Bungeni Live: Hoja juu ya Madawa ya Kulevya

Bungeni Live: Hoja juu ya Madawa ya Kulevya

Wakitajwa halafu

Mbona unauliza utadhani serikali ni kama klabu cha pombe? Ni tanzania pekee ambapo idara za ulinzi na usalama zimeacha majukumu yake na kufanya serikali itake ushahidi wa moja kwa moja toka kwa raia kwa mambo ambayo yanafanyika wazi wazi. A failed state.
 
Vile vile mh.Lukuvi ameeleza nia ya serikali kubadilisha sheria ili madawa ya kulevya yakishakamatwa na ushahidi kupatikana(kuwa kwenye kumbukumbu) basi madawa hayo yaharibiwe mara moja kuliko utaratibu wa sasa ambao madawa hayo huhifadhiwa mpaka kesi husika kuisha na ametoa mfano wa madawa kuwekwa kwa miaka hata kumi kusubiri kesi ikamilike.


MY TAKE:KAMA RAISI AMESHINDWA KUTAJA HAO VIGOGO HADHARANI, LUKUVI ATAWEZA VIPI?

Hapo kwenye RED kauli hii ya Lukuvi inaonyesha jinsi gani alivyo na upeo mdogo wa kutunza kumbukumbu mbona kila kukicha Bangi inateketezwa na kwa kauli yake hii tukimwambia atuonyeshe sehemu madawa (Cocain, Mandrax, Heroin) yalikohifadhiwa na tuonyeshwe takwimu za kiasi kilichokamatwa cha madawa na kilichopo kama yanalingana na tutamuuliza tena hayo ambayo hayapo yamepelekwa wapi?
 
Hapo kwenye RED kauli hii ya Lukuvi inaonyesha jinsi gani alivyo na upeo mdogo wa kutunza kumbukumbu mbona kila kukicha Bangi inateketezwa na kwa kauli yake hii tukimwambia atuonyeshe sehemu madawa (Cocain, Mandrax, Heroin) yalikohifadhiwa na tuonyeshwe takwimu za kiasi kilichokamatwa cha madawa na kilichopo kama yanalingana na tutamuuliza tena hayo ambayo hayapo yamepelekwa wapi?

Hawa kenge tu....eti tupo kwenye mchakato. Tumejipanga kama serikali...
 
Mkuu nayo kumbe anayo?kama kweli kazi ipo.sijui ataanzia wapinahisi itaishia anayo anayo tu.
 
Bunge limeanza leo mjini Dodoma na sasa ni kipindi cha maswali na majibu ambapo hoja inayoendelea kwa sasa ni wabunge kutaka wahusika wa biashara ya madwa ya kulevya watajwe.Waziri Lukuvi ameahidi kuwataja na ametaka mwenye ushahidi apeleke.Hata hivyo, wabunge wamemzomea na spika ameonya hiyo tabia ya kuzomea.

Baadhi ya wabunge waliotaka majina yatajwe ni mh.Mama Kilango wa CCM na mbunge wa karatu kupitia CHADEMA ambae amehoji inakuwaje hata Raisi amekiri kuwa na orodha ya wauza unga bila wahusika kutajwa na kuchukuliwa hatua.

Hata hivyo,waziri Lukuvi amesisitiza umuhimu wa kuwa na ushahidi kwani amesema kama ni kutajwa tu na wengine wamo humu bungeni na ameongeza hata gazeti la Jambo leo limewataja kwahiyo kitu muhimu ni ushahidi na sio kutaja tu.

Vile vile mh.Lukuvi ameeleza nia ya serikali kubadilisha sheria ili madawa ya kulevya yakishakamatwa na ushahidi kupatikana(kuwa kwenye kumbukumbu) basi madawa hayo yaharibiwe mara moja kuliko utaratibu wa sasa ambao madawa hayo huhifadhiwa mpaka kesi husika kuisha na ametoa mfano wa madawa kuwekwa kwa miaka hata kumi kusubiri kesi ikamilike.


MY TAKE:KAMA RAISI AMESHINDWA KUTAJA HAO VIGOGO HADHARANI, LUKUVI ATAWEZA VIPI?

Ushahidi ni muhimu, sawa' ila kazi ya kutafuta ushahidi ni ya nani? Au mwenye kazi imemshinda? Hao wanaokamatwa na unga polisi wameshindwa kuwahoji na kujua anaewatuma! Mbona mlolongo wote uko wazi, ukimpata mtumiaji, utampata muuzaji na utampata muingizaji, siwezi amini polisi hawawajui wanaoingiza unga' kama hawawajui ina maana hakuna usalama wa taifa kabisa' na labda ndo maana polisi wetu wanaambiwa ni wavuta bangi'
 
Hapo kwenye RED kauli hii ya Lukuvi inaonyesha jinsi gani alivyo na upeo mdogo wa kutunza kumbukumbu mbona kila kukicha Bangi inateketezwa na kwa kauli yake hii tukimwambia atuonyeshe sehemu madawa (Cocain, Mandrax, Heroin) yalikohifadhiwa na tuonyeshwe takwimu za kiasi kilichokamatwa cha madawa na kilichopo kama yanalingana na tutamuuliza tena hayo ambayo hayapo yamepelekwa wapi?[/QUOE]

Na wakikamata gongo utawakuta wako bwiii...sijui wanaipelekaga wapi!
 
Akiongelea suala la madawa ya kulevya leo bungeni kwa wale wanaotajwa kuhusika kwa kiasi kikubwa, mheshimiwa Lukuvi amesema kwamba ni aibu kwa serikali kumkamata na kumshitaki mtu mahakamani bila ushahidi wa kutosha. Aliendelea kufafanua kuwa yeyote mwenye majina na ushahidi wa wanaohusika na madawa ya kulevya apeleke wayafanyie kazi vinginevyo serikali haiwezi kuwakamata kila wanaotajwa maana hata bungeni wapo wengi. Vile vile alisema kwamba kazi ya serikali sio kutaja majina bali kuwashughulikia wahalifu waliothibitika kuhusika moja kwa moja.

Je, hii aibu ya serikali ni kwa wahusika wa madawa ya kulevya tu? Mbona kuna baadhi ya watu wamewahi kukamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma mbalimbali na serikali kubwagwa mahakamani kwa kutokuwa na ushahidi wa kutosha!
 
Ajibu tuhuma za majaji walioandikwa kwenye Jamhuri kujihusisha na kuvuruga ushahidi wa watu wa madawa ya kulevya asitake kuwafanya watu hawana akili. Wale waliopitisha twiga JKNIA walishakamatwa aua nao wanatafutiwa ushahidi! Watu wengine bana.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Akiongelea suala la madawa ya kulevya leo bungeni kwa wale wanaotajwa kuhusika kwa kiasi kikubwa, mheshimiwa Lukuvi amesema kwamba ni aibu kwa serikali kumkamata na kumshitaki mtu mahakamani bila ushahidi wa kutosha. Aliendelea kufafanua kuwa yeyote mwenye majina na ushahidi wa wanaohusika na madawa ya kulevya apeleke wayafanyie kazi vinginevyo serikali haiwezi kuwakamata kila wanaotajwa maana hata bungeni wapo wengi. Vile vile alisema kwamba kazi ya serikali sio kutaja majina bali kuwashughulikia wahalifu waliothibitika kuhusika moja kwa moja.

Je, hii aibu ya serikali ni kwa wahusika wa madawa ya kulevya tu? Mbona kuna baadhi ya watu wamewahi kukamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma mbalimbali na serikali kubwagwa mahakamani kwa kutokuwa na ushahidi wa kutosha!
Mifano mizuri ni kesi ya ugaidi ya Lwakatare na ile ya Igunga. Serikali imebwagwa kama haina wataalamu wa sheria (learned brothers)
 
Sijawahi kusikia serikali inaona aibu kubwagwa mahakamani, hivi maana ya mahakama nini kama sio mahali pa wengine kubwagwa na wengine kubwaga? what is wrong with hawa viongozi waliong'an'gania madaraka? yaani ni aibu kuwatafuta wauaji wa taifa letu? hii serikali sio tu dhaifu, ni mfu, tuna serikali mfu, hakuna serikali hapa kabisa
 
Mbona kwa Lwakatare hawakuogopa aibu kumkamata na kumfungulia mashtaka ya ugaidi bila kuwa na ushahidi wa kutosha wala kutimiza vigezo vya sheria za makosa ya ugaidi? Au aibu hii ipo kwa vigogo serikalini na baadhi ya wabunge ambao majina yao yanatoka CCM?
 
Yale majina ya wauza unga yalipelekwa kwa rais na nan? Je, ni watu wa usalama au raia wa kawaida?!

sasa kwa nini rais aseme anayo majina ya wauza unga kama hakua na uhakika kuwa ni kweli wanauza unga??
Ama tuseme alipewa majina ya washukiwa tu kisha mdomo ukatangulia ubongo?!
Hii nchi kiboko!

Yalipelekwa na mchungaji mmoja kutoka Mbeya. Nashauri huyo mchungaji atafutwe ili atoe nakala ya yale majina. About three weeks ago alilalamika ni kwa nini JMK hajayafanyia kazi hayo majina.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
kumbe wagonga meza wapo mjengoni?
kodi ya simu ni vipi hapo?

Hilo nilisikia halimo hata kwenye ratiba ya vikao vya sasa. Kwao halina umuhimu na watanzania tulivyo, tushasahau kila kitu. Wametudanganya watalijadili bunge hili lakini wamelipotezea tayari. Ni upepo tu na nadhani kwao wanaamini umeshapita tayari. Najiuliza tu kwamba ni kwa nini hatumbani (hata waandishi wetu wa habari hawatusaidii kumbana) yule aliyetuahidi kulipeleka bungeni na hajalipeleka?
 
asante umenisemea yaliyo moyoni mwangu ,ata mimi yaani namwona lukuvi kama kiere ere fulana vile wakizamani .yaana amechelewa kuzaliwa hadi kuwepo kizazi cha leo.yaani basi tuu

Huyu ndio memba wa kamati kuu ya chama cha magamba!!! Unategemea nini?
 
mkuu sifongo nafikiri hamumuelewi huyu lukuvu na wala hamulazimishwi kumuelewa swala la majina hata mm ni nayo lakin nashindwa kuthibitisha lakin sasa linapokuja swala la investigation hili swala kwa wanaofahamu kwanza ni linachukua muda inabidi upandikize mchwa kwa muda mrefu laskin ni gharama sana kwaiyo wenye ushahidi wapeleke hilo ndo swala la msingi kuliko kulumbana na kuzomea wakati lukuvi anabaki kuwa lukuvi

Nakubaliana na wewe Mkuu Chief,suala la ushahidi ndio hasa tatizo lakini kumbuka kauli ya Mh.Rais kuwa majina anayo vp nayeye alikuwa hana ushahidi au waliompa hayo majina walimdanganya Rais wetu, Serikali inapaswa kuonyesha kile tunacoambiwa kuwa ina mkono mrefu isibaki kulalamika ilhali viongozi wake waliapa kuwalinda Raia kwa gharama yoyote ile, kuna Polisi,Usalama wa Taifa,jeshi la wananchi, Jeshi la magereza, Jeshi la Mgambo na zana kibao za kutendea kazi bado wanataka Mwananchi ndio awapelekee ushahidi, sikatai kwa mwananchi kushirikiana na Serikali yake lkn Mkuu usalama wa huyu Raia utakuwa salama kweli na halai ndani ya Jeshi letu ilivyo kwa sasa?
 
Back
Top Bottom