Bungeni tumepeleka vichaa, wendawazimu au mateja?

Bungeni tumepeleka vichaa, wendawazimu au mateja?

They reflect the society maana ndio inayo wapeleka huko bungeni. Kwa maana taifa letu jimejaa............
 
Utaujua UJUHA/UPUMBAVU wa mtu kwa kuangalia anavyotumia muda wake kufanya yale anayotarajiwa kufanya kwa wakati huo. Kwa upande wa wabunge (WAWAKILISHI) - mbunge asiye mpumbavu ni yule anayetumia muda wake kutetea maslahi ya wananchi waliomtuma (ndani na nje ya jimbo lake) na kushiriki kuhakikisha chombo kinachoitwa Bunge kinatumika kuiondoa Tanzania na Watanzania hapa pabaya tulipo. Anayefanya kinyume na hayo ni mpumbavu.
 
Wala haihitaji uwe mwenye akili za ajabu kujua kwamba ukosefu wa heshima kati ya wabunge na wabunge, na wabunge na uongozi wa bunge umetokana na jinsi Makinda na Ndugai wanavyoliendesha bunge. Mambo yaliyolifikisha Bunge letu katika hadhi iliyopo ni kama yafuatavyo;

1. Utaratibu wa hila na ubinafsi uliotumika kumpata Spika wa sasa na kumwondoa Spika aliyekuwapo kabla yake
2. Kuruhusu wabunge wa chama tawala kukejeli na kuonyesha dharau kwa kila kauli au hoja inayotolewa na wabunge wa vyama vya upinzani
3. Wabunge wa chama tawala kutoelewa wajibu na kazi ya chama cha upinzani bungeni
4. Matumizi ya kanuni na taratibu za bunge katika namna ya kuwanyima uhuru wa uwakilishi wao wa kibunge wabunge wa vyama vya upinzani
5. Kuruhusu kanuni na taratibu za Bunge zivunjwe na wabunge wa chama tawala bila uongozi wa bunge kukemea au kuchukua hatua yeyote
6. Tabia ya wabunge wa chama tawala kuunga mkono au kushabikia kila kauli na hoja inayotolewa na wabunge wenzao wa chama tawala, hata kama kauli au hoja hiyo haina maslahi kwa taifa na wananchi
7. Kutumia nafasi ya uongozi wa Bunge kwa maslahi ya chama tawala na Raisi badala ya taifa na wananchi kwa ujumla.

Kauli na vitendo visivyo vya kawaida tunavyovishuhudia bungeni ni matokeo tu ya mambo hayo saba yaliyoorodheshwa hapo juu. Ikiwa Makinda na Ndugai wana nia ya kweli ya kurejesha heshima ya Bunge machoni pa wananchi wanapaswa kushughulikia mambo hayo, vipengele 2-7. Hii itasaidia kujenga heshima kati ya wabunge wenyewe, wananchi kuwaheshimu wabunge na Bunge.
 
One session of Tanzania Parliament is enough to tell you that some dogs are more reasonable than their keepers.
 
Nikifuatilia mijadala bungeni, nimeona mara nyingi kauli zikitolewa toka vyama vyote, chama tawala na vyama vya upinzani, kwamba tuna wabunge wapumbavu. Baadhi ya viongozi wamekuwa wakichachamaa na kusema kuwaita wabunge au viongozi wa serikali wapumbavu ni kwenda mbali mno.

Najua kwamba Biblia inatumia neno mpumbavu, na ninaamini Biblia ni kitabu kitakatifu, si kitabu cha matusi. Kwa hiyo basi, kama tuna wabunge wapumbavu yawapasa wabunge walikubali hilo na kurekebisha upumbavu wao badala ya kulalamika kwamba wanatukanwa.

Labda kwanza wana Jamii Forum, kama kioo cha jamii, tunapaswa kuwaeleza hawa Wabunge wetu (nachelea kuwaita waheshimiwa, maana huwezi kuwa mheshimiwa na mpumbavu kwa wakati mmoja) mambo mawili ya msingi

1. Mpumbavu ni mtu wa aina gani.
2. Ni kauli au matendo gani ya mbunge au kiongozi yatamfanya astahili kuitwa mpumbavu?

  • Mbunge Mpumbavu ni yeyote yule anayetaka kuthibitisha uwongo uwe ukweli.
  • Anayetengua kanuni za bunge kwa manufaa yake au ngenge lake
  • Anayefikiria tumbo lake tu na si kwa manufaa ya taifa au wananchi waliomchangua

 
Kweli uongozi wa Bunge ndio umelifikisha Bunge hapo lilipo leo.Dharau ya wazi inayoonyeshwa na spika na naibu wake hasa maneno kama "mkuki kwa nguruwe" kwa wabunge wa vyama vya upinzani ndizo zinazosababisha uwepo wa maneno ya kejeli ndani ya bunge.Nimeeangalia kwa umakini namna anavyoendesha Bunge kwa sasa naona dhahiri nia yao ni kutaka ile azma yao ya kuzuia kurushwa vipindi vya Bunge hewani itimie.Sasa kama leo kawakemea Wabunge huku akilalama wakati yeye ndio anatakiwa asimamie sheria na kanuni za Bunge.Anamlalamikia nani badala ya kusimamia sheria?Tuna safari ndefu katika Bunge linaloendeshwa kwa ushabiki wa chama.
 
Hadi sasa nimepata yafuatayo ya msingi, kwamba mtu atastahili kuitwa mpumbavu ikiwa;

1. Yeye hajui kitu, ni mbulula, mjinga, na hana hekima wala busara, hafikiri, hajitambui
2. Hatumii muda wake kufanya yale anayotarajiwa kufanya kwa wakati huo, kutofanya mambo ambayo ametumwa na yasiyo na kutetea mambo yasiyo na maslahi ya wananchi waliomtuma (ndani na nje ya jimbo lake), na kwamba yeye hafanyi mambo yanayowaondoa Watanzania kutoka hapa pabaya tulipo.
3. Anayetaka kuthibitisha uwongo kuwa ukweli
4. Anayetengua kanuni za Bunge kwa manufaa yake binafsi au kikundi chake
5. Anaeweka mbele maslahi yake binafsi badala ya watu waliomchagua au taifa kwa ujumla
6. Hapendezwi na maneno mazuri yanayotolewa na wengine

Ninajua kuna mengi yatazidi kuja.
 
Fyatu unamawazo mufilii sana..kumbe ndo lengo lako..tatizo ni spika na naibu wake ukada wa chama chake sio kuonyeshwa katika luninga.....ukiona nyumba ina watoto wajing ujue kiongozi wa familia ndio tatizo,apply hiyo fomula hata kwwa nchi utagundua.
 
Mtazunguka koote, mtajadiliana na kushauriana mpaka mpate vipanda uso, lakini jibu lake ni RAHISI sana, Viongozi ni kioo cha JAMII wanayotoka, kwa maana ukitaka kujua jamii fulani ikoje angalia viongozi wake, hivyo kwa kifupi wote tuko hivyo, na tungefanya hivyo hivyo kama tungepata hiyo nafasi ya kuongea na kusikilizwa, na kama hilo linakuchangaya usiende mbali angalia tu watu waliokuzunguka kuanzia Familia yako mpaka Marafiki zako, Je wako tofauti?

Angalia Wafanyakazi wenzako, Je wanfanyaje kazi? nenda ofisi yoyote ile ya Umma TZ au hata Dukani tu mitaani kwetu, wahusika wakoje? ukichunguza hapo utapata majibu ya kwa nini viongozi wetu wako jinsi walivyo, ni sisi!
 
Kweli uongozi wa Bunge ndio umelifikisha Bunge hapo lilipo leo.


Mkuu Mnduoeye, nakubaliana na wewe kwamba uongozi makini wa taasisi yeyote ile duniani (organization) una mchango mkubwa sana kufanya taasisi hiyo iheshimike au kutoheshimika. Hili ni kweli kwa taasisi ndogo sana kama familia hadi taasisi kubwa kama nchi. Angalia hata mtaani kwako utakuta kama baba ni mlevi asiyejiheshimu familia yake mara nyingi haipewi uzito katika jamii. Pia angalia kwamba Tanzania huko nyuma iliheshimika sana kutokana na uongozi makini wa Nyerere.

Kwa hiyo aina ya uongozi wa Bunge ina sehemu kubwa kulifanya Bunge liheshimike au la. Na hata tujiulize, je tangu uongozi wa Bunge wa Sitta hadi Makinda, ni nini kimebadilika sana, ni wabunge au uongozi? Basi ikiwa sehemu kubwa ya wabunge tulio nao ni wale wa wakati wa Sitta, kwa nini basi, Bunge la enzi ya Sitta ni tofauti sana na Bunge la enzi ya Makinda? Haya ni maswali ya msingi ya kujiuliza.
 
Ya kweli kabisa..
Kama mbunge anasema haongei na mbwa bali mwenye mbwa..tafsiri ni kwamba kawatukana wote..kuwa mote humo ndani ya Bunge ni mbwa , akiwemo yeye..na Spika na naibu wake ndo mwenye mbwa..
Nilitegemea spika angekemea lakini alikaa kimya..
Bunge limekuwa aibu tupu...
kama wabunge wangekuwa wana ubavu wangepiga kura ya kutokuwa na imani na spika na naibu wake ili wachague viongozi wengine..nadhani kanuni hiyo itakuwepo
kwa mtindo huu wa sasa kila bajeti itapita tu kwani wanajadili matusi..na si hoja..
mzeeT
 
Ndugu kumbuka1. ukiona familia inayumba ujue tatizo ni kiongozi wa familia2. Ukiona nchi inayumba ujue tatizo ni kiongozi wa nchi3. Ukiona Wizara inayumba ujue tatizo ni waziri husika wa wizara hiyo4. Ukiona BUNGE linayumba ujue tatizo ni SPIKA wa Bunge**Kumbuka wakati wa Samwel Sitta hakukuwa na upuuzi huu tunaouona sasa haya yote ni matunda ya CCM kwa kumweka Spika asye na uwezo ili mambo yao yaende**
Hizo ni Rationalization zisizo na msingi. Kwa hiyo weakness za Makinda ndio zinamwambia Nkamia na Sugu watukane wenzao? Kwa kifupi haya mabunge yetu mengi hayajiheshimu. Hakuna cha CDM wala CCM.Kwani hawawezi toa hoja bila matusi??
 
Wewe zile ndoto zako ULIZOKUWA ukiota kwenda BUNGENI ndo zilishaota mbawa HATA kwenda BUNGENI KUPIGA DEKI ndo basi tena. Mbozi nawakusubiri ukawarudishie zile pesa walizokuwa wakikuchangia.



Na anatembea na laana ya wanambozi. Si bure
 
Ndugu yangu uliyoyasema ni kweli!kila kitu kiko Wazi hata wabunge wachache ambao ni makini ndani ya ccm wanajua hili! Ila ni vigumu kwa Hayo uliyopendekeza kutokea. Kilichobaki tushuhudie anguko la chama tawala tu.
kwani unadhani mwasisi wa bunge lisiwe live covered alikuwa anamaanisha nini. This is what the meant!



QUOTE=Synthesizer;6139617]Wala haihitaji uwe mwenye akili za ajabu kujua kwamba ukosefu wa heshima kati ya wabunge na wabunge, na wabunge na uongozi wa bunge umetokana na jinsi Makinda na Ndugai wanavyoliendesha bunge. Mambo yaliyolifikisha Bunge letu katika hadhi iliyopo ni kama yafuatavyo;

1. Utaratibu wa hila na ubinafsi uliotumika kumpata Spika wa sasa na kumwondoa Spika aliyekuwapo kabla yake
2. Kuruhusu wabunge wa chama tawala kukejeli na kuonyesha dharau kwa kila kauli au hoja inayotolewa na wabunge wa vyama vya upinzani
3. Wabunge wa chama tawala kutoelewa wajibu na kazi ya chama cha upinzani bungeni
4. Matumizi ya kanuni na taratibu za bunge katika namna ya kuwanyima uhuru wa uwakilishi wao wa kibunge wabunge wa vyama vya upinzani
5. Kuruhusu kanuni na taratibu za Bunge zivunjwe na wabunge wa chama tawala bila uongozi wa bunge kukemea au kuchukua hatua yeyote
6. Tabia ya wabunge wa chama tawala kuunga mkono au kushabikia kila kauli na hoja inayotolewa na wabunge wenzao wa chama tawala, hata kama kauli au hoja hiyo haina maslahi kwa taifa na wananchi
7. Kutumia nafasi ya uongozi wa Bunge kwa maslahi ya chama tawala na Raisi badala ya taifa na wananchi kwa ujumla.

Kauli na vitendo visivyo vya kawaida tunavyovishuhudia bungeni ni matokeo tu ya mambo hayo saba yaliyoorodheshwa hapo juu. Ikiwa Makinda na Ndugai wana nia ya kweli ya kurejesha heshima ya Bunge machoni pa wananchi wanapaswa kushughulikia mambo hayo, vipengele 2-7. Hii itasaidia kujenga heshima kati ya wabunge wenyewe, wananchi kuwaheshimu wabunge na Bunge.[/QUOTE]
 
Ni udhalilishaji wa hali ya juu wa Taasisi au mhimili unaoitwa Bunge na pengine ndiyo sababu ya kila mjinga nchi hii sasa hivi kutangaza nia yake ya kugombea ubunge ifikapo 2015.
Inasikitisha kuona baadhi ya wahuni wanaojiita Waheshimiwa wakifanya juhudi kubwa kulidhalilisha na kulirahisisha Bunge mpaka limeanza kuonekana kama kijiwe cha majuha!
Mungu ibariki Tanzania.
 
Makinda sio Spika wa Bunge ni Spika wa wabunge wa CCM maana hata watukane vipi hana ubavu wa kuwakemea ndo maana tunaamini wapinzani ndio wawakilishi halali wa watanzania na sio wabunge washenzi wale wa Ccm...Hawajiheshimu,hawaaheshimu wengine,hawaheshimiki wamejaa mitusi tu na spika ndo alishakufa zamani yeye anasubiri chadema wanapoongea ndo anafufuka na kijitabu chake cha kanuni uchwara zisizo tekelezeka kwa wahuni wa Ccm...Wapinzani tukaneni kama wao watukana haki haiombwi hupiganiwa mpaka ipatikane.
 
Hawa ndio wabunge wenye akili na busara kuliko wabunge wote ndani ya CCM. Mwigulu, Lusinde, Kigwangala, Wasira, Nkamia, Makinda, Ndugai, Lukuvi na Mulugo. Hayo ndiyo majembe ya CCM!
 
Back
Top Bottom