Mbona maelezo ya huyo msemaji wa bunge yanatia mashaka sana, hamna logic yoyote hapo.
Anasema kwa kuwa Zitto ametangaza kuachia ngazi ubunge wake hivyo atalipwa mafao yake yote ikiwemo kiinua mgongo!!!
Anataka kusema Ramadhani Ally Kihiyo, Rostam Aziz, Augustino Mrema, Monica Mbega, Fred Mpendazoe ambao waliwahi kutangaza kuachia ngazi ya ubunge kabla ya muda wao kwisha nao walilipwa mafao yao yote sawa sawa na wabunge wengine?
Hii kali tena kali ya karne, yaani mfanyakazi aache kazi mwenyewe na hapo hapo mwajiri wake aseme atamlipa mafao yake yote kama mtu aliyetaafu.