Well me i am speechless coz honestly speaking sijapata hassa jina linalostahili kuitwa hili Bunge maana nahisi kuliita tukutu,butu mafisadi yooote mmelipendelea sana maaana mie nahisi kama bunge la mashetani ambalo halipendi wasiokuwa mashetani na wakigundua kuna binadamu , wanafanya ushetani wao ili kumuangamiza huyo binadamu
lakini itafika wakati dua zetu wananchi na vilio vyetu VITAMFIKIA MOLA WETU na hao mashetani wote wataangamizwa wabaki binadamu kwenye bunge letu. MUNGU TUKUBALIE DUA ZETU
Sioni sababu ya kuwa bunge Tanzania. Hili ni kundi la watu linalokutana kupoteza muda na mapesa ya watanzania. Ni kundi linalotutia hasara kubwa kila mwaka. Bunge linatakiwa kuwa wawakilishi wa wananchi kwa serikali. Linatakiwa kupeleka kero, malalamiko na matakwa ya wananchi kwa serikali na wakati huohuo linapaswa kulinda na kutetea masilahi ya wananchi na taifa. Bunge letu hapa Tanzania ni kituko, kwani linatenda kinyume na majukumu yake.
Bunge linatakiwa kuwa na meno/makucha makali kuliko serikali. Linapaswa kuiambia serikali ukweli bila kuogopa wala kutishwa. Lakini kama tuna bunge linaloiogopa serikali na kutishiwa na serikali nalo likatishika, sasa kuna haja gani ya kuwa na bunge?.
Serikali inafanya itakavyo na inawapa wabunge majibu itakavyo na bado wabunge wanakubali upuuzi huo kwa kushangilia bila aibu wala soni.
Tumeona wazi kwamba bajeti ya mwaka 2009/2010 haikuwa nzuri ama haikuwa na faida kwa mtanzania wa kawaida, na baadhi ya wabunge waliliona hilo, wamejaribu kulipigia kelele ile kutishwa kidogo tu wamefyata mkia na kukubali kupitisha bajeti hiyo. Kama wewe ni mbunge ambaye umetumwa bungeni na wananchi wa jimbo lako, kama unaona jambo fulani ni baya ama halina faida kwa wananchi kwanini ukubali lipite?. Ni bora kusimama katika ukweli na kulikataa hilo jambo kwa gharama yoyote ile.
wanaogopwa kufukuzwa toka CCM, kwani walizaliwa na CCM?. Bila CCM hawawezi kuishi?. Ni bora kufukuzwa CCM lakini unasimamia ukweli na bila shaka hata huko jimboni kwako wananchi watakuelewa, watakuthamini na hata ukiamua kugombea ubunge kwa tiketi ya chama kingine ni lazima utapita, wananchi hawachagui chama bali wanachagua mtu mwenye uwezo wa kuwawakilisha kunako husika.
katika suala la TICTS, wananchi tuelewe nani mwenye nguvu?. Wabunge kwa pamoja kabisa mliona TICTS ni mzigo na ni lazima kuiondoa pale Bandarini lakini mpaka sasa ni mwaka hawa jamaa wa TICTS bado wapo na wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.
Wabunge mnafanya nini huko bungeni?. Kwa upande wangu naona ni bora kutokuwa na bunge kwani tutaokoa pesa za wananchi wa Tanzania.
KATIKA HILI ZITTO KABWE YUKO SAHIHI KABISA NA KWAMBA BAADA YA OFISI YA SPIKA KUWAGAWIA WABUNGE NAKALA YA MUSWADA WA MOI SASA KILA MBUNGE ARUDI JIMBONI TUKASHAURIANE KWANZA TENA BILA KUKOSA!!!!
Katika hili mchangon wa Mheshimiwa Zitto IKO SAHIHI KABISA.
Kiukweli nawaasa Wapiganaji, tusiwe wanafiki kwamba kama hatukubaliani na Zitto juu ya mambo kaadha, sawa na mimi nisivyokubaliana naye juu ya mambo mengi, basi hata pale anapotetea msingi unaokubaliana na matakwa yetu kama Umma wa Tanzania (na wala si kutetea msingi wa mafisadi) basi sisi ni kukimbilia tu KUMWAGA MAJI NJE PAMOJA NA MTOTO NDANI YA BESENI.
Kimsingi kabisa, ni kwamba mara baada ya ofisi ya bunge kuwagawia kila mbunge nakala ya mswada wa CCM basi sasa ni muda muafaka kwa KILA MBUNGE KURUDI JIMBONI KWAKE KWENDA KUSHAURIANA NA MABOSI WA (Sisi Wapiga Kura) juu ya aina ya muswada uliowashilishwa bungeni, maana na mantiki yake, kwa kiasi gani inavyowakilisha maoni yetu.
Tena ni kwamba hadi hapo sasa SISI KAMA WAPIGA KURA TUNAMPA MHESHIMIWA MBUNGE WETU UJUMBE GANI WA KWENDA KUCHANGIA KULE bungeni pindi mjadala utakapoanza; yaani ni kwamba tutakuwa tunamwelekeza mbunge wetu juu ya kitu gani akiunge mkono, kipi kirekebishwe vipi na mambo yapi akayakatae moja kwa moja.
Hakika alichokisema Mhe Zitto endapo haitozingatiwa na Wabunge kudiriki kushiriki mjadala wa HUU MUSWADA BATILI WA CCM bila kwanza kuomba maelekezo ya wapiga kura basi mjue ya kwamba WABUNGE WENGI SANA WATAKAOPINGANA NA UMMA basi ni dhahiri kwamba kibarua chao kitaota mbawa.
Huu mswada, kwa watu makini na wadadisi wa mambo watagundua kwa AG Werema kaudesa kutoka kwa MUSWADA WA MOI WA KENYA enzi hizo alipojitia kicha ngumu kukubali wananchi wake kujiundia katiba mpya. Leo hii Moi hayupo madarakani huko lakini wananchi wapo wamejaa tele na KATIBA MPYA kabisa kutokana na wananchi moja kwa moja sasa hivi inafanya kazi.
Jamani huu mswada wa Moi ambayo hivi sasa Kikwete Kaudesa nukta kwa nukta isipokua kafanya tu kazi ya kuingiza 'Unite Republic of Tanzania' kila mahali kwenye ile nafasi iliyoandikwa Republi of Kenya, hata kule kwa Kibaki alikoidesea Kikwete nako pia iliwahi kukataliwa na kutupiliwa mbali na kamati ya bunge inayoshughulikia mambo ya sheria na katiba na AG kulazimishwa kushauriana kwanza na wadau wote na kuingiza mapendekezo yao moja kwa moja ndani ya muswada ndio mambo yaendelee kwenye sakafu la bunge.
Na hiyo ndio siri kwa nini huo mswada muhimu sana kwa kila raia haukuandikwa kwa lugha yetu ya Kiswahili. Maswali zaidi muulizeni Msekwa aliyeenda huko majuzi kuchukua zaidi ya MOI'S UNPOPULAR FILE ON CONSTITUTION ili waje kuvijaribishia kwetu kama tutakubali.
Tumsikilize Zitto katika hili na hatua ya kufuatia ya maandamano nchi nzima kupinga huu mswada dhalimu ni kwamba maelekezo tutapeana kwa wakati na mtindo stahiki endapo kweli serikali haitoingiza maoni ya Wadau wa katiba kwenye huo muswada.
Aluta Continua!! Vijana kote nchini tukae tayari mkao wa kulikomboa taifa letu, ONCE AND FOR ALL, kutoka mikononi mwa MAFISADI endapo maslahi yao ndio itakayoonekana wa muhimu zaidi hapa!!!!!!!!!!!!
Naona safari ya kamba kukatikia pabovu, baada ya kuibiwa sana kura zetu, kudhalilishwa sana kimaisha na MAFISADI, baada ya kulaghaiwa sana na na vingozi wa CCM, ndio huu!!!!!!