JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,462
Bunge la Tanzania Agosti 31, 2023 limeridhia Itifaki ya Biashara ya Huduma ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) ya Mwaka 2012 ambapo pamoja na mambo mengine, itaondoa vikwazo vya kikodi na visivyo vya kikodi kwa wafanyabiashara wa Tanzania katika nchi za jumuiya hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Bunge, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuridhiwa kwa itifaki hiyo kutatoa nafasi ya Tanzania kukuza biashara na kutumia huduma za biashara kwa urahisi zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Bunge, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuridhiwa kwa itifaki hiyo kutatoa nafasi ya Tanzania kukuza biashara na kutumia huduma za biashara kwa urahisi zaidi.