Huyo amelelewa katika mazingira ya kudekezwa kila kitu afanyiwe na house girl au mama yake. Yaani hakufunzwa kuwa msafi tokea mtoto sasa jaribu njia hz pengine utamsaidia..
Chumbani kwake tenganisha nguo safi na chafu. Kama ana kabati la nguo kunja vzr nguo zake na umewekee kila ina ya nguo sehemu yake. Kisha uweke tenga la nguo chafu alafu una lebel na pen "nguo chafu"
Mnunulie shoe rack panga viatu vyake vizuri. Weka kitenga kidogo au box kisha lebel "soksi+boxer+ handkachif"
Pia ondoa meza chumbani ambayo inamuhamasisha kulia chakula chumbani. Ama kama kuna kochi, tv ondoa peleka sebuleni ili kumkosesha sababu ya kula chumbani.
Nunua dustbin weka sebuleni lebel "takataka" ili hata akimaliza kula ndizi aone sehemu ya kutupa.
Jaribu ku organize kila kitu chake in order alafu weka maelekezo kwa ku lebel tu. Na ktk kila lebel weka "i love u" ili asione kama unamshurutisha au umempangia sheria nyumbani kwake.
Hapo kwny kuoga sasa ndo mpaka aamue mwenyewe aisee [emoji4]