Bunge letu si bunge tukufu

Bunge letu si bunge tukufu

Baada ya Baba kusafiri nyumba inaongozwa na Mama akisaidiana na Kaka yetu mkubwa kwa kweli sisi ni watoto wa Baba mmoja lakini Mama na Kaka yetu wanatubagua sana. Dada Leticia aliangalia picha za mbaya juzi akaja akamwambia Mama na kaka mkubwa kwamba sisi watoto wa hapa nyumbani twende kusomea namna ya kutongozana. Kaka Mwigulu alikuwa akibishana jambo na Kaka John Mnyika Mama akaingilia kati kwa kumpendelea Kaka Mwigulu ambaye alimwambia kwa kejeli kuwa wanapoongea wakubwa mtoto wa kiume anatakiwa anyamaze. Naye kaka Peter Serukamba alitoka huko kama kalewa hivi kwa kweli alipofika mlangoni tu, alianza kupiga kelele alipobishwa alitamka matusi hayo kasema "kamoni faki yu" niliwahi kumsikia Tyson akimtukana hivyo hivyo Evander siku walipopigana akamng'ata sikio. Ubishi ulikuwa mkubwa sana Kaka Juma Nkamia wakati akiendelea kusuluhisha ulitokea ubishi katikati ya mazungumzo yake alipobishwa kidogo tu basi aling'aka akasema haongei na mbwa bali anaongea na mwenye mbwa, yaani sisi ni mbwa.

Mama na Kaka mkubwa wamekuwa wakitoa maamuzi ya upendeleo sana utadhani sisi siyo watoto wa baba mmoja kaka alitufukuza tusikae pale nyumbani na mama aliporudi toka safari ameungana na kaka mkubwa kuwa tusikae pale nyumbani. Tunatamani hata kuhama hapa nyumbani lakini basi tu tukihama tutaenda wapi? Tunaishi maisha ya utukutu sana hapa nyumbani si mama, si kaka mkubwa, yaani wote ni tumegeuka watukutu. Akirudi Baba nakuja kusema yooooote!!!!
 
Baba mwenyewe katiwa limbwata na mama, hasikii wala haambiwi na mjumbe.

Mnalo!
 
Nimekuwa nikitafakari sana neno Tukufu nikajiuliza je linafaa kutumika kwenye Bunge la katiba au la Jamuhuri?. Maana ya neno Tukufu ni kitu kisicho kichafu. Mungu huwa mara nyingi anaitwa mtukufu kwa sababu hafanyi kosa. Sasa Bungeni humo kuna Mafisadi, wauza madawa ya kulevya, wabakaji, waongo na wafanyao mambo mengi yanayo fanana na hayo. Je ni sahihi kuita jina Bunge tukufu?, Au Mtukufu Rais?. Tuchangie bila jazba.
 
Linatumika kama sehemu ya mazoea tu ama kuheshimu mahali ambapo bunge hukaa
 
Wabunge wanapotoa hoja zao bungeni wanalitaja bunge hili kuwa tukufu. Mbunge akisimama utasikia 'Mh spika, napenda kulieleza bunge lako TUKUFU...'
Niwaulize wanajamii forum, hili bunge tunalolijua vyema kwa matukio lilipataje huu utukufu unaotajwa??
Kwa anayejua chanzo cha hili neno na uhalali wake kwa sasa anijuze.
 
hakuna utukufu wowote zaidi ya kuchuma dhambi mkuu,...
 
Wabunge wanapotoa hoja zao bungeni wanalitaja bunge hili kuwa tukufu. Mbunge akisimama utasikia 'Mh spika, napenda kulieleza bunge lako TUKUFU...'
Niwaulize wanajamii forum, hili bunge tunalolijua vyema kwa matukio lilipataje huu utukufu unaotajwa??
Kwa anayejua chanzo cha hili neno na uhalali wake kwa sasa anijuze.

wanajichetua tu,hao wabunge wenyewe nawadharau tu,hawana heshima,,,,,wanakazana wanapigishna picha za kuonesha nyuchi zao
 
Sijui lakin kwakuwa naamini kila mmoja ni muumini wa dini fulani,niombe tu kuhoji,hasa kwa kuzingatia maandko ya dini yako na unavyojua unadhani kwanini bunge linaitwa "tukufu"?,vigezo gani vilitumika kulitunuku sifa hio?,kwanini?

Nadiriki kuuliza kwani mim pengne naww myakubaliana namim kuwa kuna sifa yamkini zinamfaa Mungu pekee,na hasa hii ya utukufu,hata pale alipotuambia yaliyokubliwa duniani basi na mbinguni yamekubalika me sidhani kama alitupa tiketi kujipa majina yanayo mfaa yeye tu au mimi sielewi vema?

Hata hivi ni kweli kuwa bunge letu linafaa kuitwa bunge tukufu au kuna haja ya kuangalia jina jingine zaidi,na zaidi wanaoingia huko wanaitwa waheshimiwa...
 
Ni ufreemason tuu ndo umewajaa wabunge mpaka kukubali bunge kuitwa tukufu. Hakika mtukufu ni mungu tuu na si mwanadamu au sehemu fulani.
 
WABUNGE kuitwa waheshimiwa ni njama ya kujitenga kwa watumishi wengine ili wapate mishahara minono. Muheshimiwa gani serikali inakulipa mshahara mnono kwa jasho la walipa kodi .ALL WABUNGE ARE STUPID, JUST THERE FOR THEIR ECONOMICS BENEFITS.
 
WABUNGE kuitwa waheshimiwa ni njama ya kujitenga kwa watumishi wengine ili wapate mishahara minono. Muheshimiwa gani serikali inakulipa mshahara mnono kwa jasho la walipa kodi .ALL WABUNGE ARE STUPID, JUST THERE FOR THEIR ECONOMICS BENEFITS.

Unasemaje kuhusu [size=+2]Waheshimiwa[/size] Madiwani?
 
Tuliangaza zaidi bungeni,sina uhakika sana kama waheshimiwa madiwani nao wanafanyia vikao bungeni...na zaidi ni sahihi wao kuitwa waheshimiwa na je ni sahihi bungeni kuitwa sehemu tukufu(bunge tukufu)?
 
Madiwani na wabunge Lao moja, kupata maslahi minono kupitia cheo cha uheshimiwa. WABUNGE NA MADIWANI LAO MOJA KUJITENGA KWA WATUMISHI WENGINE ILI WANUFAIKE WAO.
 
WABUNGE kuitwa waheshimiwa ni njama ya kujitenga kwa watumishi wengine ili wapate mishahara minono. Muheshimiwa gani serikali inakulipa mshahara mnono kwa jasho la walipa kodi .ALL WABUNGE ARE STUPID, JUST THERE FOR THEIR ECONOMICS BENEFITS.

Mkuu ikitokea ukawa MBUNGE utajisikiaje kuitwa hivyo?
 
Back
Top Bottom