hawa wabunge wa ccm wengi wao hawajui wasemalo. Wanawakashifu wapinzani kwa kukosoa serikali ya ccm kisha na wao wanarudi kukosoa mapungufu yaliyopo kwenye bajeti ya serikali ya ccm. Hawa nawafananisha na nyoka anayemeza mkia wake mwenyewe!
CCM wanajikaanga kwa mafuta yao. Jazba za Ndugai ndiyo furaha na neema ya CDM. Hakuna jipya aliloongea Mnyika ambalo mwana-CCM hajawahi kuongea, hili ni bunge la double standard. Wananchi wanajua na hukumu wanaitoa kwa kuongeza chuki dhidi ya CCM na wabunge wake.
Jana Komba kaita watu machizi kwa na kuwataka waanzie Mirembe kabla ya kwenda Bungeni wakamshangilia, Lowassa aliwahi kuiita serikali inashindwa kufanya maamuzi magumu bungeni-> dhaifu wakamshangilia. Kwenye hili la kumtoa nje Mnyika Ndugai atajutia uamuzi wake kwani unaipaisha CDM zaidi.
Nadhani baadhi ya wabunge huwa wanaongea kama vile wamekurupushwa na hawakujua kuwa wako kwenye orodha ya kuchangia. Mtu anaongea mtiririko huuoni. Mara vijembe mara kejeli. Tarime Kazi mnayo 2015.