JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Kupitia Ukurasa wake wa X (Twitter), Fortunatus Buyobe ameitag taarifa ya SwahiliTimes kuhusu Mjane kurejeshewa umiliki wa nyumba aliyoilalamikia hivi karibuni, kisha Buyobe akaandika:
Kamishna wa ardhi mkoa wa Dar es Salaam hakutakiwa kubaki ofisini baada ya hili. Huyo aliyekuwa anamtoa kinguvu kwenye nyumba kachukuliwa hatua gani? Madalali waliohusika wamechukuliwa hatua gani?
==============================
TAARIFA YA SWAHILITIMES
Mjane Alice Haule aliyevamiwa na kuondolewa nyumbani kwake kwa nguvu na mfanyabiashara Mohamed Yusufali, amerejeshewa hati ya nyumba kama msimamizi wa mirathi ya marehemu mume wake, Justice Rugaibula.
Yusufali alisema alinunua nyumba hiyo iliyopo Mikocheni, Dar es Salaam kutoka kwa marehemu kabla ya kifo chake Mwaka 2011.