Bunge la S.Sitta (Mwendokasi) Mhimili Imara si Bunge la Ndugai (Dhaifu), tunda la udhaifu limeonjwa na UVCCM

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Wana JF.

Giza Nene lenye bundi limemfunika bwana Jobo, kakutana na mabundi wasiokuwa na huruma. Haya yote ni matokeo ya kulazimisha kila kitu kiende kigizagiza kwa kukanyaga katiba. Mabundi furaha huwa wanategemea baada ya giza totolo watapata nini, kelele za atoke zilishamili sana bila kuangalia atoke kwa sababu ipi?

Bunge imara la S. SITTA yaliyotokea usingeweza kuyaona wala kuyaota, muhimili ulikuwa na nguvu sawa na wa Rais, kiasi kwamba uliwahi kumpukutisha waziri mkuu, Lowasa. Uliwahi kumwambia Rais Jk kuongeza ukali aondoe udhaifu katika kuongoza serikali, haya yote hatukuwahi kusikia vijana wa UVCCM chini ya Nape wakikemea na kushurutisha S.Sitta aondolewe wakati serikali inasurubiwa.

Bunge la Ndugai (dhaifu) lilivyokemewa na CAG, Jobo alihamaki sana akawa mbogo, CAG akaitwa kuojiwa baadae akashauri Rais ampige chini baada CAG kugoma kuondoka kama Ndugai alivyotaka, Mr Dhaifu pia akamwita Pascal Mayala kwa kushadadia hoja alizotoa CAG Prof. Assad , Ndungai alivimba kichwa sana enzi za mwenda zake, mpaka ukilinganisha clip kumi za majigambo na majivuno ndipo utajua anayekumbatia mabaya mpe muda, leo hii anawaza hatima yake CC kuchukua kadi yake iliyompa Jeuri.

Hoja yake haikuwa mbaya sana, lakini aliitolea wapi na nyakati zipi ndio shida. Mhimili huu dhaifu ulipambana sana kuua upinzani kusudi wakae wenyewe, sasa wenyewe kwa wenyewe wamekutana kama chuma kimekosa grisi.

Dr. Tulia ikiwa ukaukwaa uspika, yale uliyoyaendekeza ukiwa na mwendazake, tafadhali jirekebishe sana kwani sala za wanyonge zinasikilizwa zaidi kuliko za wanaokurundikia cheo. Kiukweli ulikuwa ufai bali kinachokulinda ni wabunge wengi kupewa ubunge wa michongo na maded mkabaki wenyewe. Kama nawe utaki haki subiri sala za wanyonge uone zinavyofanya kazi.
 
Tulia ikiwa ukaukwaa uspika, yale uliyoyaendekeza ukiwa na mwendazake, tafadhali jirekebishe sana kwani sala za wanyonge zinasikilizwa zaidi kuliko za wanaokurundikia cheo.

Kiukweli ulikuwa ufai bali kinachokulinda ni wabunge wengi kupewa ubunge wa michongo na maded mkabaki wenyewe. Kama nawe utaki haki subiri sala za wanyonge uone zinavyofanya kazi.
 
Back
Top Bottom