukuru wazee na kuondoka zake...
kufika dar ndugu wameitisha kikao na mwenye mke amesema ndoa imefikia ukingoni wala hataki kikao na ndugu za mke wake wala hataki kumwona huyo mwanamke tena.(labda ni hasira baada ya muda zitapungua) ila imemdisturb sana..
huyu shemeji yangu kwa sasa hapendi kusocialize kama zamani,muda mwingi yuko peke yake, amekonda ghafla, sijui hali chakula, kazi anataka kuacha japo hajapata kazi nyingine (anaona aibu jinsi watu walivyohangaika kumchangia) leo hii hata miezi 6 haijafika ndoa imevunjika..
Kwa nature yake ni mchangamfu sana, lkn siku hizi amekuwa mkimya sana..ninaamini atakuwa anaumia sana ndani kwa ndani...
sijui tufanyeje katika kumsaidia maana kwa jinsi alivyo anaweza kucomit hata suicide, mawazo yenu jaman