Bure: Fursa ya mwaka, pima afya yako

Bure: Fursa ya mwaka, pima afya yako

Zainab Tamim

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2015
Posts
1,293
Reaction score
583
Hakuna kitu chenye umuhimu kwetu binaadam zaidi ya afya zetu. Afya njema haina thamani ya kuinunulia (priceless). Usione taabu wala uvivu kupima afya yako. Sasa una fursa ya kupimwa bure kabisa, itumie fursa hii kama unajijali.

Kupima afya yako si lazima uwe mgonjwa au unaumwa, tunaweza kujiona tuko fit kabisa lakini kumbe kuna vijimaradhi vinatunyemelea na hatujui. Njia rahisi kabisa ya kujua afya zetu ni kupimwa mara kwa mara kitaalam.

Hii ni fursa kwa kila anayeijali afya yake. Kituo kipya cha afya kinachopima afya ya mwili wako wote (whole body checkup, bure bila kulipia, kimeleta offer hii ya muda. Na vipimo ni vya kisasa na kwa njia ya computer.

- Utapimwa bure.
- Utapewa ripoti yako bure.
- Utapewa ushauri wa bure.

Na wakati unasubiri au baada ya kupimwa, unaweza kuchukua fursa ya kuchuliwa mwili wako na kochi letu kuchuwa (massage sofa) bure.

Unachotakiwa ni kuwasiliana nasi kwa PM kwa maelezo zaidi au mpigie simu Mzee Abdul 0756803528 atakupatia namba ya appointment.

Asante.
 
Kama mna nia ya kweli mbn hamko wazi Mpaka tuwa PM? Bado haitakuwa bure.

Ndugu yangu tuwe wazi vipi zaidi ya hivi? Tuna njia njema kabisa ya kutangaza kituo chetu kipya cha afya na ndio maana tunatoa offer ya bure (kwa muda) ya kupima afya za watu bure.

Haulipii chochote. Na ukipata majibu ya kutoka kwetu unaweza kwenda kwengine ukapata "opinion" zingine.

Katika mambo yanayohusu afya za watu mara nyingi huwa haipendezi kuyaanika ndio maana tumesema unaweza kutu PM kwa maelezo zaidi au kutupigia simu. Lakini kama wewe mwenyewe binafsi yako umeridhia yako kuwa wazi unaweza kuuliza chochote upendacho kuhusu hili na tutakujibu kiuwazi kabisa.

Hii ni fursa nzuri sana kwa wapendao na kujali afya zao.

Kwenye kituo tunatoa huduma nyingi za afya lakini nimeona kwa hivi sasa niwajulishe kuhusu hii offer ya bure. Huduma zingine tunazotoa nitaziorodhesha baadae.

Karibuni.
 
Nami nahitaji pia, vipi bado nafasi zipo?

Tupo Msasani karibu ya TANESCO, (njia ya kwenda kwa Mwalimu Nyerere) siku za kupima ni Jumanne, Alhamisi na Jumamosi saa tatu asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni, Jumamosi ni saa tatu asubuhi mpaka saa nane mchana.

Ukiwa tayari nijulishe nikupe namba ya appointment.

Free of Charge.

Asante









 

Tupo Msasani karibu ya TANESCO, (njia ya kwenda kwa Mwalimu Nyerere) siku za kupima ni Jumanne, Alhamisi na Jumamosi saa tatu asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni, Jumamosi ni saa tatu asubuhi mpaka saa nane mchana.

Ukiwa tayari nijulishe nikupe namba ya appointment.

Free of Charge.

Asante










kama nilivyosema ni kwamba nahitaji kweli, so naomba hizo namba, pia usitume PM, ahsante!
 
kama nilivyosema ni kwamba nahitaji kweli, so naomba hizo namba, pia usitume PM, ahsante!

Kama si kwa PM itabidi utupe namba ya mobile phone tukutumie kwa sms hatuwezi kuweka namba ya appointment wazi kwani inaweza kuleta mchanganyiko wa namba moja kutumiwa na watu wengi na kuleta usumbufu. Ni tahadhari tu.

Asante.
 
Kama si kwa PM itabidi utupe namba ya mobile phone tukutumie kwa sms hatuwezi kuweka namba ya appointment wazi kwani inaweza kuleta mchanganyiko wa namba moja kutumiwa na watu wengi na kuleta usumbufu. Ni tahadhari tu.

Asante.

catch me there
0715494271
 
Kwanza Jazzaka Allah kheyrn (Mungu akujaze kheri) kwa kujitolea... Wema huo uwe uzito ndani ya mizani yako...Allahuma Amn.

Sasa tuambie muhula wa mda gani mtatoa FOC.....

Shukraan bint Al-Tamimmie..
 
Kwanza Jazzaka Allah kheyrn (Mungu akujaze kheri) kwa kujitolea... Wema huo uwe uzito ndani ya mizani yako...Allahuma Amn.

Sasa tuambie muhula wa mda gani mtatoa FOC.....

Shukraan bint Al-Tamimmie..

Amin.

Tunafanya kila njia huduma hii iwe endelevu, tuombeane Mungu atupe uwezo. Kwa kuanzia tutafanya mwezi mzima na tutatangaza tena kabla mwezi haujaisha kama tutaendelea zaidi au la. Yote itategemea na matokeo ya zoezi hili la mwanzo.

Tupo Msasani karibu ya TANESCO, (njia ya kwenda kwa Mwalimu Nyerere) siku za kupima ni Jumanne, Alhamisi na Jumamosi saa tatu asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni, Jumamosi ni saa tatu asubuhi mpaka saa nane mchana.

Ukiwa tayari tujulishe tukupe namba ya appointment. Namba za appointment tunatoa kwa simu au PM tu.

Free of Charge.

Asante




 
thanks, nimeipata, nije lini au kwa nafasi yangu?

Hiyo nimekuwekea nafasi kesho. Kama utabadili nijulishe mapema, unaweza kuja Alhamisi na Jumamosi namba hiyo hiyo nitakubadilishia siku tu.
 
Pia napenda kuwafahamisha kuwa katika kituo chetu cha afya tuna wataalamu wa kutoka China wakishirikiana na wa Tanzania.

Nilisahau kuwajulisha hilo.

Na baada ya muda si mrefu tutakuwa na kipimo cha CT Scan cha bei nafuu kabisa. Mashine ya CT Scan imeshafika tunamalizia taratibu za installation na uthibitisho wa TFDA. Tutawajulisha itapoanza kazi.

Asante.
 
Hiyo nimekuwekea nafasi kesho. Kama utabadili nijulishe mapema, unaweza kuja Alhamisi na Jumamosi namba hiyo hiyo nitakubadilishia siku tu.

ok, tuombe uzima, tukijaliwa nitafika natamani uwe mwenyeji wangu, pia sina route za msasani sijajua nishuke kituo gani mkuu?
 
ok, tuombe uzima, tukijaliwa nitafika natamani uwe mwenyeji wangu, pia sina route za msasani sijajua nishuke kituo gani mkuu?

Ni Msasani barabara ya kwenda kwa Mwalim Nyerere (Old Bagamoyo Road), unashuka TANESCO, sina uhakika wa route ya mabasi, tena umefanya vyema itabidi kesho niulizie route za mabasi.

Ninaomba kama kuna mwenzetu anaejua hiyo route ya kufika TANESCO iliyo mbele ya TMJ Hospital kama unaeekea Kwa Mwalimu Nyerere atuelekeze.
 
Mnatibu meno?..

Tafadhali ningependa orodha ya huduma mtoazo kituoni kwenu..
 
Back
Top Bottom