Botswana imeniingia Akilini

Botswana imeniingia Akilini

MfalmewaKiha,
Kama utakua na mtaji wa m10..kwanini usiangalie fursa sehemu nyengine mbali na ulipo?unajua watu wengi mnawaza maisha yapo dar tu...kwa mshiko huo nakuhakikishia kama utachanganua akili vizuri hapa hapa unafanya vizuri na Botswana utaenda kutalii tu...
 
Nijuacho mimi.hapa Tanzania mtu mwenye bidii,maarifa na mipango mizuri ya kiutafutaji hasa kupitia ardhi tuliyonayo anaweza kufanikiwa pakubwa kuliko hata kuanza kukimbia kimbia nyumbani mwa watu.waTanzania wengi sana wanapenda kuidharau nchi yao na kuzisifia za nje hata kama amesikia tu maneno vijiweni na kuanza kurusha maneno asiyoyajua.imepelekea watu kufanya mipango ya kuhamia nje ya Tanzania na kweli wanafanikiwa wanaenda kisha huishia kurudi na mikogo tu ya kutembea na miwani za jua huku wakidanganya watu kwa muonekano wa mavazi kuficha aibu lakini hawana kitu.tumieni ardhi kuilima na kufuga mtafanikiwa.waliosema zamani wazee kwamba mkitaka mali mtaipata shambani msidhani walidanganya,tatizo ni hizi elimu mnazopata zenye misingi ya kigeni zisizoandaa watu kiakili kujitegemea.lakini ukiweza kuchanganya akili unayaona maisha mazuri hapa hapa nchini,potezea maneno ya wanasiasa wenye kuvunja moyo kwa kuikashifu nchi yetu na upigane na maisha kwa bidii utafanikiwa.milion 10 unayoiwaza kuendea Botswana itumie hapa hapa bila kuingia gharama za nauli na kupanga nyumba kule then unaishia kua na mataji wa milion 5 ambayo itakusumbua tu. Success is at your feet


JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Hivi huko naweza kufuga kuku,nguruwe,samaki na nng'ombe kweli???
Bora nibaki bongo tu...ardhi ya kumwaga
Yaan nipo maeneo fulan ya moro, heka ya kulima kukodi elfu 50 tu

Sasa hapo laki 5 tayari una hekari 10 za kuanzia
 
Yule mdau aliyekuwa anajiita "Shibe kijijini" aliaga hapa kwenda South kupitia Botswana anapatikana? Maana aliishia mrejesho wa safari yake katika mpaka wa Botswana na South Africa...angekuwa msaada kwako japo sehemu ya kuanzia.
Huyo atakuwa yuko either jela, au karest in peace
 
Yap! Ndivyo ilivyo mkuu
Kuna kaform flani kakijinga pale immigration unakajaza
Unaenda wapi
Kwa nani
Address yake
No yake ya simu
Yaani wasumbufu sana bila kujaza kikamilifu hiyo watakusumbua sana...Kwa hiyo unahitaji mwenyeji akupe details zake ili uzitumie pale immigration
Tunaotaka kwenda Botswana hilo tulijue wote View attachment 733071

renegade
 
Botswana ni nchi nzuri sana na ina uchumi mzuri sana. Kwa upande wa kufungua saloon, sikushauri. Zipo nyiiiingi na waenzetu wanatumia vijereta vidogo pembezoni standi kuu. Nunua vitenge vya Java na vitambaa vya nguo vinaweza kukusaidia ukapata pesa za kujikimu wakati ukitafuta biashara. Niliwahi kuzunguka na kuangalia ni kitu gani kinachokoseka na Gaborone na Tanzania kinapatikana kwa wingi, nikagundua bidhaa za nguo kule ni ghali sana hasa vitambaa vya nguo kama Java.
MfalmewaKiha,
 
Kama wazo lako ni kuhamia Botswana kwaajili ya kwenda kutafuta maisha..... Basi nioni kama kuna sababu ama ulazima was kutafuta mtu wa kuungana nae kwenye Safari yako hiyo.
Kubwa ambalo pengine ungeomba wadau wawakusaidie hapa ni:-
1. Kujua njia zipi ambazo unaweza kusitumia ili ufanikiwe pasipo kuongia matatani ikiwa utaamua kwenda Botswana.
2. Kujua miji ipi ambayo ukienda inaweza inawa kwako ni rahisi kuishi na kupata mafanikio kwa ushirikiano wa wenyeji wa kule.
3. Kujua aina za changamoto na tabia za waSwana, ili kwako ikuwe rahisi kuendana nao kimaadili nk....
Kila lakheri boss!!!!
1.-Kuwa mwangalifu na sida
2.-control mfadhaiko(mavazi yao hasa watoto wa shule) wana miguu!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom