Mnakosea sana wasomi kubwabwaja mambo bila udadavuzi.
Hao wanaotaga mayai ya kutotoleshea vifaranga, lazima "wagongwe' na jogoo ili yai liweze kutotolewa, vinginevyo haiwezekani.
Broiler wanachomkosea, hatokoswi supu ni kwa ajili ya kukaangwa tu, nyama yake ni teketeke mno.
Ukishamzoea hutataka kuku wengine.
Halafu watu wengi wanalishwa broiler kwa ajili ya brand ya jina 'kienyeji' lakini si wa kienyeji.
Kuku wengi Dar ni wa kisasa (chotara) huwezi jua kama siyo mfugaji, maana wanafanana sana sura na kuku wa kienyeji na wanaitwa wa kienyeji kwa ajili ya mahitaji ya soko.