Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Binafsi ningependa kumuona mbunge wangu anavyochangia bungeni iwe point au pumba nipo tayari kumsikiliza sababu ni haki yangu.!
 
Ndiko tunakoelekea. Nimesikitika sana kama watapitisha hlo azimio
 
Kashilila, Mabumba, Makendæ na ****** akili zao ziko ANTICLOCKWISE
 
BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.

BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.

Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wananchi juu ya hatua hiyo.
amesahau methali isemayo mficha uchi azai
 
Haya ni mapendekezo ili wapate reaction ya watanzania au ni maamuzi halisi? Ninachjoweza kusema ni kuwa ni kiongozi dhaifu tu anayefikiria kuwa anaweza kutatua tatizo kwa kuficha kinachofanyika. Ninapenda kumshauri spika na chama chake kuwa maamuzi haya yatawauiza wao na chama chao zaidi ya vyama vya ushindani.

Ebu waende Uganda wakaangalie wanavyofanya na wabunge wanataka hata kuanzisha kituo chao cha TV ili wananchi waone halisi wanavyowakilishwa.
 
yahani mkuu katika hali hii na jitihada wanazofanya kuficha taarifa unatarajia bunge hilo hilohilo litunge sheria ya huhuru wa vyombo vya habari? Nadhan atakaye peleka hoja hiyo atazuiwa kuvuka mipaka ya mkoa wa dodoma!
amesahau ile methali isemayo mficha uchi azai
 
Nimepatwa na hasira hadi natetemeka... Ngoja ninyamaze kwanza,PUMBAVU!!
 
Interfering the right to receive news
 
Hapa naona CCM wanazidi kuchemka tu.
Ama kweli siku ya kufa Nyani miti yote huteleza.
CCM hali ni mbaya wananchi wamewachoka.
Lolote mnalofanya ni Ubatili tu ,ni kujilisha upepo.
 
wakimaliza kudhibiti bunge, wamdhibiti na jk zile hotuba zake za mwisho wa mwezi ni kero tupu, bora wazi edit kwanza kabla ya kuzirusha. Maana huwa anaongea mipasho tu.!
 
walianza kwa kukimbia midahalo ya wabunge na urais wakati wa uchaguzi mkuu 2010 sasa wanaingia na mbinu mpya ili wanachi tusijue madudu yao...lakini yote yanamwisho wake like misri tunis nk.....
 
Mh.Raisi ni ushauri wangu kwako usikubali kila kitu kinachopendekezwa bali tumia madaraka na nafasi yako kupinga mambo mengine.Mh.kwa mtizamo wangu mimi kama mwananchi wa kawaida, nadiriki kusema awamu yako imegubikwa na matukio mengi ya kusikitisha na kufedhehesha ambayo yanafanya awamu yako kuonekana ni awamu yenye udhaifu mkubwa.Mambo na matukio ni mengi ambayo yote yameishia kuzimwa bila hata aibu.Kuna kashifa na tuhuma nyingi ambazo ama wahusika walitakiwa kuchukuliwa hatua au hata kufanyiwa uchunguzi lakini kwa masikitiko makubwa mambo yote hayo yamezimwa either na serikali yako au kupitia bunge lenye wabunge wengi wa ccm na serikali yako ikionekana kufaidika na maamuzi hayo "dhalimu" ya bunge.Sihitaji kuyaorodhesha hapa kwani yanafahamika.

Mh.Raisi, kauli iliyotolewa leo na katibu wa bunge,Dr.Thomasi Kashilila, kuwa wanakusudia kusitisha urushaji wa matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya bunge kupitia TV, ndio imenifanya niandike haya nayoyaandika hapa.Mh.hata kama jambo hili liko nje ya ofisi yako,bado naamini unaweza kutumia nafasi yako kama raisi kufutilia mbali jambo hili.Hakika hili likitokea, katika awamu yako hii, basi ujue unazidi kujiongezea rekodi ya mambo ya kusikitisha na kufedhehesha chini ya uongozi wako.Hii itakuwa ni aibu ya mwaka na isiyoweza kuwa na "justification" ya aina yoyote mbele ya umma wa watanzania.

Mwisho,mh.unataka watanzania wakukumbuke kwa namna gani kama utaruhusu mambo kama haya yatokee?

Mh.hamna kitu kibaya kwa kiongozi kuwa na historia isiyoridhisha.Histori hii itasomwa hata na vizazi vijavyo.

Chukua hatua sasa!
 
Kemea spika anaeshindwa kufuata kanuni za bunge...haki haiombwi inadaiwa, na anaedai haki siku zote anaonekana anasababisha fujo...chadema kazi yake ni pamoja na kuokoa mburura kama wewe.!

acha mahaba ya kijinga wewe,...nenda kapike wakati baba zako tunaongea mambo ya maana....umetoroka mirembe
 
... Tanzania tunarudishwa enzi za ukoloni. Ili halikubaliki. Wananchi tutanyimwa haki yetu ya msingi.
 
unajua kama una akili timamu huwezi shabikia eti bunge lisionyeshwe live. sasa hv tu bunge linaonyesha live lkn kwenye taarifa ya habari vitu vinahaririwa sana na tena kuwapiga mkwara baadhi ya taarifa zisirushwe je itakapopita hii hoja si ndio itazidi. kuna vitu vingine tusitie siasa sana. amkeni usingizini jaman nyie magamba.
Tumechoka na ze comedy.

 
wakimaliza kudhibiti bunge, wamdhibiti na jk zile hotuba zake za mwisho wa mwezi ni kero tupu, bora wazi edit kwanza kabla ya kuzirusha. Maana huwa anaongea mipasho tu.!

na wale wabunge ambao mwanasheria mkuu alisema wanatumia vichwa kufuga nywele badala ya kufikiri
 
Back
Top Bottom