data
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 26,943
- 23,885
Anatembea na MAGUFULI kila mahala anapokwenda na anaripoti habari zake kwa bashasha kubwaa.. Ni utaratibu gani huu?
Nimekufatilia namna yako ya kuripoti shughuli uliyo kuwa assigned yaani msafara wa mgombea wa CCM na kugundua unachofanya sio sahihi kulingana na maadili ya kazi yako na heshima ya kituo unachowakilisha.
Unatia chumvi sana na kudanganya wazi nahisi unapata malipo ya ziada toka mahali na hiyo ni rushwa.
Nikupe mfano mmoja, Leo Magufuli alikuwa na tatizo la sauti, hiyo ni kawaida kutokana na mikutano mingi na kutumia nguvu kubwa jukwaani. Lakini ulivyo muongo na bila aibu ukawaambia watazamaji eti kuna jambo anasisitiza kwa sauti ya upole kuonyesha msisitizo wa jambo!
Huo ni uongo, sauti imekauka na una tabia ya kuongeza maneno yako hata kama hayajasemwa. Tutaondoa imani kwa ITV kama ripota wao wanaanza tabia za kutiliwa shaka kujihusisha na rushwa. Nakumbuka hata kipindi cha Dakika 45 kulianza kuwepo hisia chafu dhidi yako.
Jirekebishe
Wakuu, Emanuel Buholela ni mwanahabari wa ITV, akiripoti kampeni za Magufuli.
Ni kijana machachari mwahabarishaji, lakini leo nimemtolea point zangu nilipomsikia akitatangaza habari ya Magufuli kuvunja record Mwanza na sehemu nyinginezo za kanda ya ziwa!! Hii si kweli.
Mwitikio wa watu haupo kama wanavyosema.
Watu wa CCM bado kujaza.