Bora kutumia akili ya kuzaliwa nayo kuliko Elimu ya makaratasi

Kategele

JF-Expert Member
Oct 7, 2017
971
2,233
Ni miaka imepita tangu nihitimu hii elimu ya makaratasi nimegundua kumbe ilikuwa mahususi kwa kuajiriwa na kunifanya niwe mtumwa wa kazi za wengine.​

Serikali Mungu anawaona mumeandaa mtaala wa kutumia muda mwingi shuleni, jamii nayo ikaaminishwa kuwa kusoma na kupata vyeti ndiyo kufanikiwa kumbe mlitupofusha ili tusione fursa mtaani.​

Haiwezekani Leo na elimu yangu nikiingia pale kariakoo naonekana Kama darasa la saba,wakati kuna watu hawana elimu ila ndo wamiliki wa machimbo yote ya biashara wanapiga pesa balaa.​

Kuna watu walishituka mapema wakaingia mjini kufanya mishe wako mbali Leo nakutana nao ndo naanza kufanya training ya kujua machimbo ya biashara!​

Ewe muhitimu mwenzagu nakupa ushauri shituka mapema usikalie kusambaza Cv tu Kuna fursa zipo mtaani sema elimu yetu haitusaidii zaidi ya kututoa kwenye ushamba nakutupeleka kwenye ujinga pia kutuacha hapo kwenye ujinga.​

Elimu ya makaratasi kwaheli naanza kutumia akili yangu ya kuzaliwa.​
 
Pole sana..ila tambua kuna watu wanajuta kwanini hawakusoma...wanatamani warudi shule..ujinga ni kushindwa kuona fursa kupitia elimu uliyoipata...kuna wadau wanaliwa pesa ndefu sana kupitia elimu zao.

#MaendeleoHayanaChama
 
Shukru kwa elimu uliyonayo maana kunawanaotamani wawenayo ila walikosa fursa ya kupata hiyo elimu, Elimu uliyonayo inakusaidia katika maisha halisi ya mtaani uingie wapi utokee wapi kwenye nyanja mbalimbali hususan maofini/ kitaan/ jamii inayokuzunguka/ Familia/ inakujengea confidence ya kujiamini na kujieleza kwa ufasa bila kusua sua.
 
Tunatakiwa kusoma alama za nyakati.

Kitu chochote kinakuwa na umuhimu kama ni scarce, ila kma mtu anaweza kukipata au kukiachive kinakuwa hakina maana katika jamii.

Hii ndyo sababu hivi sasa hata msomi analipwa mshahara chini ya kipato cha chini.
 
Shukru kwa elimu uliyonayo maana kunawanaotamani wawenayo ila walikosa fursa ya kupata hiyo elimu, Elimu uliyonayo inakusaidia katika maisha halisi ya mtaani uingie wapi utokee wapi kwenye nyanja mbalimbali hususan maofini/ kitaan/ jamii inayokuzunguka/ Familia/ inakujengea confidence ya kujiamini na kujieleza kwa ufasa bila kusua sua.
Kunywa Maji popote,nitalipa bili ya mwezi nikiwepo sehemu hiyo
 
Upo sahihi kabisa

Bookish Education has zero benefits to us these days.
 
Shukru kwa elimu uliyonayo maana kunawanaotamani wawenayo ila walikosa fursa ya kupata hiyo elimu, Elimu uliyonayo inakusaidia katika maisha halisi ya mtaani uingie wapi utokee wapi kwenye nyanja mbalimbali hususan maofini/ kitaan/ jamii inayokuzunguka/ Familia/ inakujengea confidence ya kujiamini na kujieleza kwa ufasa bila kusua sua.
hao wanaoitamani ni kwamba hawajui uhalisia wake, na wakiipata hawataitamani tena, na mbona kuna namna nyingi za kupata hii elimu kama mambo yako umeshayaset...

Unadhani kishimba yule mfanyabiashara na mbunge bado ni la saba tu au msukuma?
 
Kila mtu na bahati yake, unaweza ukaichukia elimu ukasema ungefanya kama mtu Fulani kumbe usingepiga hata hatua, maisha yana siri kubwa sana kama hujui
 
Pole sana..ila tambua kuna watu wanajuta kwanini hawakusoma...wanatamani warudi shule..ujinga ni kushindwa kuona fursa kupitia elimu uliyoipata...kuna wadau wanaliwa pesa ndefu sana kupitia elimu zao.

#MaendeleoHayanaChama
wadau wa miaka gani hiyo?
 
Hivi ni kwanini serikali karibu zote zinapambana raia wake wapate elimu?

Kwanini budget kubwa uwa zinapelekwa kwenye elimu?

Kwanini elimu inapewa kipaumbele hivi?

Hii elimu ni nini? Kwanini elimu? Ina faida gani kwa mwanadamu mmoja mmoja na taifa kama sio dunia kwa ujumla?
 
Hakuna mahusiano Kati ya ELIMU NA AKILI
IMG-20200703-WA0007.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom