Spika na naibu wake hawajui wajibu wao, Aibu ya kumuondoa Sita kwa hila. Hila haina fikra. Hili ni janga la taifa. Muhimili huu sasa unageuzwa kuwa chini ya serikali. Inauma sana, tuhakikishe Spika ajae hawajibiki katika chama cha siasa, tumeshajifunza.
huu uzi walipswa wauone mkuu hapa umejenga hoja na imekamilika sasa tufanyeje waione hawa watu ???Bunge ndicho chombo kikuu cha jamhuri ya muungano ambacho kitakuwa na madaraka,kwa niaba ya wananchi,kuisimamia na kuishauri serikali ya jamhuri ya muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake..... hayo ni maneno ya katiba ya JMT siyo yangu.
Wabunge wote ni wawakilishi wa wananchi wapo pale kwa niaba yetu kwa sababu haiwezekani Watanzania wote kuingia bungeni ndio maana tumechagua wachache wetu kutoka miongoni mwetu kwenda bungeni kwa niaba yetu kutuwakilisha.
Kilichopo sasa ni serikali inajisimamia yenyewe na inajishauri yenyewe kibaya zaidi inalisimamia pia bunge,bunge limekuwa kama kifaranga cha kuku na serikali imekuwa mwewe,serikali imekuwa juu ya bunge linapanga hoja ya kujadili na pia linafuta hoja ambayo hawaipendi.
Wabunge wengi wa CCM wanajiona kama nao ni sehemu ya serikali niliwahi kumsikia mbunge mmoja wa CCM(ambaye si waziri wala mkuu wa mkoa) akisema na yeye ni kiongozi wa serikali.
Kwahiyo kwa sababu bunge hili chini ya spika Makinda linasimamiwa na linashauriwa na serikali na si la wananchi basi hakuna haja ya kuwa nalo kwa sababu kuwa nalo ni kujiongezea gharama tu.tuiache serikali ijishauri na ijisimamie yenyewe kuliko kuwa na bunge la serikali.
Bunge linaonekana kuwa Bunge la vurugu nikwa sababu ya ukiritimba wa uongozi wa Bunge hasa pale Speaker's kutokuwa na ulinganifu, na kuwa na ubabe hasa kutaka wabunge wa upinzani wasionekane kama wana hoja za msingi lakini kimsingi tatizo lilopo ni jinsi ya uendeshaji wa taratibu za bunge!kwani hii yote ni mikakati ya serikali ambayo inatekelezwa na uongozi wa bunge! Na kinacholifanya sasa kila mtu alaumu Mh,Tundu Lissu anaufahamu wa sheria hivyo wanapopindisha hataki kuongopewa!Na lazima aonekane ni mwiba wa Maspeaker's Lakini kitendo cha Hamiss Kigwangala kusema CUF awanashida bungeni halina tja kwani CUF=CCMB sasa anategemea watasema nini??au Kulinganisha TLP na CDM nikama kulinganisha mtumbwi na Meli kubwa za Messina linea!!
Nikweli kabisa maana ndiyo maana walitengeneza mazingira mapema kwani walijua kambi ya upinzani imepanuka na CDM ni mwiba kwa serikali hivyo lazima watumie mbinu chafu!CCM ilitengeneza mazingira haya siku nyingi pale walipotishia kumfukuza kazi samweli sitta pale alipokuwa speaker na hawa walioko sasa wasingependa yaliyomkuta sitta yawakute nao.
unadhani tukifikia hatua ya kushushiana mangumi ndo tunaweza kuelewana na kutekeleza majukumu kwa usahihi zaidi kuliko kuzungumza kwa hoja na utulivu?Nidhamu bila haki ni ngumu..
hoja na utulivu ulishafwata sana lakini haukuzingatiwa .unadhani tukifikia hatua ya kushushiana mangumi ndo tunaweza kuelewana na kutekeleza majukumu kwa usahihi zaidi kuliko kuzungumza kwa hoja na utulivu?
sasa dada yangu; huoni zikiibuka vurugu hatimae wanaweza wakaumia wale ambao wanadhaniwa kwamba ndio wanaotetea haki?huoni itakuwa ni hasara juu ya hasara!hoja na utulivu ulishafwata sana lakini haukuzingatiwa .
ndo hivyo kwenye msafara wa mamba na kenge wapo...........bora nusu hasara kuliko hasara nzima.sasa dada yangu; huoni zikiibuka vurugu hatimae wanaweza wakaumia wale ambao wanadhaniwa kwamba ndio wanaotetea haki?huoni itakuwa ni hasara juu ya hasara!