Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

m
BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.

BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za ms

Dr kilaza mwingine !!!mwenye CV yake aweke hapa aiseee
 
kama hiyo taarifa ni ya kweli basi kifo cha CCM kimekaribia.
 
Mwisho wa siku haki itajulikana tu hata mkificha na kuacha kuonyesha watatoka humo ndani watasema jinsi hali ilivyo.Mbona Deo watu wanamkubali? hayumbishwi kama wengime
Hata msiposema na kuficha mawe ya bunge yatawaambia Watanzania madhambi yenu ndani ya jengo hilo ila
IKO SIKU
 
Kwakweli bunge lilipofikia si kuzuri,ikiwezekana livunjwe twende kwenye uchaguzi ili tupate wabunge na viongozi wapya.
 
aibu kwa demokrasia, aibu kwa utawala bora....aibu kwa ccm.

aibu hii na nyinginezo zitaendelea kwa muda mpaka tutakapo amua kamataifa kuondoa makapi ya vihiyo wote wanaojita ma dr. Bila kukanyaga darasani! Dr kashirila, dr. Dr makanyagio, dr. Kj na wengine wengi. Hawawezi kujenga hoja silaha yao kuchakachua. 2010 walikimbia midahalo leo wanataka kujificha bungeni wasionekane. Aibu kubwa
 
una ccmophobia wewe. Huwezi kuandika maneno matatu bila kuitaja. Uhuni tunaoushuhudia wa watu wazima bungeni ni bora uchujwe kwanza

unaongelea uhuni gani,? Wa makinda kuminya kanuni za bunge, au wa Ndugai kunywa viroba kabla ya kuingia bungeni au wa Kigwangala kuleta hoja ya kutongozea kura 2015.?
 
Yani ni kitu ambacho hakiwezi kukubalika hata kidogo kwa sababu bunge ni baraza la wananchi au haelewi chimbuko la bunge ni nini, na hakuna mtu anayetoa pesa zake mkononi kuwezesha bunge kurushwa ni kodi zetu ndio zinazofanya kazi na ni haki ya msingi kabisa ya kila raia kujua in timely manners kuelewa kinachoendelea bungeni during session, so sijamwelewa Kashilila anaanzia wapi na anapata wapi hyo nguvu ya kuzuia bunge kurushwa live na km nani au labda mm ndio sielewi wandugu.


Naombeni watanzania wote tuwe makini na hii kauli sababu hawa wabunge wanaopingwa na arguments zao ndio wamesababisha mabadiliko na kupunguza idadi kubwa ya kodi yetu kuendelea kutafunwa na wachache.

Jamaa anajichanganya na kusema kuwa ndani ya bunge wanatofautiana wakitoka nje wanaelewana sasa sijui yy alifkiri sisi tuliwatuma wabunge wakajenge chuki miongoni mwao huko dodoma.

Anashindwa kuelewa kuwa ni demokrasia inayokamaa vizuri pale watu wanapotofautiana kimtazamo juu ya jambo lenye maslahi ya taifa. Wabunge wako pale kuwakilisha public interest na sio personaL interest.
 
U can only fool some people sometimes but u cant.......
 
Kushadadia upumbavu nawe unakuwa mpumbavu!! Suala la kuvunja kanuni za Bunge halina uhusiano kabisa na vikao kuoneshwa LIVE bila chenga. La kama wanaona wanaumbuka basi wao ndio wafuate kanuni na si kuburuza watu kana kwamba hawajui wakisemacho.

Tatizo tulilonalo hapa ni kutokana na kuwa na wabunge wengi ambao ni bhurura vichwani ukilinganisha na wachache wa vyama vya upinzani ambao wamejaa kitabu.
 
BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa
kurusha matangazo ya moja kwamoja
kupitia televisheni kwa madai ya
kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge
kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu
kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba
tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge
Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam
wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya
kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa
kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa
baadhi ya wabunge ambao wamekuwa
wanashindwa kufuata kanuni za bunge na
kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu
kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa
kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa
moja badala yake watarekodi ili kuondoa
hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya
wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za
bunge makusudi na kusababisha kuleta
vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea
kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za
msingi.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa
kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo
zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati
hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo
limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.
Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile
ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa
na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya
wananchi juu ya hatua hiyo.
Mwisho.
ningekua mtoto wa KIKWETE ningemkana babangu,kwasababu hana akili..alaf tatzo lake hana aibu ya upuuz anaofanya..

Sasa haya natusi yanahusikaje na Wabunge kuzuiwa wasijishebedue mbele ya luninga?
Kikwete na mtoto wake hawaingii Bungeni, Mbunge mmoja anataka hoja yake ipitishwe na yeye aonekane kutwa nzima akichangia leo wakikataza ni mitusi mpaka wasiohusika
 
Ni uamuzi mgumu lakini pia ni tabia mbaya na ya kitoto kufanya fujo bungeni
 
Nafikiri ni haki ya kila mmoja wetu kuona na kusikia kinachoendelea bungeni. Anachokifanya huyu Katibu ni kupora haki ya msingi ya Watanzania. Ni jukumu letu (kila mmoja wetu) kudai na kulinda haki hii. Kama kuna Wabunge wanavunja Kanuni za Bunge (Wakiwemo Spika na Naibu Spika), wabunge hao waadhibiwe ipasavyo. Hakuna kingine bali huu ni mpango wa Spika na chama chake wa kutofuata Kanuni kwa kiwango ambacho hakijapata kufikiwa. Hovyo sana. They are not learning.
 
Kutoonyesha live ni mbinu ya kuficha maovu yao. Wanataka kuonyesha yale wanayoyapenda tu na wasioyapenda watawala yasioonekane kwa wananchi, lakini mficha maradhi kilio kitamuumbua. Binafsi naona ni ujinga wa kanga kuficha kichwa kwenye mchanga huku kiwiliwili kikiwa nje akidhani moto ukija atapona. Msuguano wowote huleta maendeleo. Anachojaribu kufanya Kashilila kuacha kuonyesha lakini hazuii msuguano wenyewe. TV sio root cause of the problem. Tatizo ni namna gani kanuni za uendeshaji wa Bunge zinafuatwa. Namna gani haki inatendeka kwa wabunge wote bila kujali vyama. Katibu wa Bunge Tomas Kashilila naye anaangukia kwenye tatizo lilelile la Anna Makinda. Ni sawa na Nurse anayeosha kidonda juujuu huku akiacha usaha unapwita ndani. Nurse wa jinsi hafai kwa kuwa kidonda hakitapona.
Kwa nini Spika anayepindisha kanuni za Bunge asionekane kupotosha jamii bali Mbunge wa Upinzani anayepinga kuonewa aonekane ni mtomvu wa nidhamu na ni mfano mbaya kwa vizazi vyetu. Maadili hayana chama tawala wala cha upinzani.
Hivi madaraka ya kuwanyima habari sahihi wananchi wa Tanzania, Katibu wa Bunge kapewa na nani?
Katibu wa Bunge Dr.Kashilila amesema wanaandaa utaratibu ili lisiwe likionyeshwa live badala yake litakuwa likirekodiwa na kuhaririwa,ndipo wananchi waweze kufahamu kilichoendelewa bungeni siku hiyo.source taarifa TBC1 saa 2 usiku
 
Viongozi wa ccm bana,sasa msiporusha live ndio mtakuwa mmetusahaulisha wananchi jinsi ambavyo mmezisigina hoja zetu za msingi Bungeni?Sijui ni ulevi wa madaraka au ni ujinga wa wananchi(walioichagua Serikali hii)kukaa kimya hata kama wanalazimishwa kukaa giza/kuoga na maji sadolini moja/kujifungulia vichakani/elimu mbovu/wizi wa raslimali zetu/kufa kwa kukosa dawa,nnahisi kuchoka..Nchi hii imekuwa ya ajabu sana yaani kila mmoja ni"kiongozi".
 
Back
Top Bottom