Jana niliweza kufuatilia mjadala uliokuwa unaendelea bungeni, kimsingi Nidhamu iliyokuwa ikionyeshwa na baadhi ya wabunge na lugha ambazo walikuwa wanazitoa kwangu mimi zimenivunja moyo sana kutokana na heshima niliyoiweka kwa bunge letu na wabunge kwa ujumla. Bila kuficha mheshimiwa spika kama atakuwa anaruhusu mijadala ya bunge itawaliwe na lugha na mazingira kama ya jana basi sitashangaa kuona bunge letu likigeuka ukumbi wa masumbwi na hivyo kuondoa kabisa ile sifa inayosemwa kuwa tanzania ni kisiwa cha amani. Sikutegemea hata siku moja kuona lugha za mtaani zinatolewa na wabunge kwa uhuru kiasi kile, kiti cha spika sidhani kuwa kiliruhusu kupewa heshima yake kitu ambacho nimeona ni dosari kubwa na kipekee sitaki kuamini kuwa ile ni dharau kutokana na ukweli kuwa watanzania tuna ustaarabu wetu ambao ni tofauti kabisa na mabunge mengine. Niliochokiona jana ni uhasama na chuki za wazi kati ya wabunge na wabunge pia kati ya vyama vya upinzani hii ni dalili mbaya sana kwani kama mambo yataendelea vile basi watanzania tumekwisha. Nina imani kubwa na uwezo wa mheshimi spika ni wakati wake kuwadhihirishia watanzania kuwa anaweza!!! Watanzania hatutaki kusikia lugha za kejeli na dharau, tunachotaka ni lugha yenye suluhisho la matatizo yanayotukabili watanzania sio kejeli, vijembe na lugha za mipasho!!