Bungeni: Magufuli azichambua barabara Tanzania kama karanga

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2005-2010 kitakwimu ni kuwa serikali iliweza kukamilisha miradi 15 kwa kiwango cha lami na hivyo kujenga barabara zenye urefu wa Kilomita 1,398.6. Kasi hii Haitii matumaini hata kidogo kwani kwa mujibu wa ilani ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2010-2015 imepanga kumalizia ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa kilomita 1,140 (barabara 9 )ambazo ni miradi ambayo ilikuwa haikukamilika kwenye kipindi cha 2005/2010 na kuanza ujenzi mpya wa kilomita 5,282 kwa kipindi cha 2010-2015 (takwimu hizi ni kwa mujibu wa Ilani ya CCM 2010-2015).takwimu hizi ni sawa na kusema kuwa serikali itaweza kujenga kilomita 6,422 za lami katika kipindi cha miaka mitano.

Wakati huo huo Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano unaonyesha kuwa ni barabara zenye urefu wa kilomita 5,552 tuu ndio zitaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami kwa kipindi cha miaka mitano ijayo (2011/2012-2015/2016).

Mheshimiwa Spika, takwimu hizi hazijahusisha mpango wa serikali wa kujenga barabara kwa viwango vya Changarawe na zile za vijijini kwa kipindi cha miaka 5 ijayo.

Kambi ya Upinzani, tunasubiri kuona muujiza huu wa serikali kujenga barabara zenye urefu mkubwa kuliko zilizojengwa tangu wakati wa uhuru yaani kwa kipindi cha miaka 50 ndani ya miaka 5 . Na haswa ikizingatiwa kuwa kwa kipindi cha miaka 5 iliyopita (2005-2010) serikali hiyo hiyo iliweza kujenga kilomita 1,398.6 tuu za kiwango cha lami kwa kipindi hicho (Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010-2015 -Mafanikio katika Sekta ya Miundombinu" uk.6 ) .

Tunasema hivyo kwa sababu tunaona kuwa wananchi wanapewa matumaini makubwa ya miradi mingi ya barabara wakati fedha kwa ajili ya barabara hizo hazionekani kutengwa kwa ajili ya kuweza kuzijenga.

Pili, kambi ya Upinzani, tunataka kupata majibu ni takwimu zipi zipo sahihi, je? Ni za Ilani ya uchaguzi ya CCM ama ni mpango wa Taifa wa Maendeleo? kuhusiana na jumla ya kilomita za barabara ambazo zitajengwa kwa miaka mitano ijayo.

Katika miaka mitano ya 2005 hadi 2010 hakuna km 1398.6 za barabara za lami zilizojengwa Tanzania huu ni uongo mkubwa sana wabunge mmedanganywa lete list ya hizo barabara zilizojengwa hapa JF
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Magufuli in no longer Magufuli yule wa enzi za Mkapa nadhani system imemuinduce na mekuwa anaexist katka form nyingine. Utaongeleaje ujenzi wa barabara za juu wakati hata za chini hujamaliza? pia barabara za juu kwa mji uliokaa kienyeji kama dar watasababisha maafa kila siku. maoni yangu:-
1. kwanza waupange mji vizuri
2. Wajenge barabara katika kiwango cha lami zote Dar
3. Umeme wapitishe undergroud
4. Ndio sasa waanze kujenga barabara za juu

Jibu maswali yafuatayo:-
a. Chama kushika hatamu maana yake ni nini?
b. Chama cha mapumbuzi kina jumuiya ngapi? zitaje.
c. CCM ilizaliwa lini?
d. wajumbe wa kamati kuu huchaguliwa na ..............
 
Hili ni jambo kubwa sana na hakutaka kulizungumzia kabisa na ameamua kulikalia kimya .

Miradi maalum ya ujenzi wa Barabara (kasma 4168).Mheshimiwa Spika, kitabu cha Miradi ya Maendeleo part-A volume iv katika fungu 98, kasma 4168 utaona kuwa kuna mradi unaitwa “Miradi ya ujenzi wa barabara maalum” (special road construction projects) na fungu hili limetengewa kiasi kikubwa kuliko mradi mwingine wowote wa ujenzi wa barabara katika mwaka huu wa fedha kwani zipo jumla ya shilingi 348,075,000,000 na hizi zote ni fedha za ndani, kwa hakika hizi ni fedha nyingi sana na haswa ikizingatiwa kuwa kitabu hicho kimeonyesha miradi yote ya ujenzi wa barabara ambayo itatekelezwa katika mwaka huu wa fedha , ila hii miradi maalum haijaonyeshwa ni miradi ya barabara gani na zitajengwa wapi.

Mheshimiwa Spika, kasma hii kwa mwaka wa fedha 2009/2010 na 2010/2011 haikuwa imetengewa kiasi chochote cha fedha na ndio maana imetustua kuona mwaka huu fedha nyingi kiasi hicho kinatengwa kwa miradi isiyojulikana kuwa itajengwa wapi.

Mheshimiwa Spika, hata ukiangalia maelezo yaliyotolewa kwenye Kamati ya Bunge ya Miundombinu juu ya mpango na bajeti ya mwaka 2011/12 kasma 4168 haipo kwenye randama na hakuna maelezo yoyote ambayo yametolewa kuhusiana na fedha hizo ambazo zimetengwa.

Hiyo ni mianya ya rushwa. Utatengaje fedha, tena nyingi kiasi hicho, kwenye project bila kutoa analysis juu ya matumizi ya hizo fedha? Shilingi 340,075,000,000 kwa matumizi hewa. Kwa stahili hii, inabidi bajeti isipitishwe mpaka tupate ufafanuzi wa matumizi ya hizo fedha. Seriously.
 
Shida yake ni pale anapochanganya siasa na miundo mbinu, hilo ndilo litakalomshinda!

Kabisa Mkuu. Ana base sana kwenye ilani ya CCM kuboresha miundombinu. Tatizo kubwa la ilani ya CCM hatekelezeki. Realistically, ilani ya CCM ya kutengeneza kilomita za barabara walizotaja ndani ya miaka mitano, is not achievable. Chukulia mfano Serengeti Highway. Hii ilikuwepo kwenye ilani ya CCM ya mwaka 2005, tuliambiwa kuwa barabara ingekamilika kabla ya uchaguzi uliopita. Ilani ya uchaguzi wa 2010 tumeambiwa hivyo hivyo.

 
Last edited by a moderator:
<font size="3"><br />
Ahaa aaa ulikuwa umelala wapi? unadhani anaweza kutetea chama gani Mkuu? umenichekesha sana kama ulikuwa humjui Magufuri</font>
<br />
<br />
ni ajabu na kweli kwamba bado kuna watu wameendelea kuwekeza matumaini yao kwa wanamagamba regardless miaka 50 ya kutujaza umasaikini.
 
heee wewe magufuli, sisi watanzania wa leo sio wajinga tena. cccm imetoa wapi hela za kujenga barabara??? Kodi zetu watanzania ndo zinajenga barabara na ni sisi watanzania tumewaajiri wewe magufuli, mwakyembe na tanroads mjenge barabara tupite muruaaa.

nyie cccm endeleeni kujivua gamba mpaka september

na msirudie tena kudanganya kuwa ccm inajenga barabara
 
Kabisa Mkuu. Ana base sana kwenye ilani ya CCM kuboresha miundombinu. Tatizo kubwa la ilani ya CCM hatekelezeki. Realistically, ilani ya CCM ya kutengeneza kilomita za barabara walizotaja ndani ya miaka mitano, is not achievable. Chukulia mfano Serengeti Highway. Hii ilikuwepo kwenye ilani ya CCM ya mwaka 2005, tuliambiwa kuwa barabara ingekamilika kabla ya uchaguzi uliopita. Ilani ya uchaguzi wa 2010 tumeambiwa hivyo hivyo.



Ilani inaandaliwa na nani?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Ndege wafananao huruka pamoja, kwa kuwa yuko CCm magufuli hana tofauti na Ngereja, Lukuvi, Lusinde, Ndugai, Sitta, Chenge, ROstam na wengine wote
 

Ilani inaandaliwa na nani?

They are written by people who know how to spin things. After each election, check the manifestos against the implementation of government policies. With time and experience, you will dawn the truth. It is worthless to know who prepare the manifestos whether they are for CCM, Chadema, or CUF, because their aim is to get the politicians elected. Full stop.

To that end, they will put into the Manifesto a lot of stuff they believe and care about. And more stuff about which they don't give a damn, but which they know is important to various segments of the electorate. The purpose of this is to be able to say, whenever a voter asks awkward questions: "Oh, yes, that's in our manifesto."

When the election is over the Election Manifesto has served its purpose, and may be burned with the rest of the election junk. Once the new government comes into office, the Manifesto is kaput and what matters is the Programme for Government. "If the voters had given us more seats, we would have been able to achieve more." This is their excuse for breaking the promises in the manifesto. It's not their fault, you see, the voters are to blame.
 
Ntaweka hotuba yote ili muweze kuona jinsi ambavyo hakujibu maswala ya msingi na ambayo yanapaswa kujibiwa .
Unajua Magufuli anatumia kutokujua kwa wananchi kuipa ccm umaarufu sasa kwa bahati mbaya anakutana na maswali ambayo hawezi kujibu pamoja na umahiri wake.

Akitaka aheshimiwe na wananchi hana budi kujibu hotuba ya kambi rasmi ya upinzani bungeni
 
Huyu Bwana ndio twamkubali ni kichwa ila jinamizi lililoko kwa CCM bwana sijui huwa haliangaliii nani awe Rais huyu bwana ni tishio CCM na hana Cheo huko CC zaidi ya ujumbe na mjumbe uko CCM ni kama tu kazi bure, ila ukiangalia vilaza wengi huko CCM na NEC duuuuh usipime ni walopokaji kama Tambwe hiza
 
Ni MCHAPAKAZI HODARI.... Mzalendo wa Ukweli.... ana DATA nyeti zinazohusu kila wizara... Lakini cha muhim zaidi sio MNAFIKI.....
 
  • Thanks
Reactions: FJM
kwa lipi kutaja idadi ya barabara bila kujibu hoja za msingi?
....Umenena vyema...anajua ku-memorize ndo silaha yake kwa wenye kumbukumbu haba.
Hana prioritization ya barabara ipi ianze ipi ifuate! Weka number chini kwanini Chato ilipata prioritization kabla ya Mtera etc!
 
Mheshimiwa Spika, Serikali iliandaa mpango wa kujenga barabara wa kipindi cha miaka 10 (2007/08- 2016/17 Transport Sector Investment Program (TSIP). Na kwa awamu ya kwanza mpango huu ulikadiriwa kutumia US$6.2 billion (takribani trilioni 9 za kitanzania) (2007/08 mpaka 2011/12) .Ni dhahiri kuwa mpango huu kwa awamu ya kwanza ndio unafikia ukomo wake kwenye bajeti hii.

Kambi ya Upinzani, tunataka kupata majibu kama lengo lililokusudiwa lilifikiwa ama kulikuwa na ukomo wa bajeti katika kutekeleza mpango huu ili hatimaye sasa tuweze kuingia kwenye awamu ya pili.

Pia tunataka kupata majibu ni kilomita ngapi za lami zilijengwa katika awamu hii ya kwanza na haswa ikizingatiwa kuwa Mpango wa Maendeleo wa miaka 5 umetenga kiasi cha shilingi trilioni 6,793 kwa ajili ya kujenga kilomita 5,204.7 za lami hapa nchini (Mpango wa Maendeleo wa miaka 5 uk.55) ambazo ni ndogo kuliko zilizotumika kwenye awamu ya mpango huu ambao unafikia ukomo wake mwaka huu wa fedha.

Nadhani mtu anayetakiwa kutoa majibu sahihi ya haya maswali ni Shukuru Kawambwa na Chenge! Nijikite kwa Kawambwa: Huyu Mheshimiwa sijui ana ngekewa gani maana anapata wizara nyeti sana lakini uwezo wake ni wa chini mno, hafai hata kuwa balozi wa nyumba kumi. Hafai! Wakati huo akiwa wizara wa miundo mbinu ujenzi wa barabara uligeuzwa kama shamba la bibi na ndio kipindi hiki Ufalme wa Mrema wa Tanroads ulipoimarika. Wafadhili na hasa wa GBS waliongelea sana kuhusu ushagalabala wa ujenzi wa barabara - na kwa taarifa bei ya kujenga km 1 ili-double! huku viwango vikishuka!

Najua Magufuli kama cabinet Minister hawezi kuanza blame game lakini amekuwa na kibarua kikubwa sana sio tu cha kishusha chini garama za ujenzi, bali pia kusuka Tanroads. Mrema ameondolewa and I can happily say Magufuli ni mwanaume maana huyu Mrema alikuwa tishio pengine ni kutokana na uswaiba wake au utii wake kwa Lowassa! Hata hivyo Magufuli ame-deal naye, sasa kazi iko kwenye kufumua mtandao wake (Mrema).

Jambo la muhimu hapa ni kwamba Magufuli kama binadamu ana mapungufu yake lakini within CCM amekuwa na uthubutu na ubunifu wa hali ya juu wa kutenda kazi ndani ya mazingiria ya siasa za 'kuviziana na visasi'. Nina kama Kikwete angemuacha kwenye wizara hii tangu 2005 leo hii Tanzania ingekuwa na barabara nyingi za lami. Nashawishika kusewa kuwa kama huyu Magufuli angepewa wizara ya Ngeleja tusingekuwa na mgao huu wa aibu!

Sasa turidi nyuma. Kwa nini Waziri Mkuu Pinda alipanda ndege kwenda kwenye jimbo la Magufuli na kutangaza mbele ya wapiga kura wake kuwa bomoabomoa imepigwa stop? Kama ilikuwa ni lazima ku-mpiga stop kwa nini asifanye hivyo hapa Dar au akamuita ofisini kwake na kumweleza hayo aliosema mbele ya kadamnasi?. Pinda 'alitumwa' kumshushia hadhi mbele ya wapiga kura wake? Na kama ndio, nani alimtuma Pinda na kwa sababu zipi? Siasa za kuviziana ndio zimeua CCM.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Sasa turidi nyuma. Kwa nini Waziri Mkuu Pinda alipanda ndege kwenda kwenye jimbo la Magufuli na kutangaza mbele ya wapiga kura wake kuwa bomoabomoa imepigwa stop? Kama ilikuwa ni lazima ku-mpiga stop kwa nini asifanye hivyo hapa Dar au akamuita ofisini kwake na kumweleza hayo aliosema mbele ya kadamnasi?. Pinda 'alitumwa' kumshushia hadhi mbele ya wapiga kura wake? Na kama ndio, nani alimtuma Pinda na kwa sababu zipi? Siasa za kuviziana ndio zimeua CCM.

Ndio hapo sasa. Unakumbua Mama Tibaijuka nae alianza kwa mbwembwe akastopishwa. Mara ya mwisho umemsikia lini? Kama hayupo tena vile.
 
Back
Top Bottom