Dejane
JF-Expert Member
- Jan 1, 2014
- 51,088
- 72,505
Umeniwahi
Sio wanaume tu
Nina rafiki zangu wawili ni wachafu wa mazingira balaa, wanaoga wanavaa wanapendeza nje utasema wanaishi masaki!! Ukiingia room kwao aisee, nguo zimejaa kabatini zimerundikana mpaka zimemwagika chini yani ukiingia unakanyaga nguo , kitanda shuka halijulikani hapajatandikwa pana mwezi shuka chafuu! Madirisha machafu kajaza chupi! Vipodozi vingine vipo kwenye dressing table ina vumbi mno halafu vimefunguliwa havijafungwa viko hovyo hovyo tu! Kama kuna viti vipo vipo tu halafu haoni aibu walaaa, kaamka asubuhi kaswaki, kanywa chai anachati kutwa nzima anashindwa hata kufanya usafi!![emoji22] juu ya neti kumejazwa nguo chafu
Wapo aisee kuna mmmoja alikuja kwangu hali ya hewa ilibadilika nakuambia baadhi ya
Watu ni wachafu usafi kwao ni tabu