Bungeni tumepeleka vichaa, wendawazimu au mateja?

Bungeni tumepeleka vichaa, wendawazimu au mateja?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,631
Reaction score
164,745
Kila mtu alieangalia bunge siku ya leo bila shaka atakuwa akijiuliza maswali kuhusu mwenendo wa wabunge wetu hawa na kama kweli wanafahamu nini wajibu wao kwa wapiga kura wao.

Mimi najiuliza hawa wabunge wanatofauti gani na mateja au wapiga debe wa stand kwa kauli zao hizi za matusi ndani ya bunge?Hivi si bora hata kichaa kwasababu ni mgaonjwa wa akili ila hawa wabunge nao ni wagonjwa wa akii?Hivi wanamdhalilisha nani kama sio wao wenyewe,ndugu,jamaa,marafiki na familia zao?Hivi hawa wabunge wanastahili kuitwa waheshimiwa na wao kujiita waheshimiwa?Hawa wabunge kweli wanastahili kulipwa mamilioni ya shilingi kila mwisho wa mwezi kama mshahara na marupurupu kwa upuuzi huu?Hivi bunge limegeuka band ya kuimba taarabu(mipasho)!

Mimi nisema kama hali hii itaendelea mpaka 2015 basi tusishangea kuona idadi ya wapiga kura ikishuka kwa kiasi kikubwa katika uchaguzi mkuu ujao kwani ni nani atakuwa tayari kuendelea kupanga foleni kuchagua "mateja" na kuwapa ticket ya kwenda bungeni!

Leo hii nimeamini ile kauli ya naibu spika alieitoa katika mahojiana na mtangazaji mmoja kwenye TV station moja hapa nchini kuwa kuna wabunge wanavuta bangi!

Bunge hili ni janga la kitaifa pengine kuliko hata ukimwi!

Mwisho namshauri mh.Spika kesho, mara tu baada ya salaa ya kuliombea bunge, atoe kauli ya kuwaomba radhi watanzania wote kwa mwenendo mbovu wa bunge analoliongoza.
 
Na bado, bongo fleva na movies takriban wote wametangaza kugombea ubunge.
 
Na sasa ndio naona sababu za kufanya bunge lisionekane live, inabidi liwe linahaririwa kwanza...

Imefika mahali ukiona inafika zamu ya wabunge fulani ni kama unaangalia muvi ya X ukiwa na familia sebuleni....mapigo ya moyo yanaongezeka. kama hawa tunaowaita viongozi wanaenda kufanya UHUNI bungeni tutegemee nini kutoka kwenye jamii ya kawaida mitaani kwetu ? Mtu anayemsema mwenzake kajamba kwenye hadhara ndio huyo huyo kesho akwambie usiibe...usizini...usiseme uongo. Nalazimika kuamini hata kati ya wachangiaji wanaotumia lugha za matusi humu baadhi yao ni hao tunaowaita waheshimiwa.

Kama mtu mzima anadiriki kutamka matusi hadharani..mbele ya TV seuse humu alipoficha utambulisho ? Ushauri wangu kwa SPIKA na naibu wake, waje na sheria (iwapo hakuna) kwamba mbunge anayetamka tusi basi mchango wake uishie pale pale akae chini..Tupo wengi tunaoumia na mwenendo huu usio wa kiungwana, mtu unaona aibu kwa niaba ya anayeongea. TUNAHITAJI VIONGOZI WANAOJIHESHIMU.

Wapo baadhi ya wabunge wanaposimama unapata amani ya kumsikiliza anavyojenga hoja na kujibu shutuma(kama zipo) bila lugha za kihuni wala jazba zisizo na msingi, Pongezi kwao...
 
Na wagonjwa waliotahriwa na visukari na presha na utapiamlo wote wako mle, na full stress, nakwambia mwaka huu watakufa wengi sana hadi wamejiwekea bajeti ya mazishi ya Billion moja???!!!!!!!!!
 
Sina hata haja ya kuiangalia!Bora hata mpiga debe anayepiga debe stand kuliko hawa wapuuzi wanaoitwa waheshimiwa wa mipasho na matusi!Hv iweje mhimili wa taifa unaotegemewa na wananchi kuwaletea maendeleo wanaenda jadili mambo ya ajabu yasiyo na tija kwa taifa?Madam spika unatupeleka wapi?Kiti chako kinapwa kabisa kuliko unavyodhani na kujifikiria!Hakika watanzania tumepeleka walevi mjengoni!Ni bora nikajiuzie mayai stand kuliko kukaa eti naangalia bunge!!
 
wakati mwingine unasema heri na Mbunge wangu angekufa tu nikajua sina Mbunge au wakati mwingine unasema hero Mbunge wangu ambaye kutwa nzima ni kusinzia tu but ukiangalia kwa undani hakuna afadhali heri kuwa na hata na Mkusanyiko wa wavuta bangi kuliko kuwa na bunge sililo na akili kama hili hasa kwa Wabunge wa CCM
 
Kwa kweli watanzania wenzangu kwa nilichokishuhudia leo bungeni ni huzuni kubwa kwetu wananchi na nchi yetu.kwa hali ya leo ilivyokuwa bungeni ni dhahiri hatuna bunge kwa sasa.Na hii yaweza kuwa ni laana ya mh. S.SITTA.MIA!
 
Mama Makinda was right, bunge limekua kama soko la Kariakoo, inakera kwa kweli.
 
Hayo hayana budi kutokea ili bunge liwe na heshima. bila kuvuja damu, amani haiwezi kupatikana. Hivi mlipenda bunge lile la kuunga mkono hoja kwa asilimia 100? Kila anayependa na kuelewa mapinduzi ya kweli, lazima akubali kupitia hatua hii, ili bunge lijalo liwe na heshima. tegemea bunge bora 2015, kwa kuwa kila mbunge asiye na tija, wapiga kura tunamwona, na 2015 ni hukumu yake.
 
Kila mtu alieangalia bunge siku ya leo bila shaka atakuwa akijiuliza maswali kuhusu mwenendo wa wabunge wetu hawa na kama kweli wanafahamu nini wajibu wao kwa wapiga kura wao.

Mimi najiuliza hawa wabunge wanatofauti gani na mateja au wapiga debe wa stand kwa kauli zao hizi za matusi ndani ya bunge?Hivi si bora hata kichaa kwasababu ni mgaonjwa wa akili ila hawa wabunge nao ni wagonjwa wa akii?Hivi wanamdhalilisha nani kama sio wao wenyewe,ndugu,jamaa,marafiki na familia zao?Hivi hawa wabunge wanastahili kuitwa waheshimiwa na wao kujiita waheshimiwa?Hawa wabunge kweli wanastahili kulipwa mamilioni ya shilingi kila mwisho wa mwezi kama mshahara na marupurupu kwa upuuzi huu?Hivi bunge limegeuka band ya kuimba taarabu(mipasho)!

Mimi nisema kama hali hii itaendelea mpaka 2015 basi tusishangea kuona idadi ya wapiga kura ikishuka kwa kiasi kikubwa katika uchaguzi mkuu ujao kwani ni nani atakuwa tayari kuendelea kupanga foleni kuchagua "mateja" na kuwapa ticket ya kwenda bungeni!

Bunge hili ni janga la kitaifa pengine kuliko hata ukimwi!

Mwisho namshauri mh.Spika kesho, mara tu baada ya salaa ya kuliombea bunge, atoe kauli ya kuwaomba radhi watanzania wote kwa mwenendo mbovu wa bunge analoliongoza.

Wananchi anaopiga kura sidhani kama watafanya makosa kurudisha vichaa wa cdm bungeni.
coz hawana Tija, sidhani 2015 idadi yao itazidi watano.
 
Ni vema wakubwa wakajishahihisha na utovu wa nidhamu wanaoufanya bungeni.

Na kama tatizo ni meza ya spika ni bora ukafanyika mchakato wa haraka wakajiuzuru kwa kuwa

sio lazima waongoze wao ilihali wanashindwa kusimamia nidhamu ya bunge na mbaya zaidi

ni pale wanapopelekwa na hisia ya chama tawala na hofu juu ya upande wa upinzani.

Kiukweli heshima na hadhi ya bunge letu tukufu inazidi kuporomoka siku hadi siku.

Binafsi ningewaomba wakubwa/wahusika kuishauri meza ya spika ikiwezekana wakakaa pembeni kidogo kwa muda huu

uliobaki ili kunusuru hadhi na heshima ya bunge kwani kufanya hivyo sio dhambi bali ni heshima kubwa kwao na taifa.
 
Wananchi anaopiga kura sidhani kama watafanya makosa kurudisha vichaa wa cdm bungeni.
coz hawana Tija, sidhani 2015 idadi yao itazidi watano.

Hahaaa....kama wamekuwa wakiwachagua vichaa tangu 1961 kitawashinda nini kuendelea kuwachagua wendawazimu? Think big madam!

 
Chuki, kweli ipo kama jina lako. Hili bunge laiti ungeambiwa uwe unaangali wewe tu then una repot kwa wana jf ungedanganya umma. Sasa wale waliotoa lugha za matusi leo walikuwa cdm tu? Be honesty Chuki!! Kwa taarifa yako kama umeambiwa basi mi nimeona.

Mtoa maada ndg Salary Slip, hajaegemea upande wwte na yupo sawa kbs kwani kama ni aibu kwa sisi raia wa kawaida ambao tunasikiliza na wale wabunge sio ndugu zetu, je kwa familia zao, rafiki zao, na waliowasaidia kuingia bungen wengine kiuchumi, kura n.k itakuwa vp? Mch. Msigwa, sugu, mwigulu nchemba, lusinde, juma nkamia ila yy nadhan kaomba msamaha palepale kwan kakiri kuropoka lile neno, wenje, kuna mbunge wa zanzibar CUF sikumshika jina lake alisema msigwa mchungaji wa nguruwe, jah people wa makambako, tundu lisu n.k ni baadhi ya wabunge ambao kwa kweli wanatakiwa kujirekebisha na kama hawatabadilika nitawashangaa wananchi wanaoongozwa na hawa wabunge watawarudisha tena bungeni 2015. Wanatia aibu na hii ni list ambayo wengi wao wamechangia leo 15.4 tu. Very shame....
 
Mwigulu ana tatizo gani? au wewe ndo mwenye matatizo . cdm walianza sasa ccm wakijibu inakuwa shida sasa twendeni tuu na mtindo huu tuone ni nani atapata Hasara kati ya ccm au cdm.
 
Nampa big up mbunge aliyemuumbua mbunge aliyejamba Acheni kabisa harufu mbaya inatesa
 
Wananchi anaopiga kura sidhani kama watafanya makosa kurudisha vichaa wa cdm bungeni.
coz hawana Tija, sidhani 2015 idadi yao itazidi watano.
Ni heri hao kuliko misukule ya ccm.. Watarudiiiiiiii....
 
Mwigulu ana tatizo gani? au wewe ndo mwenye matatizo . cdm walianza sasa ccm wakijibu inakuwa shida sasa twendeni tuu na mtindo huu tuone ni nani atapata Hasara kati ya ccm au cdm.

Kweli we rijamaa hamnazo, unachekelea upumbavu wa wabunge hawa. Wanakaa siku nzima wanazozana at the end of day wanakula posho kama ilivo na ni kodi za wananchi
 
Wengi wamo umu lakin huwakuti wakija kujibu mambo ya msingi kama aya
 
Mwigulu ana tatizo gani? au wewe ndo mwenye matatizo . cdm walianza sasa ccm wakijibu inakuwa shida sasa twendeni tuu na mtindo huu tuone ni nani atapata Hasara kati ya ccm au cdm.

Hasara ni kwetu wote na wala si kwa hivyo vyamaa.

Na utambue malumbano haya ya wabunge ndio furaha ya serikali kwani badala ya kuisimamia na kuihoji serikali wao wanaishi kutukanana na mwisho wa siku wanapitisha bajeti kibabe na kwa kudhani wanakomoana ila ukweli wanaemkomoa ni mimi na wewe na wala si vyama vyao.

Hebu hapo ulipo jiulize wakati waziri mkuu atakapokuiwa anahitimisha bajeti yake atajibu matusi waliokuwa wanatukanana?Kama sehemu kubwa ya hoja za wabunge ilikuwa ni matusi, waziri mkuu atakuwa na nini cha kujibu zaidi ya kutimiza wajibu wake kwa kuhitimisha bajeti yake?
 
Back
Top Bottom