Buzwagi: Lowassa Alikuwa London Siku Ya Mkataba

hii habari ukifuatilia vizuri ndio inamake sense.

nov-dec 2006 karamagi na el walikubali share fulani fulani toka barrick wakiwa canada kuhusu buzwagi kama wakisuspend new mining regulations. also barrick wanted them to sign contracts in areas where the law will challenge tz laws.

more to come
 
Huyu mkuu sasa amefikia mahali kila fanyalo ni aibu tupu, majuzi amejaribu kumtumia Kingunge kwenye kamati kuu, kuwaondoa wabunge wawili "waliokamatwa", na rushwa, cc nzima ikamzomea,

Aibu mtu mzima kufokewa na Muungwana, eti usituletee mahotuba hapa sema haraka hoja yako, mkuu akaambiwa hawafukuzwi mpaka kesi iiishe, kwa hiyo tulia chini! na yule mtu wako mwenyekiti wa wilaya, mwambie aache ujinga ninayajua yote!

Nasikia mkakati umeanza rasmi wa kumpromote Mwandosya, kwa hali na mali.....!
 
Mkuu FMES,

Naona unatuwekea ka-skeleton tu, ongezea basi na ka-beef japo kidogo ili angalau tupate picha japo kwa mbali.

Ninafarijika iwapo CC wamegundua kwamba huyu jamaa ana matatizo. Pamoja na hayo sijaona kama wamewatendea haki kwa kukubali kuendelea na uchaguzi wakati kesi haijaisha.

JK atakuwa ametumia busara ya kutosha kwa kugoma kuwafukuza wakati kesi haijaisha. Maana wangefukuzwa halafu wakashinda kesi ingekuwa ni aibu kubwa kwa CCM kwa kuwa lazima wangeonekana wanaendesha CCM kwa majungu yanayopikwa na wakubwa walio ndani ya CC.

Mwandosya anakuwa promoted ili awe PM? Je, wana mtandao watamkubali? Naona hapo kuna vita nyingine kubwa inaandaliwa ndani ya CCM. Lakini uwepo wa vita within CCM itasaidia kuboresha demokrasia na kupunguza kuburuzana. Kitu muhimu ni kwamba CC inatakiwa kuwa makini zaidi na hasa JK mwenyewe ili asije akaendeleza yale ya BWM ya ku-entertain majungu at the expense ya kumpandisha mtu chati na hivyo kuwaacha potential candidates!
 
Naona unatuwekea ka-skeleton tu, ongezea basi na ka-beef japo kidogo ili angalau tupate picha japo kwa mbali.

Mkuu nilizozipata, ni kwamba sasa hivi kuna mchuano mzito kati ya Membe, na Lowassa, wajumbe wengi wa cc, na wabunge, wanaridhika na kazi ya Membe, kama waziri wanasema he is doing a fine job, lakini kwenye kushika kaya hawawataki wote wawili, kwa hoja kwamba waliyoyaona na Mtandao, tayari yanatosha,

kwa hiyo waliamua kwa kauli moja na kumshinikiza Mwandosya, kugombea NEC, ili waanze kumtayarisha, nasikia huko Mbeya, kijana Tom alikuwa akishindana na almost 75%, ya cc na wabunge wa ccm, ndio maana hakuweza kuona ndani na alibidi akubali baada ya uchaguzi kuisha maana aligundua mwishoni mwiba uliomchoma,

Nasikia wenye uchungu na nchi sasa ni kumfagilia tu Mwandosya, mipango imeshaanza siku nyingi!

Kingunge alipojaribu kuleta kidomo domo, alinyamazishwa na hoja iliyotolewa na makamu na kuungwa mkono na Mama Zakhia, na mjumbe mmoja kutoka Zanzibar, na wajumbe wote baadaye, Hoja ni kwamba wabunge ni wamasai, wakati Lowassa, sio Mmasai, nasikia aliambiwa hii live huko ndani, akaambiwa kuwa wa-Mmasai huipigia kura ccm kwa asilimia 99.9%, hawajawahi kuwapigia upinzani, akambiwa kuwafukuza wabunge hao ni kuwapa Chadema majimbo ya bure maana watajiunga na Chadema na kugombea na watashinda, Muungwana akaulizwa kama anafahamu ni wa-Massai wangapi wanaoenda mahakamani kila hiyo kesi inaposomwa, akapewa namba rasmi, Muungwana, akaamuliza Kingunge, kama ameshawahi kwenda kwenye jimbo wakati wa uchaguzi mdogo wowote ule? Jawabu hakuna, akaambiwa yeye na ndugu yake wanyamaze, na hafukuzwi mtu!

Ahsante Mkuu!
 
Huyu Mwandosya kama CCM itajirekebisha na kurudisha credibility yake kwa wananchi, basi anaweza kuwa mgombea wa CCM hapo 2010. Mimi simfahamu vizuri lakini watu wengi aliowahi kuwafundisha pale UDSM na waliobahatika kufanya kazi naye wanasema ni mchapa kazi hodari.

Kama na yeye ana madudu yake basi aanze kujisafisha haraka sana kabla wanamtandao hawajaanza kumchafua. Kikwete hana credibility tena na kamwe hawezi kuirudisha na hivyo CCM hawatamkubali awe mgombea wao 2010 hata akija na akina Manji 50!
 
Mkuu wa Kasungura, anaendelea kuwa kichekesho, maana nasikia wabunge walipiga mahesabu ya jinsi taifa linavyotumia mapesa mengi kwa ajili ya umeme ambao ni temporary tu, na sio wa kudumu,

Wakuu nimeshitushwa kuambiwa kuwa mahesabu yanaonyesha kuwa toka utawala huu uingie, tumeshatumia hela za kutosha kujenga mabwawa mengine kama 22, yanayofanana na Mtera, nasikia alipogundua kuwa huenda wataiweka hoja hiyo bungeni, akawawahi kwa kumtuma Mama anyeitwa Buriani, ili kuwatisha wabunge, kuwa kama wana hoja wakaisemee ndani ya ccm na kweli wabunge wakanywea,

Halafu Kasungura, tena kakamtuma Mundhihir aanzishe hoja ya kumfukuza Zitto, yaani huyu atakuwa rais gani jamani? Dataz... zinasema yeye na Muungwana, sasa ni uhusiano wa kazi tu, ushikaji uliisha siku nyingi......!
 
Bubu,

Unataka kusema wanamuandaa Mwandosya kwa ajili ya 2010? Kama ni kwa ajili ya 2010, hapo naona swala hili linaweza kuwa tete zaidi kwa kuwa CCM huwa wana tabia ya kuachiana mpaka mihula yote miwili iishe. Nakumbuka 2005 Mh. Dr Mohamed Gharib Bilal "inasemekana" aliombwa ajitoe ili amwachie Karume amalizie miaka yake 5 ya awamu ya pili.

Kwa hiyo wenye agenda ya kum-promote Mwandosya wanaweza kuwa right kama wanaangalia 2015 na siyo 2010. Kama ni 2010 sidhani kama JK na kundi lake wanaweza kukubali hilo. Bahati mbaya JK ni mwenyekiti na ninadhani ana power zaidi kama tulivyoonyeshwa kwenye dosier ya Mzee Butiku maguvu ya mwenyekiti aliyetangulia na hasa kama atataka kuyatumia kwa manufaa yake au kundi lake.
 
Dataz... zinasema yeye na Muungwana, sasa ni uhusiano wa kazi tu, ushikaji uliisha siku nyingi......!

Kama JK na EL wamebaki na uhusiano wa kazi tu na kuweka ushikaji pembeni .... inakuwaje JK aendelee kumkumbatia mtu ambaye ame-proved failure katika maana ya kwamba ameshindwa ku-deliver completely. Kama ni kwa vigezo basi watu wanasema ni heri hata ya Mzee Zero a.k.a Masikio.

Au JK bado anambeba kwa kuwa ni mwanamtandao na hivyo anahofia kuleta balaa in case akimtosa EL?
 
Mimi sijasoma mkataba wote wa Buzwagi, lakini kutokana na tathmini ya LISSU na watanzania wengine naona wazi kabisa kuwa mkataba huo hauna maslahi kwa Taifa, na Karamagi is not a fool who can sign that kind of Contract. NI lazima kuna kitu kingine kilicho nje ya mkataba ambacho bado hatukijui, kwa hiyo nakubaliana na wanaosema kuna uwezekano kuwa beneficiary wa blunder hiyo ni hao watu wa juu ambao mpaka sasa wanamlinda Karamagi.
 
...binafsi niliamini siku nyingi zilizopita kuwa uhusiano wa JK na EL ulikuwa umekwisha!

Nataka kuamini kuwa atamtosa rasmi wakati wa kikao cha bunge mwezi ujao, kwani wakati huo bunge litaweza kuidhinisha jina la Waziri Mkuu mpya, Mizengo Kayanda Pinda!
 
...binafsi niliamini siku nyingi zilizopita kuwa uhusiano wa JK na EL ulikuwa umekwisha!

Nataka kuamini kuwa atamtosa rasmi wakati wa kikao cha bunge mwezi ujao, kwani wakati huo bunge litaweza kuidhinisha jina la Waziri Mkuu mpya, Mizengo Kayanda Pinda!

Mwanamageuzi,hii habari ya moto au ndio udaku.lets wait and see,
 
I wasn't aware of the background info surrounding this Buzwagi issue, it is quite deep and far reaching, JF kweli shule! I can now see why the PM's London "shopping trip" is being viewed with suspicion and rightly so.
 
habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

Source:Mwanahalisi

Huyu FISADI PAPA eti ndiye awe rais, haiwezekani kabisaaaaa
 
Huyu FISADI PAPA eti ndiye awe rais, haiwezekani kabisaaaaa

na kikwete alikuwepo ? aisee,wewe uwezi sema aiwezekani kwa sababu una kura za watanzania..hata mama yako akifunguliwa tigo pesa ndani ya ccm ataiba..tatizo ni ccm..
 
habari za kuaminika kutoka London zinasema ya kwamba ,mheshimiwa Lowassa alikuwapo London 17 februari mwaka huu,siku ambayo mkataba wa Buzwagi ulitiwa saini,
Lowassa aliingia London tarehe 16 february akitokea Paris,Ufaransa ambako alikuwapo kikazi kwa muda wa siku nne,pia mheshima Lowassa alifikia katika Hoteli ya Churchil hill jijini Londoa ambako waziri karamagi alikuwa amefikia.
na katika Hoteli hiyo ndipo mkataba wa buzwagi uliposainiwa,
akiwa London,Lowassa alipokutana na watendaji wa serikali waliokuwa na Rais kikwete na kwa Upole wakamuuliza 'Mheshimiwa huko hapa?'Basi naye akawaambia alikuwa amekwenda kufanya Shopping..na kabla ya hapo alimpigia Balozi wa London na kumuelezea kwamba anakuja Lodnon ila asimpangie chumba..

Je kwa maelezo haya,kwa kuwa Lowassa alikataa asifanyie booking ya chumba ,je wana wa watanzania hamuoni tayari kuna mazingira tata kuhusus mkataba huu?

huyu Lowassa ana nia gani na SISI?

Source:Mwanahalisi

itakuwa vizuro either waseme gazeti hilo husema uongo au lowasa hakuwepo siku hiyo... wakithubutu hivyo na mimi nitajiunga ukawa na kadi nipewe???
 
Kwani kuwepo london,na mkataba kuna usiana nini?kama mkataba ungefungiwa dar na viongozi wote wanaishi dar ungeongea hayo?
 
Back
Top Bottom