Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.
"Suala la Bunge kurushwa ‘live' halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?" alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.
Source: Nipashe Ijumaa
"Suala la Bunge kurushwa ‘live' halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?" alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.
Source: Nipashe Ijumaa
Kumekuwepo na Uvumi na upotoshaji mkubwa unaoendelea katika mitandao ya kijamii hasa hapa JF kuhusu kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM ndugu Nape Nnauye.
Upotoshaji huo umejitokeza kufuatia Nukuu ya gazeti moja la kila siku la Nipashe kunukuu kauli ya Nape juu ya mjadala unaoendelea hivi sasa kuhusu kuonyeshwa ama kutooneshwa kwa Bunge la Jamhuri. Kilichojitokeza ni kuwa Mwandishi wa Gazeti hili aliwasiliana na Mwenezi kutaka maoni yake juu ya suala hilo na ndipo Nape alipofafanua kuwa hawezi kupinga suala la kuonyeshwa kwa Bunge live na kueleza kuwa tunalo tatizo la msingi la kushuka kwa nidhamu ndani ya vyombo vyetu vya maamuzi wakati mwingine lakini lazima tufikiri katika njia sahihi zaidi katika kutatua matatizo hayo bila kuzalisha matatizo mengine zaidi.
Hakuna maana wala tafakuri iliyo sawa inayoweza kukubaliana na uamuzi wa kutoonyesha bunge ili kukuza nidhamu ya wawakilishi bali ni lazima kanuni zilizopo zifuatwe na zipewe makali zaidi ya kuwashughulikia wale wenye kufanya makosa.
Ninachokisema ni kuwa tunahitaji muda zaidi wa kuonyesha bunge letu, ili kuwapa fursa wananchi kulifuatilia kwa umakini zaidi na kwa namna hiyo kuwaongezea ushiriki wao katika vyombo hivi vya kimaamuzi, lakini pia kuwaongezea hoja na vigezo vya maamuzi juu ya wawakilishi wao kwa yale wanayoyasema bungeni. Lakini pia hili la kutoonesha linakinzana na kanuni za utawala bora ambazo tunazifuata na kuzidumisha.
Hata hivyo Nape ameendelea kufafanua juu ya mjadala huo kupitia mitandao yake ya Kijamii, ambapo kwenye facebook ameeleza kama inavyoonekana chini
Nape Nnauye said:Naunga mkono juhudi za kulifanya bunge letu liwajibike zaidi kwa wananchi na kuwa na heshima zaidi. Lakini naamini kutolionyesha "live" si moja ya juhudi hizo!
Lakini ni muhimu kujadili pia muda wa kurusha bunge ambapo wananchi wengi wanapata muda wa kuliangalia badala ya utaratibu wa sasa ambapo naamini watu wengi wapo/wanapaswa kuwa kazini.
Nape Nnauye
NILICHOKISEMA ni kuwa ni vizuri zaidi bunge likipewa airtime ya ziada hasa kwa muda ambao watu wengi wanakuwa majumbani.
Wakati mwingine ni makosa yanayojitokeza kwa waandishi wetu, lakini mara nyingine hayawi makosa halisi bali makosa yanayokusudiwa.