Nikifuatilia mijadala bungeni, nimeona mara nyingi kauli zikitolewa toka vyama vyote, chama tawala na vyama vya upinzani, kwamba tuna wabunge wapumbavu. Baadhi ya viongozi wamekuwa wakichachamaa na kusema kuwaita wabunge au viongozi wa serikali wapumbavu ni kwenda mbali mno.
Najua kwamba Biblia inatumia neno mpumbavu, na ninaamini Biblia ni kitabu kitakatifu, si kitabu cha matusi. Kwa hiyo basi, kama tuna wabunge wapumbavu yawapasa wabunge walikubali hilo na kurekebisha upumbavu wao badala ya kulalamika kwamba wanatukanwa.
Labda kwanza wana Jamii Forum, kama kioo cha jamii, tunapaswa kuwaeleza hawa Wabunge wetu (nachelea kuwaita waheshimiwa, maana huwezi kuwa mheshimiwa na mpumbavu kwa wakati mmoja) mambo mawili ya msingi
1. Mpumbavu ni mtu wa aina gani.
2. Ni kauli au matendo gani ya mbunge au kiongozi yatamfanya astahili kuitwa mpumbavu?
***********
Hadi sasa nimepata yafuatayo ya msingi, kwamba mtu atastahili kuitwa mpumbavu ikiwa;
1. Yeye hajui kitu, ni mbulula, mjinga, na hana hekima wala busara, hafikiri, hajitambui
2. Hatumii muda wake kufanya yale anayotarajiwa kufanya kwa wakati huo, kutofanya mambo ambayo ametumwa na yasiyo na kutetea mambo yasiyo na maslahi ya wananchi waliomtuma (ndani na nje ya jimbo lake), na kwamba yeye hafanyi mambo yanayowaondoa Watanzania kutoka hapa pabaya tulipo.
3. Anayetaka kuthibitisha uwongo kuwa ukweli
4. Anayetengua kanuni za Bunge kwa manufaa yake binafsi au kikundi chake
5. Anaeweka mbele maslahi yake binafsi badala ya watu waliomchagua au taifa kwa ujumla
6. Hapendezwi na maneno mazuri yanayotolewa na wengine
Najua kuna mengi zaidi yatakuja