BVR hatimae ndani ya Dar

BVR hatimae ndani ya Dar

ila hili zoezi linahitaji moyo!! kwani kujiandikisha tu utadhani unaomba uraia wa USA!!Leo njoo unapewa namba, then kesho ndio uje kupigwa picha, na unakutana na wengine waliopewa namba juzi hawajaisha unaambiwa tena rudi kesho, yaani ni full shida kama huna nia ya dhati kuwa liwe jua iwe mvua lazima nipate kisu cha kumchinjia mkoloni mweusi, mbona unashindwa tu. Mimi nilikaa na namba mkononi siku 3!!ndio nakuja iona hiyo mashine live!! naanza tu kuigusa mala ohho imegoma njoo kesho!! nikawa mpole kesho yake ndio napata kadi, ni shida mno, tena kama dsm sijui kwani kila siku ni mishemishe umwambie mtu leo tunatoa kadi tu urudi kesho, yaani siku 2,mtu lazima upoteze kwa ajili ya bvr!! kama ni mkakati wao wa kuacha watu wengi wasijiandikishe wamefanikiwa, Eti unamsikia kiongozi wa Tume ya uchaguzi kuwa wamevuka malengo!!? kivipi sasa, kwani unakuta kijiji kina wakazi 5000,wamepewa mashine 4,kila mashine kwa sasa hata watu 100,kwa siku haziandikishi, na ni siku 7 tu!! sasa hayo malengo wanayoyavuka ni yapi jamani??!
 
Jamani ndo tuko kwenye vituo tulivyopangiwa kwa ajili ya training

Vipi ndugu zetu Wengine na nyie mshafika vituoni
Uonapo taarifa Hii please mjuze na mwingine
Me natoka kata ya BUNJU kinondoni D's.m
Naomba kuwasilisha
asante , mimi niko tandika mwembeyanga karibu na transfoma , nakutuma fikisha ujumbe kwa huyo mzee lubuva , hapa dar hatutaki na wala hatutaruhusu magumashi ya kiwango chochote , mwambie kwamba kwa umri alonao ( inasemekana anakaribia miaka 100 ) kwanza anatakiwa amshukuru Mungu kwa kumfikisha umri huo , lakini la msingi zaidi anatakiwa kumtukuza sana Mungu aliyemlinda hadi leo kwa kutenda haki .
 
Ni kweli mkuu
Ila kama ni siku 7 kwa mkoa Wa dsm hazitoshi kwani ndogo saba mkuu
 
Haya mkuu
Zimefika jaji mstaafu ataambiwa]
 
Safi sana, tutajiandikisha kwa wingi.

asante , nawaasa watu wa dar ule wakati wa kudanganywa kwa ofa za vichwa , miguu ya kuku na ile mihogo iliyotiwa chachandu umekwisha , jitokezeni kwa wingi sana .
 
asante , nawaasa watu wa dar ule wakati wa kudanganywa kwa ofa za vichwa , miguu ya kuku na ile mihogo iliyotiwa chachandu umekwisha , jitokezeni kwa wingi sana .


Wewe punguani watu wa Dar tunajielewa, si kama misukule wanaochangishwa kwenye vibakuli halafu wajanja wanaenda kujengea mahawara zao hapo hapo Dar.

Ukiona mtu wa Dar anashobokea watu kijinga ujuwe huyo ni wakuja kama wewe.
 
Wewe punguani watu wa Dar tunajielewa, si kama misukule wanaochangishwa kwenye vibakuli halafu wajanja wanaenda kujengea mahawara zao hapo hapo Dar.

Ukiona mtu wa Dar anashobokea watu kijinga ujuwe huyo ni wakuja kama wewe.
Assalam aleykum,habar ya swaum,habar ya EID.
 
Back
Top Bottom