Buhohela analipwa na ITV, Magufuli au CCM?

Buhohela analipwa na ITV, Magufuli au CCM?

Anatembea na MAGUFULI kila mahala anapokwenda na anaripoti habari zake kwa bashasha kubwaa.. Ni utaratibu gani huu??

aliyeripoti jana mkutano wa CHADEMA naye analipwa na CHADEMA au Tundu Lissu au Lembeli, ache umbulula.
 
haya maswali hata mm nimejiuliza sana. Wakati yupo mwanza akasema eti anasema kwa nyomi hii ya watu ni ishara kwamba nyumbani wamabaki kuku tu.

Kauli hiyo niliishangaa sana.
 
Ninanusa harufu ya waandishi wengi wa habari kununuliwa na kambi ya Magufuli.
Hapo kampeni bado hazija anza.
Mengi kusoma mchezo mapema., target yake ni vitalu tu vya gesi.

we unadhan ITV wanakurupuka tu wanajua nin wanakifanya uo ndo UHURU WA WAANDISHI WA HABARI. Ndorooooobbboo
 
Soon lazima afukuzwe kazi.... Aende huko Radio Uhuru...

Tutampa nafasi ya Salva Rweyemamu, acheni nongwa na Buhohela subirini tukamilishe ratiba ya uchaguzi tu atakuwa Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu.
 
Ngoja tukianza kusikia za lowasa au the so called ukawa utuambie analipwa na nani. Nasema hivyo maana alitangaza naanatangaza kuwa atatuletea vipindi kama hivyo kwa wagombea wote wa urais.

Tuache giliba na ubinafsi wa kupenda kusikia ya kwetu tu. Na ndiyo maana hatuendelei
 
Anatembea na MAGUFULI kila mahala anapokwenda na anaripoti habari zake kwa bashasha kubwaa.. Ni utaratibu gani huu??

Kwani wewe unataka aripoti kwa huzuni? Yeye ni mwandishi na aripoti kwa namna ambavyo anapaswa ili kuitendea haki taaluma yake.
Pia, kwa nini huwasemi wale wanaoripoti habari za lowassa? Ambao wanaongeza na chumvi nyingi hadi kuanza habari kwa ku-quote speech za nyerere? Huko sio kufanya kampeni?
Au ndo msemo wa waswahili kwamba nyani haoni kundule?
Ifike mahali tuache ushabiki wa kiitikadi na tujadiri hoja kwa hoja.
 
yawezekana kanunuliwa....mbona kawaida yao hiyo hasa kipindi cha uchaguzi kinapofika
 
Nimekufatilia namna yako ya kuripoti shughuli uliyo kuwa assigned yaani msafara wa mgombea wa CCM na kugundua unachofanya sio sahihi kulingana na maadili ya kazi yako na heshima ya kituo unachowakilisha.
Unatia chumvi sana na kudanganya wazi nahisi unapata malipo ya ziada toka mahali na hiyo ni rushwa.

Nikupe mfano mmoja, Leo Magufuli alikuwa na tatizo la sauti, hiyo ni kawaida kutokana na mikutano mingi na kutumia nguvu kubwa jukwaani. Lakini ulivyo muongo na bila aibu ukawaambia watazamaji eti kuna jambo anasisitiza kwa sauti ya upole kuonyesha msisitizo wa jambo!

Huo ni uongo, sauti imekauka na una tabia ya kuongeza maneno yako hata kama hayajasemwa. Tutaondoa imani kwa ITV kama ripota wao wanaanza tabia za kutiliwa shaka kujihusisha na rushwa. Nakumbuka hata kipindi cha Dakika 45 kulianza kuwepo hisia chafu dhidi yako.

Jirekebishe
 
Nimekufatilia namna yako ya kuripoti shughuli uliyo kuwa assigned yaani msafara wa mgombea wa CCM na kugundua unachofanya sio sahihi kulingana na maadili ya kazi yako na heshima ya kituo unachowakilisha.
Unatia chumvi sana na k udanganya wazi nahisi unapata malipo ya ziada toka mahali na hiyo ni rushwa.
Nikupe mfano mmoja, Leo Magufuli alikuwa na tatizo la sauti, hiyo ni kawaida kutokana na mikutano mingi na kutumia nguvu kubwa jukwaani. Lakini ulivyo muongo na bila aibu ukawaambia watazamaji eti kuna jambo anasisitiza kwa sauti ya upole kuonyesha msisitizo wa jambo!
Huo ni uongo, sauti imekauka. Na una tabia ya kuongeza maneno yako hata kama hayajasemwa.
Tutaondoa imani kwa ITV kama ripota wao wanaanza tabia za kutiliwa shaka kujihusisha na rushwa. Nakumbuka hata kipindi cha Dakika 45 kulianza kuwepo hisia chafu dhidi yako.
Jirekebishe
Wote wanafanya higyo. Hata Asraj (anayeripoti kampeni za CHADEMA) naye anafanya yaleyale ya Buhohela. Ndivyo waandishi wetu walivyo na yote hii ninhayo malipo ya pembeni wanayopewa na vyama!
 
Back
Top Bottom