macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 22,187
- 40,453
Siku hizi kuna nyuzi nyingi zinafunguliwa na members kujaribu kuonyesha elimu ya darasani haina faida. Mtu ukifikia hatua ya kuona elimu uliyosoma darasani haikusadii na ulipoteza muda bure basi ujue ulienda shule kukariri ili ushinde mtihani na hukwenda kuelimika. Na hili liko sana kwenye shule nyingi za Tanzania.
Nadhani mfumo wetu wa elimu ni mbovu haswa ndiyo maana watu wanamaliza mpaka chuo kikuu lakini hawana tofauti na walipomaliza darasa la saba. Muda wote kuanzia sekondari mpaka chuo kikuu walikuwa wanakariri ili mtihani ukija wafaulu vizuri. Mimi nimemaliza degree na shughuli ninazofanya ni tofauti kabisa na vitu nilivyosoma lakini sijawahi hata siku moja kujuta ni kwanini nilisoma.
Nadhani mfumo wetu wa elimu ni mbovu haswa ndiyo maana watu wanamaliza mpaka chuo kikuu lakini hawana tofauti na walipomaliza darasa la saba. Muda wote kuanzia sekondari mpaka chuo kikuu walikuwa wanakariri ili mtihani ukija wafaulu vizuri. Mimi nimemaliza degree na shughuli ninazofanya ni tofauti kabisa na vitu nilivyosoma lakini sijawahi hata siku moja kujuta ni kwanini nilisoma.