Itscharlie
JF-Expert Member
- Apr 15, 2022
- 3,794
- 15,773
Mwanamke mmoja katika Manispaa ya Iringa amepoteza maisha baada ya kupokea kichapo kutoka Jeshi la Polisi.
Polisi wakiwa katika zoezi la kuondoa wafanyabiashara ndogondogo katika Manispaa ya Iringa. Polisi walikuwa wanatumia nguvu kuwakata na kuwapiga baadhi ya wakina mama waliokuwa wanauza mboga na kutembeza ndizi eneo la mashine 3-Iringa.
Mwanamke huyo ambaye bado natafuta jina lake na ndugu zake kupita uongozi wa wafanya biashara amefariki baada ya kupigwa na Polisi hadi presha kushuka.
Video inaonyesha wakina mama wenzie wauza mbogamboga wakimpatia Mwanamke huyo huduma ya kwanza, muda mchache baada ya kupoteza fahamu na baadae kuaga Dunia.
Nawapa pole sana wakina mama wote ambao ni wapambanaji wa maisha kwa kupitia biashara ndogondogo.
Najua mlijua Rais akiwa Mwanamke mwenzenu huenda anajua shida zenu zaidi. Poleni.
By:Boniface jacob/twitter x